Mahesabu
JF-Expert Member
- Jan 27, 2008
- 5,972
- 3,830
Kifo cha kusikitisha kimetokea Manzese Midizini, Shilingi 200 ikiwa ni sababu.
Mtu mmoja ameuawa kwa kuchomwa kisu maeneo ya shingoni, mashuhuda wameeleza kuwa kijana mmoja (marehemu) akiwa anafahamiana na mwenzake (muuaji) wakati ametoka shule/chuo alipita mahali walipo rafiki zake. Ndipo mmoja akamfata na kumuomba/kumlazimisha ampe shilingi mia mbili.
Marehemu akatoa elfu moja ili akate mia mbili anayohitaji. Kwa namna isiyoeleweka kwa urahisi bila marehemu kuleta purukashani zozote mwenzake akamchoma kisu.
Baada ya kuona damu nyingi huku marehemu akilalama kwa kumtaja na jina (dying declaration) "fulani unaniua kwa sababu ya 200?" Ndipo kijana huyo wa kipemba akaomba amsamehe kwani hakukusudia kumfanyia hivyo.
Waliokuwa karibu wakataka kumshambulia kijana huyo wa kipemba marehemu akawasihi wasimpige, Kulikuwa na gari karibu aina ya NOAH ( ya Man-rasta) marehem akawaishwa hospitali na muuji kujisalimisha polisi Magomeni.
Marehemu amepelekwa kuzikwa Morogoro (Dumila/Dakawa).
Mtu mmoja ameuawa kwa kuchomwa kisu maeneo ya shingoni, mashuhuda wameeleza kuwa kijana mmoja (marehemu) akiwa anafahamiana na mwenzake (muuaji) wakati ametoka shule/chuo alipita mahali walipo rafiki zake. Ndipo mmoja akamfata na kumuomba/kumlazimisha ampe shilingi mia mbili.
Marehemu akatoa elfu moja ili akate mia mbili anayohitaji. Kwa namna isiyoeleweka kwa urahisi bila marehemu kuleta purukashani zozote mwenzake akamchoma kisu.
Baada ya kuona damu nyingi huku marehemu akilalama kwa kumtaja na jina (dying declaration) "fulani unaniua kwa sababu ya 200?" Ndipo kijana huyo wa kipemba akaomba amsamehe kwani hakukusudia kumfanyia hivyo.
Waliokuwa karibu wakataka kumshambulia kijana huyo wa kipemba marehemu akawasihi wasimpige, Kulikuwa na gari karibu aina ya NOAH ( ya Man-rasta) marehem akawaishwa hospitali na muuji kujisalimisha polisi Magomeni.
Marehemu amepelekwa kuzikwa Morogoro (Dumila/Dakawa).