Jethro
JF-Expert Member
- Mar 23, 2009
- 2,219
- 370
Wana JF,
Niko ndani ya Jiji la Arusha ila makubwa nimeyakuta hapa
Jamani wandugu, kilichotekea huku Matongee Club Arusha Jana Usiku ni aibu tuuuupu kweli kwani Jana Fally Ipupa alipaswa kutumbuiza wana Arusha,
Kiinglio Front Seats a.k.a VIP = 30,000/=Tsh and Back Seats = 15,000/=Tsh
Cha ajabu kuanzia watu wameingia saa 3 usiku kulifahamika kuwa kuna tatizo la Umeme wa TANESCO hautoshi sukuma Music system zilizopo kwenye stage na Generator ikawa ni kimeo, ikawa haiwezi fua umeme wa kutosha; kila ikiwaka na baada ya 10mins inakata hali hiyo ya kutopatikana kwa nishati ya umeme kusukuma mitambo ya muziki ilifika hadi saa 6 usiku na ndipo hapo watu wakachoka na uvumilivu ukawashinda.
Jasmine alikuwa akihangaika sana kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa pamoja na kutoka kwenda kutafuta Generator jingine huku nyuma watu wakajichukulia maamuzi yao binafsi wengi wao walibeba viti kila mtu aliye beba viti una mkuta anaviti 5 hadi 6 sio tu vya plastic (@ per sale ni 8000/=Tsh na vilikuwa ni viti 200) hata vile vya conference seat (@ per sale ni 30,000/=Tsh na vilikuwa kama viti 30) watu walibeba na kujiwekea kwenye magari yao na wale ambao hawakuambulia kitu imekula kwao, pia hakukuwa na mtu wa kuwazui hata police walikuwepo (Ndani na LandRove 110 Nyeupe) na hawakufanya chochote kwani waaandaaji walikuwa ni matapeli hawakujipanga.
Na viti vyote vilikwenda na pale getini wale watoza pesa ati walisema waliporwa pesa kumbe wao ndio walio zichimbia pesa mifukoni.
NB;
Je, Office zinazo husika za serikali kwa kutoa kibali ili show kama hizo kupigwa huchukulia vipi swala kama hili kuwawajibisha wale waandaaaji na wadhamini wa show kama kutatokea tatizo kama hilo lililojitokeza hapa Arusha?
My Take;
Hawa waandaaji kwanza watambue nini maana ya kuandaaa show za band
Wakisha andaaa wanatakiwa kujua vitu gani ni muhimu kwanza katika show vinatakiwa visipate matatizo na kuwa na plan B. Utangazaji wa Show kwa raia kwani hii ya fally Ipupa wengi walishtukizwa tu one day before.
Bifu za mapromotor zisiwepo kwani jana pia kulikuwa na wananmuziki toka Dar na Nairobi wakipiga show Tripple A; kwanini nasema hivyo, kwani kulizuka neno kuwa kulifanyika hujuma generator kutotengenezwa ili kutofanikisha show ya Fally ili watu wahamie Tripple A.
Niko ndani ya Jiji la Arusha ila makubwa nimeyakuta hapa
Jamani wandugu, kilichotekea huku Matongee Club Arusha Jana Usiku ni aibu tuuuupu kweli kwani Jana Fally Ipupa alipaswa kutumbuiza wana Arusha,
Kiinglio Front Seats a.k.a VIP = 30,000/=Tsh and Back Seats = 15,000/=Tsh
Cha ajabu kuanzia watu wameingia saa 3 usiku kulifahamika kuwa kuna tatizo la Umeme wa TANESCO hautoshi sukuma Music system zilizopo kwenye stage na Generator ikawa ni kimeo, ikawa haiwezi fua umeme wa kutosha; kila ikiwaka na baada ya 10mins inakata hali hiyo ya kutopatikana kwa nishati ya umeme kusukuma mitambo ya muziki ilifika hadi saa 6 usiku na ndipo hapo watu wakachoka na uvumilivu ukawashinda.
Jasmine alikuwa akihangaika sana kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa pamoja na kutoka kwenda kutafuta Generator jingine huku nyuma watu wakajichukulia maamuzi yao binafsi wengi wao walibeba viti kila mtu aliye beba viti una mkuta anaviti 5 hadi 6 sio tu vya plastic (@ per sale ni 8000/=Tsh na vilikuwa ni viti 200) hata vile vya conference seat (@ per sale ni 30,000/=Tsh na vilikuwa kama viti 30) watu walibeba na kujiwekea kwenye magari yao na wale ambao hawakuambulia kitu imekula kwao, pia hakukuwa na mtu wa kuwazui hata police walikuwepo (Ndani na LandRove 110 Nyeupe) na hawakufanya chochote kwani waaandaaji walikuwa ni matapeli hawakujipanga.
Na viti vyote vilikwenda na pale getini wale watoza pesa ati walisema waliporwa pesa kumbe wao ndio walio zichimbia pesa mifukoni.
NB;
Je, Office zinazo husika za serikali kwa kutoa kibali ili show kama hizo kupigwa huchukulia vipi swala kama hili kuwawajibisha wale waandaaaji na wadhamini wa show kama kutatokea tatizo kama hilo lililojitokeza hapa Arusha?
My Take;
Hawa waandaaji kwanza watambue nini maana ya kuandaaa show za band
Wakisha andaaa wanatakiwa kujua vitu gani ni muhimu kwanza katika show vinatakiwa visipate matatizo na kuwa na plan B. Utangazaji wa Show kwa raia kwani hii ya fally Ipupa wengi walishtukizwa tu one day before.
Bifu za mapromotor zisiwepo kwani jana pia kulikuwa na wananmuziki toka Dar na Nairobi wakipiga show Tripple A; kwanini nasema hivyo, kwani kulizuka neno kuwa kulifanyika hujuma generator kutotengenezwa ili kutofanikisha show ya Fally ili watu wahamie Tripple A.