Shirika la “One Acre Fund” na shughuli za kiutapeli kwa wakulima wadogowadogo, Singida

Mshikawezi Mwizi

JF-Expert Member
Jul 24, 2013
751
374
Ninaandika haya kwa uchungu mkubwa nikiwa na ombi moja kuu kwa mamlaka zinazohusika kulichunguza kwa kina shirika hili, ili kubaini ukweli wa utapeli nitakaoufafanua hapa; kisha hatua husika ziweze kuchukuliwa kwa haraka.

Shirika hili limekuwa likijifafanua kuwa limekuja kutusaidia sisi wakulima wadogowadogo katika shughuli zetu za kilimo kwa kutuwezesha kupata pembejeo za kilimo kupitia mikopo isiyo na riba na kuirudisha mikopo hiyo mara tu baada ya kuvuna na kuuza mazao. Mimi nikiwa muathirika wa mradi huu, walikuja kwangu na kunihoji juu ya ufugaji wa kuku ninaoufanya, baada ya hapo waliahidi kuniwezesha kwa kunipatia vifaa na tiba zote za kuku ili kuboresha uzalishaji. Walinipatia vifaa na dawa mbalimbali za kuku, vyote vikiwa na thamani ya shilingi 180,000/= na kunitaka nianze kurudisha pesa hiyo baada ya miezi mitatu.

Vilevile walinihakikishia kuwa nitakapoanza kurudisha pesa hizi, nitarudisha kwa kila wiki kiasi cha shilingi 18,000/= kwa wiki zisizopungua 10, ila nitakuwa huru kurudisha hata kabla ya muda husika, au kurudisha pesa yote kwa mkupuo mmoja. Baada ya mwezi mmoja niliamua kwenda kuirudisha pesa yao yote kwa mkupuo mmoja, cha ajabu niliambiwa deni langu linakuwa kwa asilimia 35 kwa kila mwezi, hivyo ninadaiwa jumla ya kiasi cha shilingi 243,000/=, kama ningekaa na pesa yao kwa muda tajwa (miezi mitatu) deni langu lingefikia kiasi cha shilingi 369,000/=.

Hali hii ilinisikitisha sana, nilipohoji, nikaambiwa kwa nini ninalalamika wakati wamenisaidia kuongeza uzalishaji; nilipowaambia tatizo si kuongeza au kupunguza uzalishaji bali ni wao kwenda kinyume na maelezo yao, kiongozi wao mmoja mwenye jina lenye herufi za mwanzo L.L alinijibu kwa ufupi, “dawa ya deni ni kulipa”.

Nililipa pesa yao lakini nilihudhunika sana. Naziomba mamlaka husika zifanye kazi za kulichunguza shirika hili kujua ni jinsi gani linafanya kazi zake.
 
Hawa huko kilolo wanaliza watu vibaya sana,,hasa wakulima wa mahindi mabichi.


Wana solar zao wanawapiga wanavijiji,,

Kampuni nyingi zinazo fanya mambo yao mengi vijijini ni wezi ,mfano Zola ,mobisol na one acre find. Wanatumia ufahamu mdogo walio nao watu wengi wa vijijini kuwaibia
 
Kwani kuna mikataba mnasiniana nao au ni verbal agreement
Waje town wapoteze hata hizo wanazotoa.
Kama hatuandiki badala ya 100k nakupa 1k
 
Hawa huko kilolo wanaliza watu vibaya sana,,hasa wakulima wa mahindi mabichi.


Wana solar zao wanawapiga wanavijiji,,

Kampuni nyingi zinazo fanya mambo yao mengi vijijini ni wezi ,mfano Zola ,mobisol na one acre find. Wanatumia ufahamu mdogo walio nao watu wengi wa vijijini kuwaibia
Hatari hao Zola wanawatapeli vipi watu?
 
Lakin ninachojua mm haya mambo yanaenda jwa maandiah,huwez pewa mkopo bila kuwa na repayement/installment schedule
 
Ninaandika haya kwa uchungu mkubwa nikiwa na ombi moja kuu kwa mamlaka zinazohusika kulichunguza kwa kina shirika hili, ili kubaini ukweli wa utapeli nitakaoufafanua hapa; kisha hatua husika ziweze kuchukuliwa kwa haraka.

Shirika hili limekuwa likijifafanua kuwa limekuja kutusaidia sisi wakulima wadogowadogo katika shughuli zetu za kilimo kwa kutuwezesha kupata pembejeo za kilimo kupitia mikopo isiyo na riba na kuirudisha mikopo hiyo mara tu baada ya kuvuna na kuuza mazao. Mimi nikiwa muathirika wa mradi huu, walikuja kwangu na kunihoji juu ya ufugaji wa kuku ninaoufanya, baada ya hapo waliahidi kuniwezesha kwa kunipatia vifaa na tiba zote za kuku ili kuboresha uzalishaji. Walinipatia vifaa na dawa mbalimbali za kuku, vyote vikiwa na thamani ya shilingi 180,000/= na kunitaka nianze kurudisha pesa hiyo baada ya miezi mitatu.

Vilevile walinihakikishia kuwa nitakapoanza kurudisha pesa hizi, nitarudisha kwa kila wiki kiasi cha shilingi 18,000/= kwa wiki zisizopungua 10, ila nitakuwa huru kurudisha hata kabla ya muda husika, au kurudisha pesa yote kwa mkupuo mmoja. Baada ya mwezi mmoja niliamua kwenda kuirudisha pesa yao yote kwa mkupuo mmoja, cha ajabu niliambiwa deni langu linakuwa kwa asilimia 35 kwa kila mwezi, hivyo ninadaiwa jumla ya kiasi cha shilingi 243,000/=, kama ningekaa na pesa yao kwa muda tajwa (miezi mitatu) deni langu lingefikia kiasi cha shilingi 369,000/=.

Hali hii ilinisikitisha sana, nilipohoji, nikaambiwa kwa nini ninalalamika wakati wamenisaidia kuongeza uzalishaji; nilipowaambia tatizo si kuongeza au kupunguza uzalishaji bali ni wao kwenda kinyume na maelezo yao, kiongozi wao mmoja mwenye jina lenye herufi za mwanzo L.L alinijibu kwa ufupi, “dawa ya deni ni kulipa”.

Nililipa pesa yao lakini nilihudhunika sana. Naziomba mamlaka husika zifanye kazi za kulichunguza shirika hili kujua ni jinsi gani linafanya kazi zake.

Kwenye mkataba mliosaini kulikuwa na hiyo 35%? Maana wakati mwingine hilo lilikuwa wazi kwenye masharti ya mkopo
 
Kwani kuna mikataba mnasiniana nao au ni verbal agreement
Waje town wapoteze hata hizo wanazotoa.
Kama hatuandiki badala ya 100k nakupa 1k
Suala hapa si mkaba, kitu cha kuangalia ni kwa nini wanafanya biashara? Kwani One Acre Fund ni kampuni? Je, wanalipa kodi kwa biashara hii wanayoifanya kinyume na sheria za kusajiliwa kwao?....Jambo la mwisho ni kwamba kama wanakopesha kwa riba, hiyo tayari ni biashara.
 
Back
Top Bottom