issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Sambwee Shitambala, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Mkoa wa Mbeya, amekitaka Chadema kutambua kuwa siasa haiwezi kuendeshwa kwa namna ya maandamano,vurugu na uchochezi.
Amesema hayo jana wakati CCM kikizindua kampeni zake katika uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Majengo kwa ajili ya kumnadi mgombea wa nafasi hiyo, Samweli Mwamboma.
Shitambala alisema Chadema wamekuwa wakitumia maandamano yanayoambatana na vurugu wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia mwafaka ya kukijenga chama chao bila kutambua kuwa Watanzani wanachotaka ni kuwa na chama ambacho kina mfumo mzuri utakaowawezesha kuwaletea maendeleo.
Alisema wananchi wa Mbeya wasikubali kuwapiga mawe viongozi na badala yake wapige kura kuwachagua viongozi waadilifu ambao wataweza kuwaletea maendeleo.
CCM msipige mawe pigeni kura, CCM fanyeni maendeleo msifanye fujo, CCM jengeni hoja msifanye maandamano, alisema Shitambala.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Mbeya, Dk. Mary Mwanjelwa, alisema wanachama wa CCM watembee kifua mbele kwani serikali yao iliyopo madarakani inafanya mambo mengi ya kuwaletea maendeleo.
Naye mgombea udiwani kata ya Majengo, Samweli Mwamboma, alisema akichaguliwa atahakikisha anashirikiana na wananchi wa kata hiyo katika kuwaletea maendeleo.
Amesema hayo jana wakati CCM kikizindua kampeni zake katika uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Majengo kwa ajili ya kumnadi mgombea wa nafasi hiyo, Samweli Mwamboma.
Shitambala alisema Chadema wamekuwa wakitumia maandamano yanayoambatana na vurugu wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia mwafaka ya kukijenga chama chao bila kutambua kuwa Watanzani wanachotaka ni kuwa na chama ambacho kina mfumo mzuri utakaowawezesha kuwaletea maendeleo.
Alisema wananchi wa Mbeya wasikubali kuwapiga mawe viongozi na badala yake wapige kura kuwachagua viongozi waadilifu ambao wataweza kuwaletea maendeleo.
CCM msipige mawe pigeni kura, CCM fanyeni maendeleo msifanye fujo, CCM jengeni hoja msifanye maandamano, alisema Shitambala.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Mbeya, Dk. Mary Mwanjelwa, alisema wanachama wa CCM watembee kifua mbele kwani serikali yao iliyopo madarakani inafanya mambo mengi ya kuwaletea maendeleo.
Naye mgombea udiwani kata ya Majengo, Samweli Mwamboma, alisema akichaguliwa atahakikisha anashirikiana na wananchi wa kata hiyo katika kuwaletea maendeleo.