SHOGA WA KIKE anataka anizalie (Nimzalishe) mtoto!

Sikonge

JF-Expert Member
Jan 19, 2008
11,550
6,062
Wakali wa JF,

Kuna dada mmoja nje ya nchi ambaye anataka kuja hadi hapa Sikonge ili nimtungishe Mimba na hatimaye azae mtoto. Huyu mdada ni mtu ambaye ninafahamiana naye kwa miaka mingi kidogo tangu nikiishi nje ya nchi ambapo siku hizo, hakuwa au nilikuwa sijajua kama ni SHOGA.

Anasema yupo tayari kuwekeana kabisa mkataba na mie kwamba gharama zote za mimba na kulea mtoto hatanidai na mtoto ataandikishwa kwa jina lolote nitakalokubali mie na hata akitaka atanilipa. Sijui kaona kitu gani cha ajabu kwa Mnyamwezi mie ingawa kiukweli hadi leo hii sijawahi hata kumbusu, acha kutembea naye.

Kuhusu Mimba anasema inaweza kuwa kwa njia ya kawaida kwa kufanya mapenzi au kwenda hospital na huko wakafanya kupandikiza kama wanavyofanya kwa wale wanaotoa mbegu za Kiume na kuwapa akina mama ambao hata hawawajui.

Shida kubwa iliyopo ni kuona kuwa Mtoto wangu anaweza kukulia kwenye familia au nyumba ambayo Mama anaishi na GIRLFRIEND wake na kwa maana nyingine ni kwamba, hawa ni Wasagaji. Mbaya zaidi kakiwa ka kike, si ndiyo itakuwa shida kwa mtoto huyo? Itabidi ajifunze kuwa Mliberali mapema sana au aungane nao.

Hebu nyie wakali na wazoefu wa haya mambo mniambie, kwa hili NIKUBALI au NIKATAE?

ANGALIZO: Hii ni habari ya kweli, utani pembeni Bandugu.
 
Boss,

Hapo ndiyo wasiwasi wangu kwamba siku moja watu wanaanza kuona magezetini "SIKONGE kumbe ni Shoga".

Hii itakuwa kasheshe kubwa sana kwa familia nzima. Upande mmoja nataka kumsaidia ila nikifikiri maisha atakayoanza kukuzwa nayo mwanangu, inaanza kuniwia ngumu. Na kibaya zaidi, wanataka kuja wote wawili yaani huyu Mdada na huyo Girlfriend wake na wote wanataka kuwa na mtoto na mie na eti nikigoma, basi niwape walau mtoto mmoja tu.

Nashindwa kumuelewa huyu dada kwa sababu ana wanaume wengi wanaoweza kumsaidia ila anadai kazimia tabia yangu.
Na akiwa mvula copyright na wewe but ana boyfriend?
si unajua ataona its ok
 
Kwa hiyo unashauri nikimbie au nifumbe macho kwa msemo "Liwalo na liwe?" Ungelikuwa wewe ungelifanyaje?
unasema haujatembea naye wala kumbusu,
so kati ya wanaume wooote kakuchagua wewe,
naona umetunukiwa halahala
azaliwe mtoto wa kiume aanze kuweka vidole juu,
hapo tena kitakuwa kimekula kwako baba mtu.
 
Sijaelewa vizuri, eti nini? Ngoja nishushe fundo moja kwangu arafu nije uni fafanulie.
 
..............Nguruwe pita leo sina Mkuki ...... signature yako Sikonge nimeipenda sana.
Sema na moyo wako,
amua utakavyopenda mwenyewe.

Kwa hiyo unashauri nikimbie au nifumbe macho kwa msemo "Liwalo na liwe?" Ungelikuwa wewe ungelifanyaje?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

Kama ulishawahi kuishi nje na hasa USA na Europe, utagundua kuwa ulikuwa umezungukwa na Mashoga kibao na hasa kama unaishi Mijini. Labda kama ulikuwa hufahamu tu kuwa hao ni mashoga. Hebu waangalie hawa jamaa, unaweza kudhani ni MASHOGA? Na kila siku wanadunda kwenye fani zao.

anderson-cooper-gay-lebron-admints-hes-black1.jpg



STORY ni ya kweli ingawa imebadilishwa KIDOGOOO.....
Mie nisoma mwanzo mpaka mwisho nikadadavua nakubaini kuwa neno Mliberali ndio msingi wa thread hii, haya kazi kwao waliberali
 
Ni kweli hakatai. Ila hapa inakuja na Majukumu ya muda mrefu ambayo pia ni kuwajibika kama MZAZI.

Hiyo ni biashara kwa namna nyingine so we mwambie akutajia dau atalotoa alafu mkubaliane kua mtoto atakuja kuambiwa baba yako alikifafa kwa ajali akiwa na ndugu zake wote ambao mama yake alikua anawafahamu so hakuna ndugu mwingine anafahu!

Ingekua mm na donge lingekua nono ningemtia mimba fasta! Mbegu za kiume haziishi hadi cku ya kufa
 
Huko kujidai mwema kutakuponza ohoooo...! Mambo mengine lazima uyatolee maamuzi bila kujali upande wa pili utajisikiaje..!
 
Nilivyokusoma naona wewe hujui utakalo na wengi itakuwa shida kukushauri, unauzi kiaina fulani.

Umeleta hoja unajibiwa, unakuwa tena haujaridhika unataka mtu aendelee kuongea. Mada yako, kichwa chako, uamuzi wako sasa kutaka kujibishana zaidi na hata huwaulizi y wamesema hayo upate mawaiza zaidi unakuwa kama unawakata paaaa.

Unaleta story nyingine ndefuuuuuuu, hata baada ya kuomba eti sio mautani. Mmmmm!!!!!
 
Sasa Mkuu, siku moja Mtoto akaambiwa ukweli na anitafute na aje apewe habari kamili si itakuwa kasheshe?

Anyway, kinachoniambia nifanye ni kama ulivyoandika ila sintahitaji kuuza kwa sababu siyo kawaida yangu. Ila wasiwasi wangu ni MALEZI. Itakuwaje Mtoto akikuzwa kwenye nyumba za Mashoga? Huo ndiyo wasiwasi wangu pekee. Kuhusu mahitaji mengine wala haina shida kwa sababu Binti nyumbani kwao wapo fresh....
Hiyo ni biashara kwa namna nyingine so we mwambie akutajia dau atalotoa alafu mkubaliane kua mtoto atakuja kuambiwa baba yako alikifafa kwa ajali akiwa na ndugu zake wote ambao mama yake alikua anawafahamu so hakuna ndugu mwingine anafahu!

Ingekua mm na donge lingekua nono ningemtia mimba fasta! Mbegu za kiume haziishi hadi cku ya kufa
 
Back
Top Bottom