Na mimi polisi akinichokoza nampiga maana adhabu zake ni kuhojiwa tu na kurudi kuja kulala homeJeshi la Polisi mkoani Shinyanga limemwachia huru mgombea Ubunge wa jimbo la Maswa Magharibi kupitia CHADEMA, John Shibuda baada ya upepelezi wa wali kukosa ushahidi wa kumhusisha moja kwa moja na vurugu zilizotokea Maswa mara baada ya mkutano wa kampeni za kisiasa, kampeni zilizosababisha kifo cha Steven Kwilasa ambaye alikuwa dereva wa mgombea wa CCM, kwa jimbo hilo.
Polisi pia wamethibitisha kuwa lilimshikilia mgombea wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Simon Kisena, kwa tuhuma za kumshambulia Mkuu wa Polisi Maswa kwa muda na kumwachia huru mara baada ya mahojiano.
Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai, Robert Manumba amesema watu kumi na mmoja walioswekwa rumande kutokana na vurugu hizo wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yanayowakabili
SORCE: Jeshi la polisi lawaachia huru Shibuda na Kisena -