Shule 10 bora matokeo ya Kidato cha Sita: Zimo shule 7 za serikali. Wakongwe Marian Girls, Feza Boys, Kibaha Sekondari, Ilboru Sekondari watupwa mbali

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,661
18,035
Kuna mabadiliko makubwa sana katika ushindani wa matokeo ya kidato cha sita. Wakongwe waliotesa kwa miaka mingi wamepigwa mweleka mkali wakiwemo Marian Girls, Feza boys, Marian boys, Feza boys, Kibaha sekondari, Uwata sekondari nk. Je tatizo ni nini? Mkeka huu hapa:
  1. Kemebos Sekondari, Kagera - Shule ya Binafsi.
  2. Kisimiri Sekondari Arusha - Shule ya Serikali.
  3. Tabora Boys Sekondari Tabora -Shule ya Serikali.
  4. Tabora Girls Tabora - Shule ya Serikali
  5. Ahmes Sekondari Pwani - Shule ya Binafsi
  6. Dareda Sekondari Manyara - Shule ya Serikali
  7. Nyaishozi Sekondari, Kagera - Shule ya Binafsi
  8. Mzumbe Sekondari Morogoro, Shule ya Serikali
  9. Mkindi, Tanga - Shule ya Serikali
  10. Ziba, Tabora - Shule ya Serikali.
Karibuni kwa comments!
 
Labda zile zama za kale zinaanza kurudi, ngoja tuone next year kama hao wazalendo wenzangu wataendelea kukomaa hapo juu.
 
Haka kashule ka Kisimiri kako porini sana. Sijui wanafanyaje wanakuwa na matokeo ya namna hii.
Kuna mabadiliko makubwa sana katika ushindani wa matokeo ya kidato cha sita. Wakongwe waliotesa kwa miaka mingi wamepigwa mweleka mkali wakiwemo Marian Girls, Feza boys, Marian boys, Feza boys, Kibaha sekondari, Uwata sekondari nk. Je tatizo ni nini? Mkeka huu hapa
 
Haka kashule ka Kisimiri kako porini sana. Sijui wanafanyaje wanakuwa na matokeo ya namna hii.
Shule ya kisimiri ilikuwa na ufadhili mkubwa sana wa wazungu kwa A level. Mazin gira ya kufundishia na kujifunzia yalikuwa ni mazuri sana. Ndio maana wako juu. Sina uhakika kama ufadhili huo unaendelea. Serikali ilipoona inafanya vizuri wakaifanya kuwa SPECIAL SCHOOL. Ikiwa special school ikapata boost ya kupewa watoto waliofaulu sana hivyo kusaidia kubaki juu!
 
Kuna mabadiliko makubwa sana katika ushindani wa matokeo ya kidato cha sita. Wakongwe waliotesa kwa miaka mingi wamepigwa mweleka mkali wakiwemo Marian Girls...
Kwa nilivyofuatilia kidato cha sita huwa shule za serikali zinaingia sana ila kwa matokeo ya kidato cha nne shule za serikali zinaingia chache sana nyingi zinazoongoza ni shule binafsi.

Mfano
20220706_142818.jpg
20220706_142614.jpg
 
Loooo kweli dunia imekimbia sana ,hapo kwangu nakumbuka Tabora Boys &Girls sec schools na Mzumbe sec School, zingine zote ni blue tupu, wapi PCBs za Tosamaganga sec school(Dr.Sarungi record),wapi PGM ya pale Mazengo sec school?,looo wale wa PC &Educ.pale Mkwawa CNE tuonane!
 
Back
Top Bottom