Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Siku zote nilikuwa nikijiuliza, hivi hawa wenye makampuni ya simu wanapata vipi faida kwa mtindo wa shilingi moja kwa sekunde katika kipindi hiki ambapo karibu kila mtu ana simu (mijini) na cha zaidi Mchina anatengeneza simu zenye line mbili? Na je, kwa mwendo wa vocha za 300, 500, na nipige tafu faida itapatikana wapi?
Baada ya kuzagaa kwa taarifa za ujumbe unaohusu "kuichangia CCM kwa lazima", sasa naweza kujua kwa nini tunadanganywa gharama za kupiga simu zimeshuka. Kuna uwezekano mkubwa kwamba CCM wamewalipa makampuni ya simu pesa ya kutosha kabisa ili makampuni yashushe bei na kwa hiyo, kimya-kimya watumiaji wa mitandao wanakatwa salio bila kujua.
Inakuwaje CCM wanatapatapa namna hii jamani? Siri zote tunazipata kutoka huko huko kwenu CCM. Fanyeni ghiliba zote. Tutazinyaka. Hata mfanyie kuzimu. Tutazinyaka.
Kila nafsi itaonja mauti jamani. Tulieni.
Baada ya kuzagaa kwa taarifa za ujumbe unaohusu "kuichangia CCM kwa lazima", sasa naweza kujua kwa nini tunadanganywa gharama za kupiga simu zimeshuka. Kuna uwezekano mkubwa kwamba CCM wamewalipa makampuni ya simu pesa ya kutosha kabisa ili makampuni yashushe bei na kwa hiyo, kimya-kimya watumiaji wa mitandao wanakatwa salio bila kujua.
Inakuwaje CCM wanatapatapa namna hii jamani? Siri zote tunazipata kutoka huko huko kwenu CCM. Fanyeni ghiliba zote. Tutazinyaka. Hata mfanyie kuzimu. Tutazinyaka.
Kila nafsi itaonja mauti jamani. Tulieni.