Shituka haraka sana unapoona biashara yako imekuwa yebo yebo

CONTROLA

JF-Expert Member
Sep 15, 2019
6,939
22,963
Nawambiaga watu hamna biashara isiyo na faida chini ya JUA yani hakuna,ukiona umefungua biashara halafu wewe huoni faida tambua 1.umekosea location 2.unafungua kitu kile kile ambacho watu wanacho tayari.

tukiachana na yote hayo bado biashara inataka uvumilivu 81% unaweza ukakosea location ila ukiwa mvumilivu ukakaza hapo hapo (utatoboa) japo kwa mbinde,lakini pia unaweza kosea bidhaa ukaleta bidhaa sehemu isiyo sahihi ila ukiwa mvumilivu ukakaza hapo hapo (utatoboa) japo kwa mbinde pia.

Msingi wa biashara yyte chini ya jua ni 1.Mtaji 2.Uvumilivu ukiwa na hizi vitu viwili wewe biashara kwisha habari yesu atarudi atakukuta unafanya biashara maana wakukuweka SUB hatopatikana kwenye biashara.

Bana leo nataka niwasanue wananchi wenzangu ambao mpo ktk biashara na sasa hv umekaa ofisini kwako huoni wateja biashara kwako inazidi kuwa mbaya kadri siku zinavyoenda Afadhali ya Jana.

Sikia nikwambie ndugu yangu Hapo ulipo toka nnje ya ofisi yako angalia upande wakulia na kushoto angalia ofisi kama yako zipo ngapi? kama ni una tigo/M pesa angalia zipo ofisi ngapi za aina yako? kama unasuka kagua chochoro zote krbu na wewe kuna msusi mwingine wapi kama wewe? kama ni saloon ya kiume/kike inuka kagua kuna saloon ngapi kama yako mtaa huo?

ukitoka tu ukikutana na watu wanafanya biashara kama yako eneo lako,au mtaa wa pili fahamu upo kwenye Danger zone..Wanasemaga kwamba kwenye biashara "Ataewahi ndio Mshindi" biashara inataka hivyo wahi kufanya kitu ambacho bado watu hawajasanuka kinahela,Mfano mzuri ni mr.MAX wa max.malipo huyu mwamba ndio mtu wakwanza kula hela tamu za umeme hii nchi,enzi hyo umeme tunaenda nunua sheli foleni huku na kuleee..

Njo kwenye tigo/m pesa hii biashara n nzuri ila si nzuri kama unavyoiona sasa hv,nadhani upo hapo unaona hizo kamisheni zinakutosha kbsa (ni sawa) ila fahamu kwamba ingekulipa mara 4 ya unachokipata kama ungefanya tigo/m pesa miaka ya nyuma huko.

Kila biashara inalipa ila unapoona kila mtu anafanya biashara unayofanya,shtuka tambua anytime utaanza lia lia hali ngumu (usifurahi sanaaa) kuona mahali kuna biashara kama yako fahamu lazima mtagawana wateja,unafkiri wanaofungua biashara kama yako eneo ulilopo unadhani wanapata wapi wateja?

hamna cha kusema "kila mtu na wateja wake" huo ni uwongo,mtu anaefungua biashara kama yako eneo ulilopo kubali kataa Lazima mgawane wateja,akiongezeka mwingine nae mnagawana nae wateja,nk nk

Usisubiri maji yakufike shingoni,usisubiri sema biashara mbaya angalia tu majirani na mtaa uliopo wangapi wanafanya unachofanaya SIO tunasingizia vyuma vimekaza hali ngumu wakati sisi wenyewe akili zetu hazifunguki kuwaza zaidi.

sijasema uache unachokiifanya Point yangu ni wewe uone matokeo chanya ya biashara yako,ufungue asubuhi urudi jioni na pochi imejaa tembo sio urudi nyumbani na lawama na huzuni sasa basi ukishaona u yebo yebo umezidi HAMA.

HAMA
hapo ulipo tafuta connection mahali pengine kafungue huko ofisi yako,kwani hiyo frem yako au umegundishwa kwani? kodi ikiisha tembea mbele kafungue mahali pengine biashara jitenge na hao iga iga yanini kugawana wateja wakati zipo sehemu unaweza kwenda ukafungua ukapata wateja peke ako au mkawa tu wawili kuliko kukaa sehemu ofisi mmepangana kama mahindi bana.

Kuhama sio dhambi,kuna wafanyabiashara wanaona aibu sana kuachia frem wakiamini ni dalili ya kufeli,nataka kuwambia kuwa kugandana kwenye hayo mafrem ambayo mnashnda siku nzima na bado mnarudi nyumbani hamna cha maana ndio kufeli kwenyewe.

imeisha hiyo/newspaper hilo.
 
Nimeichukua kama ilivyo. Nina biashara yangu flani nilikua faida sana siku za mwanzo. Ila sahivi dah inapita siku mbili sijaingiza ata mia.

Ngoja nifanye ushauri wako. NAHAMA kodi ikiisha miezi miwili ijayo.
 
Yeah ni kweli ila unakinzana na kauli yko umesema kua "atakae wahi ndie mshindi"

Then unasema kama watu wanafanya kile unacho fanya uhame kwa maana ya kugawana wateja

Asee mfano Mimi niende labda kariakoo huwa na maduka yng special nikikosa apo ndo nitaenda kwingine

Amin kila mtu huwa na wateja wake hata kwa bodaboda kuna mtu yupo radhi angojee boda wake kuliko kupanda boda tofauti
 
Sawa mkuu kama ubunifu tu ndio unaleta wateja basi sawa.

ila fahamu kuna sehemu hazitaki bunifu,wanataka huduma.Kwisha.
Kwenye huduma hapo hapo kuna ubunifu...
ww kuwa na huduma mbovu watu hawaji..
kwenye customer care muweke mtu anayejua machejo......
 
  • Thanks
Reactions: _ID
nimekupta, maendeleo hayana chama.
mm ni CCM.
ila mwaka huu nabadili gia,
NAHAMISHA KURA.
pmj bro.
 
Kuhama kuna cost zake, ni bora Uvue gamba La biashara yako Hapohapo Ulipo
unaweza hamia sehemu ukajikuta kabla ya mzunguko kukubali pumzi imekata

Hakuna location ya peke yako, utakaa hapo watu watakuona unapiga hela nao wataanza kufanya kama ww, Sema wengi tukipata ushindani Tunakata tamaa mapema

kaa tulia fikiria kwanini wateja wanaenda kwa jirani yako, kwanini hauna trusted customer

isije ikawa wenzako wanakuzidi padogo tu, labda wenzako wanapunguza 50 TZS kwenye bidhaa zao, sasa itakua ukichaa kukimbia washindani bila kutafuta solution Hapohapo Ulipo, Lasivyo kafungulie biashara familia Yako chumbani

mfano hapa jirani kuna jamaa kaweka kijana asimamie biashara yake, kumbe yule kijana anaongeza chajuu, hii imefanya mimi nionekane nauza bidhaa zilezile kwa bei ya jumla


Utahama location ngapi, tambua kujulikana nako ni mtaji
 
Mawazo ya kipumbavu kabisa.


Biashara yoyote Ni consistency hizo zingine Ni porojo. Hakuna sehemu utaenda duniani ukafanya biashara isiyokuwa na competitors. Cha msingi Ni kuwa mbunifu.

Mbona Azam media imeanzishwa na kuzipita kampuni kongwe za media tanzania!!!
 
...........................Sidhani kama ni sahihi kusema funga biashara eneo A kisha hamia eneo B kisa umepata wapinzani,kwenye biashara (mfano nayofanya mimi) ukisema utumie technique hii sekunde tu unapotea kwenye mchezo watu wanakusahau.kutokana na unapohama hama sana inabidi utakakohamia usubiri uanze tena kutengeneza wateja wapya na kule ulikohama wale wateja permanently uliokwishajitengenezea wakija wakakukosa wanahamia kwa wapinzani wako uliowaacha pale na endapo utajichanganya ukosee location na umeshalipa kodi ukijifariji kodi ikiisha nitahama tena jua pumzi zitakuishia njiani.

Jua kuwajali wateja wako,shusha bei kidogo hudumia mteja kwa wakati na kwa uaminifu utadumu sehemu hiyo hiyo watakaokuja wataondoka wao wakuache muhimu siri zako jinsi unavyoifanya hii biashara yako jitahidi wasizijue,haijatokea bado biashara halali utakayoianzisha mtu wenzako wasikuige muhimu mapema unapoanza weka msingi imara kiasi hata kama akija mpinzani isiwe rahisi kwake ku-survive kizembe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mawazo ya kipumbavu kabisa.


Biashara yoyote Ni consistency hizo zingine Ni porojo. Hakuna sehemu utaenda duniani ukafanya biashara isiyokuwa na competitors. Cha msingi Ni kuwa mbunifu.

Mbona Azam media imeanzishwa na kuzipita kampuni kongwe za media tanzania!!!
Nope!!

Siyo mpumbavu mkuu tatizo anawakaririsha watu hints za kwenye makaratasi alizokaririshwa na lectures wa chuo ambao wenyewe hawajawahi kufungua hata magenge ya nyanya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom