Shida humfanya mtu kuwa tapeli!

Si hizi biashara ndugu yangu za kuagiza mzigo mikoani kisha wewe ndio uje uuze
Msela wangu tulikuwa nae Geita...aliachishwa kazi kisa ulevi uliopindukia, mwisho wa siku akarudi Mwanza, siku ya siku akanipigia simu yuko Katavi , kumuuliza akasema anajishughulisha na biashara ya nafaka...huku na huku akasema nitumie kiasi nitume mzigo....nikajimix...mzigo sikuwahi kuuona...siku akanipigia kwamba yuko Mwanza..nikaenda kumcheki nikiwa na minajili ya kuchukua hata simu yake ku recover loss walau...nikamkuta amechoka kinoma ...hata kumdai nikaona noma akaishia kuomba jero la nauli...
 
Ungemwelewa usingekurupuka; nilijua umekalia kwenye cariha kumbe nawe umedandia motokaa kwa mbele!???
Sio sahihi kulazikisha watu wafanye atakacho yeye Kama Raisi haimpi mamlaka kulazimisha watu wafanye kaxi sehemu flani au kuwafutia kibali Cha udaktari not fair KWA kweli
 
Wengi yamewapata.

Kuna rafiki yangu kazini alikopa hela benki kwa kumuamini shangazi yake amtumie mazao awe anauza, kilichotokea ilibidi rafiki yangu aende huko kwa shangazi yake alichokuta ni kichefchef, shangazi aligeuka shangingi hicho kijiji alichoishi alikuwa ndio boss lady kwenye mabaa, pesa za mkopo anazitumia kugawa ofa baa na kichwani ana wigi la laki 3 nyumbani kaweka tv ya milioni.

Rafiki yangu nusu afe ganzi, hakuwa na cha kumfanya ila hadi leo hawana mahusiano mazuri
Dah
 
Kuna wenye shida na siyo matapeli..huyo nduguyo ni tapeli ni vile tu hakupata nafasi ya Kufanya utapeli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom