Shikamoo wewe kipofu uliyeniibia pikipiki na ukaiendesha

Huo wizi upo sana, ila mara nyingi hua wanapanda mwanamke na mwamaume halafu mdada andosndosha kiatu halafu wanakuomba ushuke uwaokotee, hilo vumbi lake watalokuachia sio la nchi hii.
 
SHIKAMONI/MARAHABAA

STORY YAHUSU: NILIVYOIBIWA BOBABODA MAGOMENI JIJINI DSM

Nipo zangu kijiweni nikisubiri abiria mara paap wanakuja wanaume wawili mmja mtu wa makamo miaka 40/55 amevaa miwani meusi akionekana ni mtu mwenye ulemavu wa macho (kipofu) na mwingine ambae ni kijana Kati ya miaka 18/25 akimsadia kumuongoza njia huku wote wamekamata fimbo moja.

Wamefika kwangu baada ya salamu fupi yule kijana akanambia "oya abiria anaenda Manzese darajani ni shilingi ngapi"? Nikamwambia buku tatu (3000) kipofu na yeye akaongea na kuniomba kwmba nimsaidia ana buku 2 (2000) tu..

Nikakubali nikampakia na kuanza safari mbele kdogo kipofu akaangusha fimbo yake akaniambia "kijana samahani fimbo yangu imenianguka" fasta nikasimama nikageuka nyuma kweli nikaiona haikuwa mbali na niliposimama kama hatua 15 hivi ila ni katikati ya barabara nikaona bora niende kwa miguu

Sasa kumbe mluguru mimi nilijichanganya kwenda kumuokotea fimbo yake bila kuizima boxer yangu.kudadeq hatua kama kumi hivi nikasikia chombo inapigwa race ya kufa mtu KUGEUKA NYUMA MTUMEEE KIPOFU ANAENDESHA PIKIPIKI MWEEEE
Mwenzako aliangushiwa gongo la kilema pikipiki ikaenda yeye akabaki na gongo.
 
SHIKAMONI/MARAHABAA

STORY YAHUSU: NILIVYOIBIWA BOBABODA MAGOMENI JIJINI DSM

Nipo zangu kijiweni nikisubiri abiria mara paap wanakuja wanaume wawili mmja mtu wa makamo miaka 40/55 amevaa miwani meusi akionekana ni mtu mwenye ulemavu wa macho (kipofu) na mwingine ambae ni kijana Kati ya miaka 18/25 akimsadia kumuongoza njia huku wote wamekamata fimbo moja.

Wamefika kwangu baada ya salamu fupi yule kijana akanambia "oya abiria anaenda Manzese darajani ni shilingi ngapi"? Nikamwambia buku tatu (3000) kipofu na yeye akaongea na kuniomba kwmba nimsaidia ana buku 2 (2000) tu..

Nikakubali nikampakia na kuanza safari mbele kdogo kipofu akaangusha fimbo yake akaniambia "kijana samahani fimbo yangu imenianguka" fasta nikasimama nikageuka nyuma kweli nikaiona haikuwa mbali na niliposimama kama hatua 15 hivi ila ni katikati ya barabara nikaona bora niende kwa miguu

Sasa kumbe mluguru mimi nilijichanganya kwenda kumuokotea fimbo yake bila kuizima boxer yangu.kudadeq hatua kama kumi hivi nikasikia chombo inapigwa race ya kufa mtu KUGEUKA NYUMA MTUMEEE KIPOFU ANAENDESHA PIKIPIKI MWEEEE
Kwa bei uliyowapa ya book 3 Magomeni hadi Manzese, wewe sio dereva wa boda boda na hii hadithi umetunga maana hata bei za boda huzijui.

Na kama ni kweli wewe ni dereva wa bodaboda unawapiga watu kwa bei ya kitapeli kama hiyo na tena kipofu - ulistahili kuibiwa, karma hiyo!
 
Kuna jamaa aliibiwa piki piki yake maeneo ruaha(anakofanyia shughuli zake) ilimuuma sana akaelekezwa kwa mtaalam pale mahenge morogoro. Yule mama alimwambia usijali baba we endelea shughuli zako. Baada ya siku3 jamaa alieiba aliipeleka mwenyewe kituo cha polisi pale ruaha na akasema anamtafuta sana mwenye nayo... kwa iyo njia za kupata mali zako zipo... kuwa na connection tu.
 
Kwa bei uliyowapa ya book 3 Magomeni hadi Manzese, wewe sio dereva wa boda boda na hii hadithi umetunga maana hata bei za boda huzijui.

Na kama ni kweli wewe ni dereva wa bodaboda unawapiga watu kwa bei ya kitapeli kama hiyo na tena kipofu - ulistahili kuibiwa, karma hiyo!
Huwezi ukaanza bei ya chini kwenye biashara za kuelewana bei,nilimwmbia 3000 lakini hata angesema ana buku jero ningeenda (Ulemavu sio sababu ya kulipa nauli ndogo kwangu)
 
Kuna jamaa aliibiwa piki piki yake maeneo ruaha(anakofanyia shughuli zake) ilimuuma sana akaelekezwa kwa mtaalam pale mahenge morogoro. Yule mama alimwambia usijali baba we endelea shughuli zako. Baada ya siku3 jamaa alieiba aliipeleka mwenyewe kituo cha polisi pale ruaha na akasema anamtafuta sana mwenye nayo... kwa iyo njia za kupata mali zako zipo... kuwa na connection tu.
Aisee dah mkuu nipo ifakara sahizi lakini nilishaamua kumuachia Mungu
 
Huwezi ukaanza bei ya chini kwenye biashara za kuelewana bei,nilimwmbia 3000 lakini hata angesema ana buku jero ningeenda (Ulemavu sio sababu ya kulipa nauli ndogo kwangu)
Huwezi kuanza na 3000 kwenye nauli ya 1000. HUo ni utapeli tu. Vipi kama ni mgeni, si utamwibngiza mjini. Kwanza kwa nini usimwambie nauli inayotozwa, kwa nini utarajie mbishane kwanza ndio mkubaliane?
 
Back
Top Bottom