Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Wadau kuna issue imeibuka hapa, dada mmoja kaniomba ushauri juu ya mambo yafuatayo;
1. Je iwapo mahakama ikatoa kibali cha kutolewa talaka, mtalakiwa (mke) ana haki ya kugawana mali ambayo mtalaka (mume) aliichuma kabla ya ndoa yao kufungwa?
2. Kama mtalakiwa alikuwa ni mama wa nyumbani (hafanyi kazi yoyote inayomwingizia kipato), je ana haki ya kugawana nusu kwa nusu mali yote ambayo ilipatikana wakati wakiwa wanandoa (wanaishi pamoja)?
3. Je mtalakiwa ana haki ya kugawana mali ambazo zimechumwa na mtalaka katika kipindi ambacho tayari mtalakiwa alikuwa haishi na mtalaka lakini kabla ya ndoa yao kuvunjwa rasmi mahakamani? (i.e. ni miaka miwili imepita toka mke aondoke kwa mume, je mali iliyochumwa katika kipindi ambacho mume alikuwa peke yake lakini kabla ya kutolewa talaka)
Naomba mwongozo wa kisheria wadau ili niweze kumsaidia huyu dada.
1. Je iwapo mahakama ikatoa kibali cha kutolewa talaka, mtalakiwa (mke) ana haki ya kugawana mali ambayo mtalaka (mume) aliichuma kabla ya ndoa yao kufungwa?
2. Kama mtalakiwa alikuwa ni mama wa nyumbani (hafanyi kazi yoyote inayomwingizia kipato), je ana haki ya kugawana nusu kwa nusu mali yote ambayo ilipatikana wakati wakiwa wanandoa (wanaishi pamoja)?
3. Je mtalakiwa ana haki ya kugawana mali ambazo zimechumwa na mtalaka katika kipindi ambacho tayari mtalakiwa alikuwa haishi na mtalaka lakini kabla ya ndoa yao kuvunjwa rasmi mahakamani? (i.e. ni miaka miwili imepita toka mke aondoke kwa mume, je mali iliyochumwa katika kipindi ambacho mume alikuwa peke yake lakini kabla ya kutolewa talaka)
Naomba mwongozo wa kisheria wadau ili niweze kumsaidia huyu dada.