MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah
1. ......Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 ni mbovu kwa kuwa inambana na kumfanya ashindwe kuwafikisha watuhumiwa wa rushwa kubwa mahakamani.
2. sheria hiyo inamruhusu kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wadogo wa rushwa na wale wakubwa inamtaka apeleke kwanza jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), jambo ambalo linafanya aonekane hafanyi kazi yake ipasavyo.
3. Alisema anajua matarajio ya wananchi ni makubwa kwa Takukuru, lakini akasema sheria hiyo imewafunga mikono kwa kuwa hawawezi kuchukua uamuzi dhidi ya kesi kubwa za ufisadi bila ushauri wa DPP.
4. "Sheria yetu imetufunga mikono kwa kuwa kumpeleka mtu mahakamani siyo uamuzi wangu, bali wa DPP." (a) Kifungu cha 37 hakimruhusu kutaja majina ya watuhumiwa wa rushwa; (b) Kifungu cha 57 inamzuia kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wakubwa wa rushwa, mpaka awafikishe kwa DPP. (c) Kifungu hicho cha 57 (1) kinasema kuwa shtaka lolote la kosa lililoelezwa kwenye Sheria ya Takukuru lazima lifunguliwe kwa ruhusa ya maandishi kutoka kwa DPP. (d) Kifungu cha 57 (2) kinamtaka DPP ndani ya siku 60 kutoa au kukataa ruhusa ya kushtakiwa.
5. wananchi wasubiri mabadiliko ya kiutendaji kama sheria itabadilika na kumruhusu kufanya hivyo.
6. "Tusaidieni sheria hii ibadilishwe ili iweze kuturuhusu kufanikisha kupambana na rushwa nchini,"
7. Dk Hoseah alisema ofisi yake inazo taarifa kuna mabilioni ya fedha yamefichwa Uswisi na kwamba taasisi yake inayafuatilia.
Source: Mwananchi:Thursday, 16 August 2012
1. ......Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 ni mbovu kwa kuwa inambana na kumfanya ashindwe kuwafikisha watuhumiwa wa rushwa kubwa mahakamani.
2. sheria hiyo inamruhusu kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wadogo wa rushwa na wale wakubwa inamtaka apeleke kwanza jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), jambo ambalo linafanya aonekane hafanyi kazi yake ipasavyo.
3. Alisema anajua matarajio ya wananchi ni makubwa kwa Takukuru, lakini akasema sheria hiyo imewafunga mikono kwa kuwa hawawezi kuchukua uamuzi dhidi ya kesi kubwa za ufisadi bila ushauri wa DPP.
4. "Sheria yetu imetufunga mikono kwa kuwa kumpeleka mtu mahakamani siyo uamuzi wangu, bali wa DPP." (a) Kifungu cha 37 hakimruhusu kutaja majina ya watuhumiwa wa rushwa; (b) Kifungu cha 57 inamzuia kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wakubwa wa rushwa, mpaka awafikishe kwa DPP. (c) Kifungu hicho cha 57 (1) kinasema kuwa shtaka lolote la kosa lililoelezwa kwenye Sheria ya Takukuru lazima lifunguliwe kwa ruhusa ya maandishi kutoka kwa DPP. (d) Kifungu cha 57 (2) kinamtaka DPP ndani ya siku 60 kutoa au kukataa ruhusa ya kushtakiwa.
5. wananchi wasubiri mabadiliko ya kiutendaji kama sheria itabadilika na kumruhusu kufanya hivyo.
6. "Tusaidieni sheria hii ibadilishwe ili iweze kuturuhusu kufanikisha kupambana na rushwa nchini,"
7. Dk Hoseah alisema ofisi yake inazo taarifa kuna mabilioni ya fedha yamefichwa Uswisi na kwamba taasisi yake inayafuatilia.
Source: Mwananchi:Thursday, 16 August 2012