Shigongo: Sitagombea tena ubunge maisha yangu yote!

mambali

Senior Member
Oct 16, 2012
172
64
mkurugenzi mtendaji wa Global Publisher Ndg Erick Shigongo amesema katika maisha yake yote yaliyobaki hapa Duniani Atagombea tena Ubunge ameyasema hayo wakati akikabidhi msaada wa Gari la Wagonjwa Huko Sengerema amesema kuwasaidia watu sio lazima uwe Mbunge ndipo uweze kutoa msaada yeye ajatoa msaada wa gari kwa nia ya kugombea ubunge bali ni moyo wa kutoa hivyo ajatoa kwa nia ya kuwa mbunge.

N.B JE MH E.LOWASA NAYE ANATOA MISAADA LAKINI HANA MPANGO WA KUWANIA URAISI?????
 
Ni kawaida ya wanaisa uchwara kama wakina Zitto na Membe, kwa kauli za uongo uongo
 
kwani akigombea au asipogombea ana kipi cha maana? Huyu nae ni mnafiki kama wanafiki wengine.
 
Katika watu wasioaminika hapa tz au kutabirika ni huyo jamaa.......shigongo hana rafiki wakudumu wala adui wa kuduma....na hilo jimbo analitaka kwa udi na uvumbi hata naibu waziri ambaye ndiye mbunge wa jimbo la buchosa analijua hilo
 
mkurugenzi mtendaji wa Global Publisher Ndg Erick Shigongo amesema katika maisha yake yote yaliyobaki hapa Duniani Atagombea tena Ubunge ameyasema hayo wakati akikabidhi msaada wa Gari la Wagonjwa Huko Sengerema amesema kuwasaidia watu sio lazima uwe Mbunge ndipo uweze kutoa msaada yeye ajatoa msaada wa gari kwa nia ya kugombea ubunge bali ni moyo wa kutoa hivyo ajatoa kwa nia ya kuwa mbunge.

N.B JE MH E.LOWASA NAYE ANATOA MISAADA LAKINI HANA MPANGO WA KUWANIA URAISI?????

Kiswahili sahihi ni "hatagombea" na si "atagombea" hizi ni maana mbili, tofauti wahitimu wa sasa mbona ha na a inawasumbua sana???
 
Kiswahili sahihi ni "hatagombea" na si "atagombea" hizi ni maana mbili, tofauti wahitimu wa sasa mbona ha na a inawasumbua sana???

hata mimi amenichanganya sana jamaa au ndo division 5
 
Aisee, yaani huwa inaniudhi sana humu ndani. Hata kama hawakusoma, ila hawawezi kuona wengine wanaandikaje?

"Aise, yaani Uwa inaniuZi sana Umu ndani. Ata kama Awakusoma, ila Awawezi kuona wengine wanaandikaje?"
Kiswahili sahihi ni "hatagombea" na si "atagombea" hizi ni maana mbili, tofauti wahitimu wa sasa mbona ha na a inawasumbua sana???
 
Huyu anaumizaga sana watu kupitia magazeti yake pendwa. hebu mwenye data zake atiririke jamani
 
Back
Top Bottom