Bado uko mulemule kwani wakisema wanna njaa Wana maanisha nini !Sio njaa ni imani za watu ushirikina. Fisi akigogwa hata barabarani wasukuma watasafisha hadi unyoya na damu.Fisi kwa imani zao anasadikika kuwa na nguvu ,bahati.Hata baadhi wacheza ngoma za jadi nguli huwafuga na kwenda nao katika matamasha kama kivutio na nguvu za ziada.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu wacha kuongopa!Kama simba mwenyewe anagwaya kula nyama ya fisi, binadamu wanagombania fisi kweli? hao watu kwa kweli wamebobea kwenye ushirikina..
Documentary 1 niliiona simba walikua watatu na wana njaa hatari mpk wamekonda,wakamuua Fisi wakaanza kumla ila simba mmoja na njaa yake aligoma kabisa kumla yule fisi akabaki na njaa yake tu(wanasema nyama ya fisi inanuka).Mkuu wacha kuongopa!
Haujaangalia chanel za wanyama kama Natgeo nk, fisi kwa simba ni 'sambusa'.
Analiwa hadi anaisha huku akipiga kelele za vitisho zisizomsaidia!
Simba naye akikaa vibaya analiwa na mbwa mwitu.
Mbwa mwitu akiingia kwenye anga za fisi, anafyagiliwa huku akibweka.
Hakuna aliye salama.
Nilidhania tembo hawezekani, kumbe kwa simba ni mswaki!
Mambo ya porini yaacheni jamani nyie.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakutokea Ngokolo. Alikurupushwa sehemu nyingine, na kukimbilia huko.ngokolo si ni mjini kabisa..fisi anatoka wapi?
Aliyeondoka na matumbo nampa pole sana... Akamakinike na nyongoKatika hali isiyo ya kawaida wakazi wa kata ya Ngokolo Mjini Shinyanga wamegombania nyama ya fisi waliyemuua baada ya kuonekana akiranda randa katika kata hiyo.
Tukio hilo la aina yake limetokea Ijumaa Februari 7,2020 majira ya mbili usiku katika mtaa wa Magadula kata ya Ngokolo ambapo mamia ya wananchi wameonekana wakisukumana huku wengine wakikata viungo vya mnyama fisi anayedaiwa kuwa na hirizi katika mguu wake wa mbele.
“Huyu fisi ametokea maeneo ya Seif Hotel, akaelekea maeneo ya Stendi ya mabasi Mjini Shinyanga, wananchi wamemkurupusha Stend, akatokezea eneo la Mapinduzi shule ya Msingi, kisha Mshikamano baadae akaingia kwenye kalavati/daraja lililopo mtaa wa Magadula karibu na barabara ya Mohamed Trans.
“Huyo fisi alivyoingia kwenye kalavati akatulia humo, wananchi wakachoma tairi upande wa pili, kutokana na moshi fisi akatoka, ndipo mmoja wa wananchi hao akampiga jiwe huyo fisi akaanguka. Jamaa aliyempiga jiwe akakata mguu wa mbele wenye hirizi, akaondoka zake na wananchi wakaendelea kugombania viuongo vya fisi, kila mmoja akikakata kiungo alichoona kinamfaa. Askari polisi wamefika ikashindikana kuondoa wananchi." Mashuhuda wamesema.
Tukio hili limehusishwa na imani za kishirikina kutokana na madai kwamba fisi huyo alikuwa na hirizi na siyo rahisi fisi kuonekana mjini kwani fisi mara nyingi hupendelea kwenye mapori/vichaka.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa baada ya fisi huyo kuuawa na wananchi kugawana nyama,mwanamke mmoja ameonekana eneo alipouawa fisi huyo na kuanza kuangua kilio akidai fisi wake kauawa.
"Yaani huku ni vituko, kuna mama kaja mpaka eneo alipochinjiwa fisi akaangua kilio fisi wake wamemchinja akaanza kutafuta kichwa hajakipata, akawaambia watu fisi wangu alikuwa na kitu bora wangenirudishia tu. Kazoa mabaki yote kaondoka nayo alikuwa na bodaboda. Watu walivyoona hivyo wamemfuata na daladala na bodaboda kwa nyuma hadi wajue anakoelekea." amesema mmoja wa wakazi wa eneo hilo.
View attachment 1350642
Sent using Jamii Forums mobile app
Documentary 1 niliiona simba walikua watatu na wana njaa hatari mpk wamekonda,wakamuua Fisi wakaanza kumla ila simba mmoja na njaa yake aligoma kabisa kumla yule fisi akabaki na njaa yake tu(wanasema nyama ya fisi inanuka).
dodge
Ukute huyu jamaa msumbufu ni mlaji wanyama ya fisi. Maana huwezi kuelezea vituko vyake.
Ila hiyo yote inaakisi wimbi la umasikini walilonalo jamii hiyo.
Katika hali isiyo ya kawaida wakazi wa kata ya Ngokolo Mjini Shinyanga wamegombania nyama ya fisi waliyemuua baada ya kuonekana akiranda randa katika kata hiyo.
Tukio hilo la aina yake limetokea Ijumaa Februari 7,2020 majira ya mbili usiku katika mtaa wa Magadula kata ya Ngokolo ambapo mamia ya wananchi wameonekana wakisukumana huku wengine wakikata viungo vya mnyama fisi anayedaiwa kuwa na hirizi katika mguu wake wa mbele.
“Huyu fisi ametokea maeneo ya Seif Hotel, akaelekea maeneo ya Stendi ya mabasi Mjini Shinyanga, wananchi wamemkurupusha Stend, akatokezea eneo la Mapinduzi shule ya Msingi, kisha Mshikamano baadae akaingia kwenye kalavati/daraja lililopo mtaa wa Magadula karibu na barabara ya Mohamed Trans.
“Huyo fisi alivyoingia kwenye kalavati akatulia humo, wananchi wakachoma tairi upande wa pili, kutokana na moshi fisi akatoka, ndipo mmoja wa wananchi hao akampiga jiwe huyo fisi akaanguka. Jamaa aliyempiga jiwe akakata mguu wa mbele wenye hirizi, akaondoka zake na wananchi wakaendelea kugombania viuongo vya fisi, kila mmoja akikakata kiungo alichoona kinamfaa. Askari polisi wamefika ikashindikana kuondoa wananchi." Mashuhuda wamesema.
Tukio hili limehusishwa na imani za kishirikina kutokana na madai kwamba fisi huyo alikuwa na hirizi na siyo rahisi fisi kuonekana mjini kwani fisi mara nyingi hupendelea kwenye mapori/vichaka.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa baada ya fisi huyo kuuawa na wananchi kugawana nyama,mwanamke mmoja ameonekana eneo alipouawa fisi huyo na kuanza kuangua kilio akidai fisi wake kauawa.
"Yaani huku ni vituko, kuna mama kaja mpaka eneo alipochinjiwa fisi akaangua kilio fisi wake wamemchinja akaanza kutafuta kichwa hajakipata, akawaambia watu fisi wangu alikuwa na kitu bora wangenirudishia tu. Kazoa mabaki yote kaondoka nayo alikuwa na bodaboda. Watu walivyoona hivyo wamemfuata na daladala na bodaboda kwa nyuma hadi wajue anakoelekea." amesema mmoja wa wakazi wa eneo hilo.
View attachment 1350642
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu unaona nasema uongo kuongea kuhusu hali ya umaskini Nchini?
Bila shaka