Shinyanga: Polisi kutangaza matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa inakubalika kisheria?

Watu wa sheria kama wapo hivi hatuwezi kufungua kesi kwa huu ukiukwaji wa sheria???
 
Watu wa sheria kama wapo hivi hatuwezi kufungua kesi kwa huu ukiukwaji wa sheria???

Huwezi amini tume hii ya uchaguzi ndiyo iliyomtangaza naibu waziri wa madini ubunge kwa tofauti ya kura moja,hivyo basi hata polisi nao wamegeuka tume ya uchaguzi.Wametumiwa sana kupiga mabomu ya machozi kwenye chaguzi ambazo wapinzani wamekuwa wakiongoza,lakini ipo siku deni la usaliti litalipika kutokana na wahanga wa mabadiliko ya kweli toka mikono michafu ya madhalimu wanao kula bila kunawa
 
Hawajifunzi kwa wenzetu,Tunisia ilikuwa hivyo hivyo lakini leo wako wapi?Misri ya leo tofauti na ya Mubarak,alijiona Mungu mtu lakini leo ana pumulia mashine.Alikuwepo Mabutu Seseko amekufa kifo cha aibu.Walikuwepo watawala wabovu kama Thomas Sankara leo wako wapi?IGP wa Malawi yuko wapi leo hii kama si kusubiri kifungo chake kwa kuibaka demokrasia akisahau kuwa yeye kazi yake ni ulinzi wa raia na mali zake na si siasa.
 
tupo kwenye kipindi cha mpito tunasubiri katiba yetu wote hawa polisi waliona wangewaachia watangaze hawa tume wasingesema ukweli ndiyo maana CDM 7 na hao wengine 4
 
Kama demokrasia ndiyo hii basi nachelea kusema imevuka mipaka na kukoma zaidi hata ya nchi za magharibi.Hali hii imejitokeza siku ya Jumapili ya tarehe 24/06/2012 mkoani Shinyanga kata ya Masekelo maarufu kama kambi ya upinzani mkoani humo mtaa wa bondeni.Kitendo kilicho washangaza wapiga kura ni kwa jeshi la Polisi kuchukua dhima ya kutangaza matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Kinacho shangaza ni sheria gani iliyotumika kwa jeshi la polisi kugeuka tume ya uchaguzi na kutangaza matokeo ya uchaguzi huu ambao matokeo yake yalitangazwa mnamo mida ya saa tano usiku, kitendo kilicho sababisha mabomu ya machozi kurindima na kuwatawanya wakazi wa maeneo hayo ya Bondeni.Kama hali ndiyo hii basi demokrasia nchini mwetu imevuka mipaka na kushinda hata nchi za magharibi.

Wakuu wana JF tujaribuni kuliweka sawa hili kama kweli sheria za uchaguzi zina ruhusu chombo cha dola kuchukua majukumu hayo.


Source sammosses from Shinyanga
Serikali dhaifu huzaa vitendo vya ajabu ajabu, tume ya uchaguzi ilikuwa wapi????
 
Kwa staili hii serikali inazidi kujichimbia kaburi lake yenyewe,tumeona chaguzi ndogo za ubunge watu wakiuwawa bila hatia kwa kuwa tu wamekuwa kikwazo kwa mbinu zao chafu.Leo tena lina zuka jingine la kutekwa kwa kiongozi wa chama cha madaktari ndugu Ulimboka kwa kupigwa na kujeruhiwa vibaya sana vyote hivyo vikienda sambamba na tamko la waziri mkuu,kweli hii ni hatari
 
Huu ni ukibaka wa demokrasia. Hivi hawa polisi wa miaka hii wanafundishwaje?
 
Polisi hawa ndiyo wanatumika katika ku engineer uhalifu hapa nchini,wakati mwingine napata wakati mgumu kujua nini hasa nafasi ya katika kuihudumia nchi yetu.Maana wanaongoza kwa matukio mbalimbali,Tukio la dk.Ulimboka askari walikuwepo,tukio la kuchakachua matokeo ya uchaguzi wamo,tukio la kutoroshwa wanyama wetu wamo,hivi kuna haja ani ya kuwa na jeshi hili lisilona nidhamu ya utendaji.
Huu ni ukibaka wa demokrasia. Hivi hawa polisi wa miaka hii wanafundishwaje?
 
kwa hiyo unamaanisha yatakuwa yanatolewa kwenye kambi za jeshi

i hope so ili mzalendo yeyote atakayetia pua yake kambini amiminiwe mabomu ya kutosha na hivyo kuwatia uoga wengine. Ama kweli ada ya mja hunena na mwungana ni kitendo. WENYENCHI WAMEKOSA BUSARA NA WANANCHI WANAHAHA. Kuna haja ya kuwa na mtazamo tofauti kwa wananchi kuanzia leo hii ili hitimisho likamilike itakapofika 2015 kwa kuwaondoa wenyenchi madarakani!!!
 
Lazima haki ionekane ikitendeka,tukilalamika bila kuchukua hatua hatutamaliza hili tatizo,ifike mahali watu wote tuheshimianae mbeleya sheria,isiwe uti wa sheria kwa tabaka fulani ili hali wengine wakiendelea kuvunja sheria
 
Ndiyo maana nashauri tulivunje jeshi hili tutengeneze lingine lenye maadili na kulinda heshima wakiongozwa na utashi wa kisheria.Haiwezekani jeshi letu hili likawa kichaka cha wahalifu na kimbilio la wahuni walioshindikana vijiweni.Sifa kama huvutaji bangi ndani ya jeshi hili inatakiwa kupingwa kwa nguvu zote kwani watendaji wengi wa chini ndiyo wahusika wakuu wa kuvuta na kuuza.
 
Back
Top Bottom