Katika mizunguko yangu, nilipita katika eneo la Kigamboni, Kata ya Vijibweni, Mtaa wa Mkwajuni ambapo nilikutana na shimo kubwa lililozungukwa na makazi ya watu, eneo hilo ambalo limejaa takataka, linafanana na jalala lililoachwa wazi.
Kwa kuwa nilikuwa mgeni, nilidhani pengine ni sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya kutupia taka. Hata hivyo, nilipouliza baadhi ya wenyeji, walinieleza kuwa shimo hilo limekuwepo kwa miaka kadhaa, likizidi kutanuka na kuleta madhara kwa wakazi wa maeneo jirani.
Wakazi waliniambia kwamba, mvua zinaponyesha, shimo hili hujaa maji na kusababisha mafuriko yanayoingia katika nyumba zao, hali ambayo imefanya baadhi ya nyumba kulegea kwenye misingi, na baadhi kubomoka.
Nilipozungumza na wakazi wa eneo hilo kuhusu jinsi wanavyokabiliana na tatizo hili, walieleza kuwa baadhi yao wameamua kujenga upya misingi ya nyumba zao kwa kuimarisha kuta zinazozunguka nyumba ili kuzuia athari zitokazo na maji kutuama katika shimo hilo.
Wakazi walijaribu kuziba shimo hili kwa kutupa takataka ndani yake ili kuzuia mafuriko, lakini walikataliwa na serikali ya mtaa na halmashauri kwa madai kuwa kuweka takataka kwenye shimo hilo ni hatari kwa afya zao.
Kwa sababu ya tatizo hili kuwa kubwa, mnamo tarehe 9 mwezi wa 8, 2024 viongozi walikubaliana na Diwani wa kata hiyo kuleta vifusi ili kuziba shimo hilo kwa haraka iwezekanavyo. Wananchi walifurahi wakiamini kuwa suluhisho la kudumu limepatikana.
Wananchi wanasema walishtushwa baada ya siku kadhaa walipokuta pembezoni mwa shimo hilo kumejaa lundo la takataka badala ya vifusi walivyoahidiwa. Wakazi walipohoji kuhusu ujio wa takataka hizo, waliambiwa kuwa diwani alileta takataka hizo kwa ajili ya kujaza shimo.
Picha ikionesha takataka zilizomwagwa pembezoni mwa shimo
Wakazi wa Vijibweni wanasema wameshangazwa na hatua hiyo kwani awali waliambiwa kuwa kuweka takataka kwenye shimo ni hatari kwa afya, lakini sasa diwani ameamua kutupia takataka hizo akidai ni kwa ajili ya kuziba shimo hilo. Wananchi wanajiuliza, "Je, takataka hizi zilizoletwa na diwani si hatari kwa afya zetu?"
Katika uchunguzi wangu, nimebaini kuwa baada ya takataka kumwagwa, baadhi ya wananchi wamegeuza eneo hilo kuwa jalala rasmi, wakiamini kuwa ni rahisi kumwaga taka hapo kuliko kulipia gharama za magari ya kuzolea taka. Hali hii inazidi kuweka mazingira hatarishi kwa wakazi wa Vijibweni na kuongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa.
Kwa kuwa suala hili lilifikishwa kwa viongozi, nilimtafuta diwani wa eneo hilo ili kujua kwa nini ahadi ya kuleta vifusi na kuziba shimo haijatimizwa, na badala yake takataka ndizo zimewekwa. Diwani alinijibu kuwa anahitaji muda zaidi kulizungumzia suala hili kwa kina.
Wakazi wa eneo hili wanalalamikia sana uwepo wa shimo hili, hasa kwa sababu ya kuongezeka kwa mbu wanaoeneza malaria.
Ni kawaida kwa wakazi hao kwenda hospitali mara kwa mara kupima malaria kutokana na hofu ya kuambukizwa maradhi hayo. Ni wazi kuwa shimo hili limekuwa chanzo cha hatari kwa afya na maisha ya watu wa eneo hili.
Mimi kama mwananchi, natoa wito kwa uongozi wa Wilaya ya Kigamboni kuchukua hatua mara moja kushughulikia tatizo hili.
Afya na usalama wa Wananchi uko hatarini, na ni jukumu la viongozi kuhakikisha kuwa maisha ya watu hayapo kwenye hatari kama hii.
Je, Serikali iko tayari kuendelea kushuhudia madhara makubwa zaidi kwa wakazi wa Vijibweni?
Kwa kuwa nilikuwa mgeni, nilidhani pengine ni sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya kutupia taka. Hata hivyo, nilipouliza baadhi ya wenyeji, walinieleza kuwa shimo hilo limekuwepo kwa miaka kadhaa, likizidi kutanuka na kuleta madhara kwa wakazi wa maeneo jirani.
Wakazi waliniambia kwamba, mvua zinaponyesha, shimo hili hujaa maji na kusababisha mafuriko yanayoingia katika nyumba zao, hali ambayo imefanya baadhi ya nyumba kulegea kwenye misingi, na baadhi kubomoka.
Nilipozungumza na wakazi wa eneo hilo kuhusu jinsi wanavyokabiliana na tatizo hili, walieleza kuwa baadhi yao wameamua kujenga upya misingi ya nyumba zao kwa kuimarisha kuta zinazozunguka nyumba ili kuzuia athari zitokazo na maji kutuama katika shimo hilo.
Wakazi walijaribu kuziba shimo hili kwa kutupa takataka ndani yake ili kuzuia mafuriko, lakini walikataliwa na serikali ya mtaa na halmashauri kwa madai kuwa kuweka takataka kwenye shimo hilo ni hatari kwa afya zao.
Kwa sababu ya tatizo hili kuwa kubwa, mnamo tarehe 9 mwezi wa 8, 2024 viongozi walikubaliana na Diwani wa kata hiyo kuleta vifusi ili kuziba shimo hilo kwa haraka iwezekanavyo. Wananchi walifurahi wakiamini kuwa suluhisho la kudumu limepatikana.
Wananchi wanasema walishtushwa baada ya siku kadhaa walipokuta pembezoni mwa shimo hilo kumejaa lundo la takataka badala ya vifusi walivyoahidiwa. Wakazi walipohoji kuhusu ujio wa takataka hizo, waliambiwa kuwa diwani alileta takataka hizo kwa ajili ya kujaza shimo.
Picha ikionesha takataka zilizomwagwa pembezoni mwa shimo
Wakazi wa Vijibweni wanasema wameshangazwa na hatua hiyo kwani awali waliambiwa kuwa kuweka takataka kwenye shimo ni hatari kwa afya, lakini sasa diwani ameamua kutupia takataka hizo akidai ni kwa ajili ya kuziba shimo hilo. Wananchi wanajiuliza, "Je, takataka hizi zilizoletwa na diwani si hatari kwa afya zetu?"
Katika uchunguzi wangu, nimebaini kuwa baada ya takataka kumwagwa, baadhi ya wananchi wamegeuza eneo hilo kuwa jalala rasmi, wakiamini kuwa ni rahisi kumwaga taka hapo kuliko kulipia gharama za magari ya kuzolea taka. Hali hii inazidi kuweka mazingira hatarishi kwa wakazi wa Vijibweni na kuongeza hatari ya kuenea kwa magonjwa.
Kwa kuwa suala hili lilifikishwa kwa viongozi, nilimtafuta diwani wa eneo hilo ili kujua kwa nini ahadi ya kuleta vifusi na kuziba shimo haijatimizwa, na badala yake takataka ndizo zimewekwa. Diwani alinijibu kuwa anahitaji muda zaidi kulizungumzia suala hili kwa kina.
Wakazi wa eneo hili wanalalamikia sana uwepo wa shimo hili, hasa kwa sababu ya kuongezeka kwa mbu wanaoeneza malaria.
Ni kawaida kwa wakazi hao kwenda hospitali mara kwa mara kupima malaria kutokana na hofu ya kuambukizwa maradhi hayo. Ni wazi kuwa shimo hili limekuwa chanzo cha hatari kwa afya na maisha ya watu wa eneo hili.
Mimi kama mwananchi, natoa wito kwa uongozi wa Wilaya ya Kigamboni kuchukua hatua mara moja kushughulikia tatizo hili.
Afya na usalama wa Wananchi uko hatarini, na ni jukumu la viongozi kuhakikisha kuwa maisha ya watu hayapo kwenye hatari kama hii.
Je, Serikali iko tayari kuendelea kushuhudia madhara makubwa zaidi kwa wakazi wa Vijibweni?