barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Je, uliona harusi ya Semenya?
Hivi ndivyo mshindi wa mbio za mita 800 kwenye mashindano ya Olimpiki ya mwaka huu Caster Semenya alivyofanya harusi yake na mpenzi wake Violet Raseboya mwezi Desemba mwaka jana (2015).
Kwa mujibu wa ripoti za SA Fame Awards, bingwa huyu wa olimpiki alifunga pingu za maisha katika eneo la Ga-Dikgale, wilaya ya Limpopo..
Caster Semenya amekuwa akilalamikiwa kuwa anaweza kuwa na "jinsia mbili" na hili lilizuwa mzozo mara baada ya mashindano ya Olympic 2008 kule Beijing.Mwaka huu huko "Rio2016 Olympic" Semenya alishinda mbio za mita 800 za wanawake akifuatiwa na mwanamke toka Burundi,mwanariadha wa Uingereza katika mbio hizo amelalamika kuwa siyo haki wao kama wanawake kuweka kundi moja na Semenya ambaye sio "Mwanamke Kamili".
Je hali hii ya Semenya "kuoa" inafanya zile tetesi za kuonyesha ana "uanaume" kuliko "uanamke" zitapata nguvu?
??