Affet
JF-Expert Member
- Jul 8, 2018
- 1,189
- 1,663
Hiki ni kipindi cha mvua jinga weweAsante CEO Barbara Gonzalez na Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu na Mwenyekiti wa Bodi ya Simba SC Salim Abdallah 'Try Again' kwa Kusikiliza Ushauri wa Wanachama na Kazi imeshamalizika hivyo leo wana Simba SC tunaenda kupata Furaha ya Ushindi.
Kwa Uchawi uliofanyika, Umakini mkubwa wa Kuificha Timu, na Watu Kulishana Yamini ili kutunza Siri na Kutosalitiana, kutafuta Wataalam makini na kuwapa Pesa yao waitakayo na kwa Mshikamano wetu nimeamini Simba SC ni Nguvu Moja kweli.
Jana usiku kuna Mtu Mmoja wa Kamati ya Uchawi na Fitna wa Simba SC aliniambia kuwa leo kati ya Saa 12 hadi Saa 4 Asubuhi nitaona ama Mvua au Manyunyu na nikiyaona tu jua Kazi imeshamalizika na Kukamilika hivyo Yanga SC anafungwa na kweli hilo limetokea na nimelishuhudia Mubashara.
Asanteni Simba SC Matawi ya Morogoro, Kikwajuni Zanzibar, Tanga, Ruvuma, Tabora na Dar es Salaam hakika Kazi yenu mmeifanya na KEROZENE nimeishuhudia. Watake wasitake Yanga SC wanakufa na wakiponapona basi wataambulia tu Sare.