Elections 2010 Shilingi Moja Kwa Sekunde Masaa 24 na Kuichangia CCM

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Siku zote nilikuwa nikijiuliza, hivi hawa wenye makampuni ya simu wanapata vipi faida kwa mtindo wa shilingi moja kwa sekunde katika kipindi hiki ambapo karibu kila mtu ana simu (mijini) na cha zaidi Mchina anatengeneza simu zenye line mbili? Na je, kwa mwendo wa vocha za 300, 500, na nipige tafu faida itapatikana wapi?

Baada ya kuzagaa kwa taarifa za ujumbe unaohusu "kuichangia CCM kwa lazima", sasa naweza kujua kwa nini tunadanganywa gharama za kupiga simu zimeshuka. Kuna uwezekano mkubwa kwamba CCM wamewalipa makampuni ya simu pesa ya kutosha kabisa ili makampuni yashushe bei na kwa hiyo, kimya-kimya watumiaji wa mitandao wanakatwa salio bila kujua.


Inakuwaje CCM wanatapatapa namna hii jamani? Siri zote tunazipata kutoka huko huko kwenu CCM. Fanyeni ghiliba zote. Tutazinyaka. Hata mfanyie kuzimu. Tutazinyaka.

Kila nafsi itaonja mauti jamani. Tulieni.
 
Mkuu,

Hivi huu ujumbe wako una uhusiano na huu ujumbe? Kama ni kweli basi naomba MODS muunganishe huu ujumbe ili ulete mtiririko mzuri. Tunaomba watu wajulishwe ili wajitoe na ikiwezekana siku ya Nyerere Day basi Mawakili wayashitaki haya mashirika kwa niaba ya Watanzania woote ili waipate habari yao.

wana jf na watanzania wenzangu!!

tuma ujumbe kwa mtandao wowote ule wenye neno "hapana" kwenda kwenye namba 15016 kuna jibu linalokuja na linaonyesha kwamba watanzania tumeliwa hela nyingi sana kwa ujumbe unaoonyesha kwamba ccm imekuwa na mpango maalum wa kuichangia ishinde, tena bila idhini ya watanzania!!!

tunza ujumbe huo mara utakapoupata, ni silaha ya kuing'oa ccm na kampeni zao chafu!!
 
Mkuu,

Hivi huu ujumbe wako una uhusiano na huu ujumbe? Kama ni kweli basi naomba MODS muunganishe huu ujumbe ili ulete mtiririko mzuri. Tunaomba watu wajulishwe ili wajitoe na ikiwezekana siku ya Nyerere Day basi Mawakili wayashitaki haya mashirika kwa niaba ya Watanzania woote ili waipate habari yao.

Ndiyo mkuu
 
Back
Top Bottom