Shinyanga: Askari anayemlinda mwekezaji adaiwa kumuua kijana kwa risasi, wananchi wamlilia Rais Samia

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Mkazi mmoja wa Kitongoji cha Mwamala, Kijiji cha Igumanghobo, Kata ya Idukilo Mkoani Shinyanga aliyekuwa akichimba madini katika Kijiji cha Mwang’holo, Kata ya Mwadui Lohumbo anadaiwa kuuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi wanaolinda eneo la Mwekezaji Kampuni ya El-Hillal Minerals Ltd.

Marehemu ametajwa kwa jina la Cosmas Hamis Kusililwa umri wa miaka 25 ambaye ni mchimbaji mdogo inadaiwa amepigwa risasi tarehe 10/3/2022 akiwa nje ya eneo la mwekezaji huyo ambako wachimbaji wengi wadogo hujitafutia riziki kwa kuchimba Madini ya Almasi.

Tukio hilo limelaaniwa vikali na viongozi mbalimbali kikiwemo Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan asitishe uwekezaji wa mwekezaji huyo ambaye ameshindwa kuliendelea eneo alilopewa kwa zaidi ya miaka 15 hivi sasa.

Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, William Jijimya na Katibu wa CCM Wilayani humo, Peter Mashenji wamesema kitendo kilichofanyika ni cha kinyama na kwamba wakazi wa Kishapu hawahitaji mwekezaji anayewafanyia vitendo vya ukatili wananchi ambapo pia wamemuomba Mhe Waziri wa Madini kuchukua hatua haraka.






=====================================================


JESHI LA POLISI LAFANYA UCHUNGUZI
Alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP George Kyando alisema: “Hilo ni tukio ni la muda nikilizungumza leo itaonekana kama ni jipya.

Alipoulizwa likuwaje akasema: "Uchunguzi unaendelea, ukikamilika hatua zitachukuliwa.”

Kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa mtuhumiwa na kama bado anaendelea na majukumu yake kama kawaida alisema: “Hatujamkamata, anaendelea na majukumu yake kama kawaida kwa kuwa uchunguzi haujakamilika, wala siwezi kumtaja jina kwa kuwa tutaharibu uchunguzi.

“Nimeshazungumza na ninarudia wananchi wawe watulivu na kama kunakuwa na tatizo lolote wasichukue hatua mkononi, maana askari anaweza kufanya hivyo katika njia ya kujihami.

“Wasivamie askari kwa kuwa kama kuna malalamiko yao kwa wawekezaji au ardhi basi wafuate taratibu za kisheria, kuna mahakama na vyombo vingine vya kufikisha kile wanachokilalamikia na siyo kuchukua hatua mkononi.”
 
Mkazi mmoja wa Kitongoji cha Mwamala, Kijiji cha Igumanghobo, Kata ya Idukilo Mkoani Shinyanga aliyekuwa akichimba madini katika Kijiji cha Mwang’holo, Kata ya Mwadui Lohumbo anadaiwa kuuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi wanaolinda eneo la Mwekezaji Kampuni ya El-Hillal
Nenda nyamongo kule uone jinsi raia wanavyopewa risasi kama kuku. Leo kuna msiba raia anazikwa alipewa risasi na askari.

Ile dhana ya askari hawezi kukupiga risasi ukimkimbia inakufa polepole.
 
Nenda nyamongo kule uone jinsi raia wanavyopewa risasi kama kuku. Leo kuna msiba raia anazikwa alipewa risasi na askari.

Ile dhana ya askari hawezi kukupiga risasi ukimkimbia inakufa polepole.
Ni kweli hawa polis wanaua vijana wengi tu tena kama nyamongo imekuwa kama kitu cha kawaida kabsa mtu anauliwa nje kbsa ya eneo la mgodi halafu kabsa polisi wanaishi hapa hapa nyamongo na bado wanatoa sababu za kipuuzi jua ya haya mauaji ya vijana wa kitanzania tena wazawa
 
Ni kweli hawa polis wanaua vijana wengi tu tena kama nyamongo imekuwa kama kitu cha kawaida kabsa mtu anauliwa nje kbsa ya eneo la mgodi halafu kabsa polisi wanaishi hapa hapa nyamongo na bado wanatoa sababu za kipuuzi jua ya haya mauaji ya vijana wa kitanzania tena wazawa
Inauma sana lakini ndio hvio. Mwenye nguvu
 
Inauma sana lakini ndio hvio. Mwenye nguvu
Mkuu siyo mwenye nguvu sema tumelelewa katika misingi mibovu sana ndo maana hata polisi wanajua wananchi hawana cha kuwafanya maana hata sheria zetu bado ni mbovu sana, vijana wa nigeria walisimama kama nguvu ya umma dhidi ya polisi wao
 
Hatari sana; ila tujifunze, kama 'huruhusiwi kwenda eneo fulani, tusiende', kwenda tofauti maana yake ni uvamizi au wizi.
 
Hatari sana; ila tujifunze, kama 'huruhusiwi kwenda eneo fulani, tusiende', kwenda tofauti maana yake ni uvamizi au wizi.
Mkuu shida kubwa ni moja tu, watu walio zoea kitu fulani yaani ndo kama maisha yao mfano wachimbaji ni ngumu sana kuacha hizo kazi, na ujue mwekezaji mkubwa anapokuja anachukua sehemu kubwa ya aridhi ambayo watu hapo awali walikuwa wanaitumia kuingiza kipato na wanaifahamu vizuri , swali je mwekezaji anapokuja anakuja na alternative gani kupunguza hiyo changamoto kwa wazawa?
 
Hizi bunduki zikabidhiwe kwa watu wenye akili timamu.

Kwa jinsi inavyoonekana, mapolisi wetu wengi wao hawako sawasawa kiakili.

Ni kufyatua tu kila mahali na kwa kila mtu. HAPANA.
 
Mkuu shida kubwa ni moja tu, watu walio zoea kitu fulani yaani ndo kama maisha yao mfano wachimbaji ni ngumu sana kuacha hizo kazi, na ujue mwekezaji mkubwa anapokuja anachukua sehemu kubwa ya aridhi ambayo watu hapo awali walikuwa wanaitumia kuingiza kipato na wanaifahamu vizuri , swali je mwekezaji anapokuja anakuja na alternative gani kupunguza hiyo changamoto kwa wazawa?
Mwekezaji yeye hausiki na wazawa, ila aliyepokea hela ya mauzo ya ardhi ndio anatakiwa abuni wazawa wataishije. Kwa mtu mmoja mmoja, itabidi wao binafsi watafute njia mbadala ya kujipatia kipato.
 
Hizi bunduki zikabidhiwe kwa watu wenye akili timamu.

Kwa jinsi inavyoonekana, mapolisi wetu wengi wao hawako sawasawa kiakili.

Ni kufyatua tu kila mahali na kwa kila mtu. HAPANA.
Polisi wengi wanafanya kazi kwa mazoea ama wana mawazo sana, mambo ya madili ya pesa na michongo na pia usimamizi mbovu wa sheria zetu na ile kulindana sana, maeneo yote ya migodini yani mwisho wake yaani zile bicon ila cha ajabu kabisa polisi wa mgodi wa north mara wanakimbiza watu mpaka mto mara yaani ni mbaliii sana na eneo la mgodi sasa tujiulize kama siyo mazoea ni nini na hata hili tukio la juzi polisi wamempiga kijana risasi nje kbsa ya eneo husika
 
Mwekezaji yeye hausiki na wazawa, ila aliyepokea hela ya mauzo ya ardhi ndio anatakiwa abuni wazawa wataishije. Kwa mtu mmoja mmoja, itabidi wao binafsi watafute njia mbadala ya kujipatia kipato.
Ni kweli kabisa anaehusika hapo ili mambo yote yawe sawa huwa lazima kuwe na mwekezaji, serikali kupitia wizara husika na wananchi wa eneo husika ila ukweli ni kwamba kwenye huu mchakato wananchi hasa wazawa huwa ni kama wanaachwa tu nyuma bila kujariwa na serikali husika, mnafaika mkubwa hapo ni mwekezaji na serikali yetu basi, sasa watu waliozoea kuchimba miaka yote unafikiri wataishije
 
Nenda nyamongo kule uone jinsi raia wanavyopewa risasi kama kuku. Leo kuna msiba raia anazikwa alipewa risasi na askari.

Ile dhana ya askari hawezi kukupiga risasi ukimkimbia inakufa polepole.
Alipewa risasi aipeleke wp!?nyoosha kiswahili bwashee
 
Ni kweli kabisa anaehusika hapo ili mambo yote yawe sawa huwa lazima kuwe na mwekezaji, serikali kupitia wizara husika na wananchi wa eneo husika ila ukweli ni kwamba kwenye huu mchakato wananchi hasa wazawa huwa ni kama wanaachwa tu nyuma bila kujariwa na serikali husika, mnafaika mkubwa hapo ni mwekezaji na serikali yetu basi, sasa watu waliozoea kuchimba miaka yote unafikiri wataishije
Serikali ya mtaa/kijiji, wilaya n.k nadhani mkikaa pamoja mnaweza kufikia muafaka iwapo kama mmoja wenu hatoshawishika.
 
Back
Top Bottom