Nyanswe Nsame
Senior Member
- Jul 9, 2019
- 158
- 175
Milioni 251 zatengwa kulipana posho kuondoa machinga Jiji la Mwanza.
Wanaolipwa CD, DC na wenzao
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida jiji la Mwanza limetenga Sh. milioni 251 kwa ajili ya kulipana posho watumishi wake kwa siku 10 ili kusimamia zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu Machinga katikati ya jiji na kwenda maeneo waliyotengewa.
Kadhalika, jiji hilo limetenga Sh. milioni 10 kwa ajili ya kuchimba mtaro wenye urefu wa wa mita 100 katika uwanja wa Mchafukuoga uliokuwa ukitumiwa na shule nane zikiwamo za msingi na sekondari kwa ajili ya michezo ili kuuweka sawa kwa ajili kuhamishia machinga 2500 wa mtaa wa Makoroboi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mmoja wa Diwani aliyeshiriki kupitisha bajeti hiyo ya jiji iliyopitishwa Oktoba 5 mwaka huu, alisema fedha hizo ni nyingi, lakini cha kushangaza madiwani asilimia 99 walikubali kuipitisha.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, diwani huyo alifunguka kwamba huo ni ufisadi wa kutisha kwa sababu kuhamisha machinga hakuhitaji fedha nyingi kiasi hicho.
Alifafanua kwamba machinga walio wengi wamekubali wenyewe kuhama na huko wanapopelekwa hawajengewi vibanda wala hawalipwi gharama za kuhamisha biashara zao.
"Hizi fedha ni nyingi sana ndugu mwandishi na cha kushangaza hawa madiwani wote walikubali kupitisha bajeti hii ambayo waandishi wa habari walitolewa nje ya kikao cha baraza la madiwani,'' alisema.
Aliongeza kuwa katika bajeti hiyo waandishi wa habari nao wametengewa posho zao ili kuandika mambo mazuri pekee katika zoezi la kuhamisha machinga hao.
Alifafanua kuwa jiji lina magari yenye vipaza sauti ambayo yanapita kila kona walipo machinga na kuwataka wahame na kuwaelekeza sehemu za kwenda, lakini anashangaa kuona fedha hizo zinatengwa kwa ajili ya kuratibu zoezi hilo.
Kuhusu uwanja huo wa michezo, diwani huyo alisema, Serikali ilielekeza maeneo ambayo hayapaswi kupelekwa machinga kuwa ni pamoja na kuvamia viwanja vya shule.
Alisema shule hizo zilizopo kata ya Igogo watoto wake kwa sasa hawatakuwa na sehemu za kuchezea na kwamba kutakuwa na mwingiliano wa watu wengi hatua ambayo inaweza kuharibu masomo ya watoto hao.
Kuhusu kutengwa Sh. milioni 10 kwa ajili kuchimba mtaro na kusambaza udongo katika uwanja huo, alisema kiasi hicho pia ni kikubwa kwa kuwa jiji lina magari na magreda yake ambayo kama yangetumiwa wangeweza kuokoa fedha nyingi.
Akizungumzia kupitishwa kwa bajeti hiyo ya mamilioni, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Sekiete Yahaya alisema suala hilo siyo kweli na kushindwa kueleza ukweli.
Alipoulizwa kikao cha Oktoba 5 mwaka huu cha baraza la madiwani ambacho kiliitishwa kwa dharura kilikuwa na ajenda gani alikata simu na alipopigiwa hakupokea tena.
Aidha, alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno kutaka ufafanuzi, Mkurugenzi huyo hakujibu kitu siku nzima ya jana.
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi, alipotafutwa kuzungumza tuhuma hizo, alidai yeye sio anayepanga bajeti ya Jiji la Mwanza ambapo awali Mkurugenzi wa Jiji hilo Yahaya alidai zoezi hilo linaratibiwa na Mkuu huyo wa wilaya.
Zoezi la kuhamisha machinga na kuwapeleka maeneo waliyopangiwa linaendelea jijini Mwanza na linatarajia kukamilika Oktoba 14 mwaka huu.
Wanaolipwa CD, DC na wenzao
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida jiji la Mwanza limetenga Sh. milioni 251 kwa ajili ya kulipana posho watumishi wake kwa siku 10 ili kusimamia zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu Machinga katikati ya jiji na kwenda maeneo waliyotengewa.
Kadhalika, jiji hilo limetenga Sh. milioni 10 kwa ajili ya kuchimba mtaro wenye urefu wa wa mita 100 katika uwanja wa Mchafukuoga uliokuwa ukitumiwa na shule nane zikiwamo za msingi na sekondari kwa ajili ya michezo ili kuuweka sawa kwa ajili kuhamishia machinga 2500 wa mtaa wa Makoroboi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mmoja wa Diwani aliyeshiriki kupitisha bajeti hiyo ya jiji iliyopitishwa Oktoba 5 mwaka huu, alisema fedha hizo ni nyingi, lakini cha kushangaza madiwani asilimia 99 walikubali kuipitisha.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, diwani huyo alifunguka kwamba huo ni ufisadi wa kutisha kwa sababu kuhamisha machinga hakuhitaji fedha nyingi kiasi hicho.
Alifafanua kwamba machinga walio wengi wamekubali wenyewe kuhama na huko wanapopelekwa hawajengewi vibanda wala hawalipwi gharama za kuhamisha biashara zao.
"Hizi fedha ni nyingi sana ndugu mwandishi na cha kushangaza hawa madiwani wote walikubali kupitisha bajeti hii ambayo waandishi wa habari walitolewa nje ya kikao cha baraza la madiwani,'' alisema.
Aliongeza kuwa katika bajeti hiyo waandishi wa habari nao wametengewa posho zao ili kuandika mambo mazuri pekee katika zoezi la kuhamisha machinga hao.
Alifafanua kuwa jiji lina magari yenye vipaza sauti ambayo yanapita kila kona walipo machinga na kuwataka wahame na kuwaelekeza sehemu za kwenda, lakini anashangaa kuona fedha hizo zinatengwa kwa ajili ya kuratibu zoezi hilo.
Kuhusu uwanja huo wa michezo, diwani huyo alisema, Serikali ilielekeza maeneo ambayo hayapaswi kupelekwa machinga kuwa ni pamoja na kuvamia viwanja vya shule.
Alisema shule hizo zilizopo kata ya Igogo watoto wake kwa sasa hawatakuwa na sehemu za kuchezea na kwamba kutakuwa na mwingiliano wa watu wengi hatua ambayo inaweza kuharibu masomo ya watoto hao.
Kuhusu kutengwa Sh. milioni 10 kwa ajili kuchimba mtaro na kusambaza udongo katika uwanja huo, alisema kiasi hicho pia ni kikubwa kwa kuwa jiji lina magari na magreda yake ambayo kama yangetumiwa wangeweza kuokoa fedha nyingi.
Akizungumzia kupitishwa kwa bajeti hiyo ya mamilioni, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Sekiete Yahaya alisema suala hilo siyo kweli na kushindwa kueleza ukweli.
Alipoulizwa kikao cha Oktoba 5 mwaka huu cha baraza la madiwani ambacho kiliitishwa kwa dharura kilikuwa na ajenda gani alikata simu na alipopigiwa hakupokea tena.
Aidha, alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno kutaka ufafanuzi, Mkurugenzi huyo hakujibu kitu siku nzima ya jana.
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi, alipotafutwa kuzungumza tuhuma hizo, alidai yeye sio anayepanga bajeti ya Jiji la Mwanza ambapo awali Mkurugenzi wa Jiji hilo Yahaya alidai zoezi hilo linaratibiwa na Mkuu huyo wa wilaya.
Zoezi la kuhamisha machinga na kuwapeleka maeneo waliyopangiwa linaendelea jijini Mwanza na linatarajia kukamilika Oktoba 14 mwaka huu.