Shinyanga: Kijana mmoja akamatwa na Polisi kwa kumdanganya Waziri Ummy kuwa anaumwa COVID-19

Someni muelewe, huyu jamaa baada ya kutoa taarifa akavunja laini na timu ya madaktari ilipofika kumpa huduma wakamkosa. Hii inamaana alikuwa anajua alitendalo kwamba anadanganya. Angeruhusu madaktari wampe huduma halafu asikutwe na covid 19, hapo isingekuwa kosa
Soma Post Na. 17.., and anyway wewe upo akilini mwake huenda baada ya kutoa hii taarifa akapanic.., pia kwenye hili janga ambalo wengi wanaogopa kupimwa au kugunduliwa wanao kuongezea hatari ya kukamatwa ni kuwazidishia woga (hata kama wangemsulubu huyu dogo hakuna haja ya kuutangazia umma)[/QUOTE]Hakuna kitu kama hicho, kukata kwake mawasiliano ndo kumemponza, yeye angetulia madaktari wamcheck wakute hola wamwachie basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kadanganya kwani ana vipimo ?
Yeye kwa upeo wake amedhani anayo, sasa kama hana si bahati nzuri ?
Tunatumia nguvu nyingi kwa vitu ambavyo tungeweza kuvipuuza..., sasa na mimi kesho nikidhani ninayo si taogopa kupiga simu nisihukumiwe kudanganya ?
Shida alipiga simu kwa Waziri alafu akazima simu, kuzima simu, na kuharibu Ile line, Ni kiashiria tosha Cha Nia ovu, dhamira mbaya. Na hiyo ndiyo huwa inaadhibiwa na Sheria.

Evil mind. Askari hawajakosea, alifanya makusudi huyu kijana apate haki yake.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati tukumtetea tukumbuke kuwa alikubali kuvunja laini na kisha kuitupa hali ambayo iliwachanganya madaktari hadi walipoamua kuwatumia watu wa usalama kufuatilia suala hilo,ingekuwe vyema kama angeendelea kushirikiana na madakatari ili hata baadae aje aseme kuwa alisikia dalili za ugonjwa huu,sasa wewe unazima na lini,unategemea huruma gani hapo
 
Sasa kati yangu mimi na wewe sijui nani sio makini..., hii habari imekuwa edited mwanzoni ililetwa nusu kwa maandishi kwamba habari zaidi zitaendelea..., au wewe mgeni humu hujui kuna editing after the fact...
Kwa hiyo hata sasa Jf kuna watu wanafanya huu mchezo wa kuedit habari ?
 
Kwa hiyo hata sasa Jf kuna watu wanafanya huu mchezo wa kuedit habari ?
Kwani hauoni kitufe cha edit kwenye post yako ? Zamani kulikuwa kuna indication edited saa fulani na muda fulani sasa hivi hakuna hio indication, huu sio mchezo mtu anaweza akakosea editing sio kosa....
 
Bado sioni sababu ya kukamatwa........labda aliona ana dalili zote za Corona ndio maana akatoa taarifa?
Wamekweka karantini kwa siku 14?
Si serikali ishukuru Mungu kwamba jamaa hana corona.....
 
Kwani hauoni kitufe cha edit kwenye post yako ? Zamani kulikuwa kuna indication edited saa fulani na muda fulani sasa hivi hakuna hio indication, huu sio mchezo mtu anaweza akakosea editing sio kosa....
Kwa hiyo aliamua kuibali taarifa na kuufuta ukweli aloandika mwanzo ikabidi alazimishwe kuandika mambo mengine ambayo hayakuwepo ?
 
Back
Top Bottom