Shinyanga: Nyumba za Walimu zageuzwa danguro

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Majengo mawili ya nyumba za walimu ambayo ujenzi wake haujakamilika katika Shule ya Sekondari Mwasele, Kata ya Kambarage, Manispaa ya Shinyanga, yamedaiwa kugeuzwa danguro na kusababisha baadhi ya wanafunzi kupewa ujauzito na kuacha masomo.

Diwani wa Kambarage, Hassani Mwendapole, alipaza kilio hicho wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la manispaa hiyo kilichojadili utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2019/20 ya Sh. bilioni 41.5 kwa kipindi cha nusu mwaka.

Alidai miradi mingi ya maendeleo imeendelea kuwa kiporo, zikiwamo nyumba mbili za walimu zilizoko katika shule hiyo, ambazo kwa sasa zimegeuka kuwa 'guest house' na kusababisha ujauzito kwa wanafunzi shuleni hapo.

“Nyumba hizi za walimu katika Shule ya Sekondari Mwasele zilijengwa tangu mwaka 2011 na sasa kuna mapagale tu, na yameshageuka kuwa kama guest house, zinatumika kwa ngono na kusababisha kuwapo mimba za wanafunzi," alilalamika.

Diwani wa Viti Maalum, Shela Mshandete, alitoa ushuhuda kuwa kwenye majengo hayo ya nyumba za walimu ambayo hayajakamilika kujengwa, kuna wanafunzi walishakamatwa wakifanya ngono.

Pia Diwani wa Mwamalili, Paulo Machela, alisema kuna haja ya kukamilisha miradi ya maendeleo ambayo ni viporo, akieleza kuwa mingi ilijengwa kwa nguvu za wananchi.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, John Kisandu, aliuagiza uongozi wa manispaa hiyo kuhakikisha hadi kufikia Juni mwaka huu, unakamilisha miradi ambayo ni viporo, na ile ambayo haitakamilika, iingizwe kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, Geofrey Mwangulumbi, alisema tayari alishamwagiza mchumi wa manispaa hiyo, Gwakisa Mwashebya, afuatilie miradi yote ambayo ni viporo ili kupata idadi kamili.

Chanzo: IPP Media
 
Hivi vitoto vya kike vinatakiwa kupewa elimu ya kujitambua.

Otherwise, vitaliwa mpaka! Na vinapenda kweli kweli!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha vikijitambua ndio vinaongeza kasi.
Mwalimu mmoja alikuwa anasema hivi vitoto vikiwa secondary utasikia kila kamoja kana boyfriend, vikifika high school utasikia kila kamoja kana kwambia nina mchumba sijui yuko chuo fulani, vinajiona vime-advance kumbe mwendo ule ule kuliwa tu.
 
Hahaha vikijitambua ndio vinaongeza kasi.
Mwalimu mmoja alikuwa anasema hivi vitoto vikiwa secondary utasikia kila kamoja kama boyfriend, vikifika high school utasikia kila kamoja kanakwambia nina mchumba sijui yuko chuo fulani, vinajiona vime-advance kumbe mwendo ule ule kuliwa tu.
Kuliwa ndio necha yao wapewe elimu ya kujitambua.....
viliwe huku vinajitambua...
 
Hahaha sio kweli, ha madiwani walitaka kufikisha kilio cha nyumba za walimu serikalini.
Mimba inaignia popote, wewe unadhani zikimalizwa hizo nyumba mimba zitaisha?!
Hizo Nyumba zikimalizika hapatakuwa na sehemu ya mafichoficho ya kufanyia zinaa wasionekane.
 
hizo nyumba tayari 'gundu' yaani mwalimu ya jinsia ya 'ke' watakao jaribu kuishi kwenye hizo nyumba watakuwa wanacharazwa mimba tuu
 
Majengo mawili ya nyumba za walimu ambayo ujenzi wake haujakamilika katika Shule ya Sekondari Mwasele, Kata ya Kambarage, Manispaa ya Shinyanga, yamedaiwa kugeuzwa danguro na kusababisha baadhi ya wanafunzi kupewa ujauzito na kuacha masomo.

Diwani wa Kambarage, Hassani Mwendapole, alipaza kilio hicho wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la manispaa hiyo kilichojadili utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2019/20 ya Sh. bilioni 41.5 kwa kipindi cha nusu mwaka.

Alidai miradi mingi ya maendeleo imeendelea kuwa kiporo, zikiwamo nyumba mbili za walimu zilizoko katika shule hiyo, ambazo kwa sasa zimegeuka kuwa 'guest house' na kusababisha ujauzito kwa wanafunzi shuleni hapo.

“Nyumba hizi za walimu katika Shule ya Sekondari Mwasele zilijengwa tangu mwaka 2011 na sasa kuna mapagale tu, na yameshageuka kuwa kama guest house, zinatumika kwa ngono na kusababisha kuwapo mimba za wanafunzi," alilalamika.

Diwani wa Viti Maalum, Shela Mshandete, alitoa ushuhuda kuwa kwenye majengo hayo ya nyumba za walimu ambayo hayajakamilika kujengwa, kuna wanafunzi walishakamatwa wakifanya ngono.

Pia Diwani wa Mwamalili, Paulo Machela, alisema kuna haja ya kukamilisha miradi ya maendeleo ambayo ni viporo, akieleza kuwa mingi ilijengwa kwa nguvu za wananchi.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, John Kisandu, aliuagiza uongozi wa manispaa hiyo kuhakikisha hadi kufikia Juni mwaka huu, unakamilisha miradi ambayo ni viporo, na ile ambayo haitakamilika, iingizwe kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, Geofrey Mwangulumbi, alisema tayari alishamwagiza mchumi wa manispaa hiyo, Gwakisa Mwashebya, afuatilie miradi yote ambayo ni viporo ili kupata idadi kamili.

Chanzo: IPP Media
Hahaaa umenikumbusha mbali sana, wasalimie kwa mzee kasiga, kwa assey na mashineni kwa fabiani hapo. Nimemisi mitaa ya home hapo.
 
Nyumba zisizoisha hutumiwa vibaya na wengi
. Madanguro
. Vijiwe vya madawa ya kulevya
. Maficho ya vibaka
. Vilinge vya wachawi
. Makazi ya wadudu na wanyama hatarishi
. Maeneo ya ubakaji
. nknk
Si vema sana kuanza ujenzi kisha ukakaa muda mrefu bila kumaliza


Jr
 
Hizo Nyumba zikimalizika hapatakuwa na sehemu ya mafichoficho ya kufanyia zinaa wasionekane.
Hahaha mapenzi sio zinaa sister, hizo nyumba hazijaisha lakini wako comfortable kufanya mapenzi, unadhani hizo ndio nyumba pekee hazijamalizika huko shinyanga?! kama wanaweza kula urada humo watashindwaje kuula uroda madarasani?! Au vichakani?!
Mimba haichagui uwanja, popote ina mea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom