Shida ya maji jiji la Tanga

lolypop

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
2,430
1,681
Yapata siku ya tatu leo bomba hazitoi maji. Tunaomba mamlaka husika watatue hili tatizo kwani dada zetu na akina mama wanapata tabu yakwenda mbali kutafuta maji.

Tukiachana na hilo wenye watoto wadogo na wanao wauguza wagonjwa majumbani ndo kabisa hawawezi ishi bila maji.
Bili za maji tunalipa kwa nini mnatutesa kwa kutukatia maji siku 3 bila huruma.

Nyie idara ya maji Tanga yafungueni hayo maji hata kwa lisaa li moja tu basi maana haya ni mateso.
 
Maeneo yapi? Au jiji lote? Nadhani kutakuwa na tatizo ambalo watakuwa wameshalitangaza ila ww hujasikia. Mamlaka ya maji tanga wako very smart na ndio mamlaka inayoongoza tz kwa Huduma bora
Nipo Tanga city -chungurira, Tangazo leo walisema maji yatatota ili watu wachote , alafu yatakatika tena na baada ya siku 3 nyingine yatatoka. Ajabu mpaka muda huu hakuna kimya
 
Duh poleni kwani ni maenei yote???? Mbona nilipo jana yametoka
Nilipo mimi maji yalikatika Tangu alhamis asubuhi mpaka leo muda huu maji hayajatoka. Nimeenda kutafuta maji mbali tena yakisima
 
Nilipo mimi maji yalikatika Tangu alhamis asubuhi mpaka leo muda huu maji hayajatoka. Nimeenda kutafuta maji mbali tena yakisima
Jamani ijumaa nilikinga maji tena nikasemanikinge ya dharura maana hayaeleweki na nikakinga vyombo vyote sikupatiliza habar ya maji jana nina jirani yangu nimemsikia akikinga maji bombani kwake kata moja nipo na wewe sema niko huku mwisho wa lami
 
Jamani ijumaa nilikinga maji tena nikasemanikinge ya dharura maana hayaeleweki na nikakinga vyombo vyote sikupatiliza habar ya maji jana nina jirani yangu nimemsikia akikinga maji bombani kwake kata moja nipo na wewe sema niko huku mwisho wa lami
Na mpaka muda huu maji hayajatoka bado nawaona wamama na mabinti wakipita na ndoo kwenda kutafuta maji. Mamlaka husika wasikie hiki kilio watusaidie maji ni muhimu sana
 
20180108_070123.jpg



This morning
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom