Shirika la Ndege, FlyBMI lafirisika!

imhotep

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
46,678
71,032
3720.jpg


Shirika lingine hili nalo limefifisika BMI budget airline limepaki.

Nasikia ATCL nalo linasukumwa na abiria sasa habari ndio hiyo.

Tundu Lissu, Zitto Kabwe walituonya tukawaona wachawi haya sasa!!

Soma: British airline Fybmi collapses, leaving passengers stranded na Flybmi collapses and grounds flights - what next and can you get a refund
 
Mashirika ya ndege yanayofilisika yapo mengi sana, tena mengi yake yapo Ulaya na Marekani kwenye wasafiri wengi wanaotumia ndege.

Kwenye wasafiri wengi wanaotumia ndege na pia ujuzi wa kiundeshaji, na access ya mitaji na wawekezaji na wataalam wa kiufundi na kiiiila kitu, na bado wanakula hasara kwa sababu ya ugumu wa biashara hii.

Hapa kwetu wataficha kwamba tunakula hasara, na watamwaga hela kuziba mapengo, cash injection, kama ambavyo juzi wame pampu bilioni 600 zikatengeneze ndege ambazo kumbe hazina warranty. Mkataba mbovu!
 
View attachment 1027133

Shirika lingine hili nalo limefifisika BMI budget airline limepaki.
Nasikia ATCL nalo linasukumwa na abiria sasa habari ndio hiyo.

Tundu Lissu,Zitto Kabwe walituonya tukawaona wachawi haya sasa!!
Ujinga ni kuzungumzia jambo lenye maana nyingine ukimaanisha kitu kingine.

Ndege kusukumwa unaona jambo la ajabu sana? Unaona kama ndege ni mbovu? Unaona kama ATCL imefirisika?

Kwanini tunaomba mabaya kwa mambo yahusuyo nchi? Eti unaomba shirika la ATL lifirisike? Sasa utapata faida gani?
Bora liendelee kuwepo maana kuna watanzania wamepata ajira pale either direct au indirect.

Hao wanasiasa wenyewe wanapanda ndege hizo hizo lakini bado wanaponda.

Pamoja na ndege hizo kutokua na nauli ya mtanzania wa kawaida kama mimi bado siwezi kuziombea mabaya, acha ziwepo zifanye kazi wenye uwezo watapanda nami siku nikipata hela nitapanda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mada zako nyingi zinauwalakin samahan kwa kuusema ukweli huu, angalia aina ya presentation yako, mara uweke vituko mara uweke mbwembwe,

Jaribu kuwa unaleta hoja ili hata Lumumba waamini kwamba wamepoteza kweli mtetezi mtandaoni,
Umeona mkuu naona saizi haishiwi vituko na mbwembe sioni kama tumepoteza chochote kwa huyu jamaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom