Sheria Zetu ni nguzo ya ufisadi na ulinzi kwa wakubwa

tenende

JF-Expert Member
Jan 10, 2012
6,511
500
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah

1. ......Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 ni mbovu kwa kuwa inambana na kumfanya ashindwe kuwafikisha watuhumiwa wa rushwa kubwa mahakamani.

2. sheria hiyo inamruhusu kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wadogo wa rushwa na wale wakubwa inamtaka apeleke kwanza jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), jambo ambalo linafanya aonekane hafanyi kazi yake ipasavyo.

3. Alisema anajua matarajio ya wananchi ni makubwa kwa Takukuru, lakini akasema sheria hiyo imewafunga mikono kwa kuwa hawawezi kuchukua uamuzi dhidi ya kesi kubwa za ufisadi bila ushauri wa DPP.

4. "Sheria yetu imetufunga mikono kwa kuwa kumpeleka mtu mahakamani siyo uamuzi wangu, bali wa DPP." (a) Kifungu cha 37 hakimruhusu kutaja majina ya watuhumiwa wa rushwa; (b) Kifungu cha 57 inamzuia kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wakubwa wa rushwa, mpaka awafikishe kwa DPP. (c) Kifungu hicho cha 57 (1) kinasema kuwa shtaka lolote la kosa lililoelezwa kwenye Sheria ya Takukuru lazima lifunguliwe kwa ruhusa ya maandishi kutoka kwa DPP. (d) Kifungu cha 57 (2) kinamtaka DPP ndani ya siku 60 kutoa au kukataa ruhusa ya kushtakiwa.

5. wananchi wasubiri mabadiliko ya kiutendaji kama sheria itabadilika na kumruhusu kufanya hivyo.

6. "Tusaidieni sheria hii ibadilishwe ili iweze kuturuhusu kufanikisha kupambana na rushwa nchini,"

7. Dk Hoseah alisema ofisi yake inazo taarifa kuna mabilioni ya fedha yamefichwa Uswisi na kwamba taasisi yake inayafuatilia.

Source: Mwananchi:Thursday, 16 August 2012
 
Sheria irekebishwe haraka, wananchi wanaumia kwa wizi wa fedha za umma.
 
ORGANISED CRIME:......... The involvement in organized crime is the justification of corruption as the normal business. That is the participation of the government officials in corruption and treating it as a normal business." At the surface level they campaign against it but in actual sense they organize it and create mechanism to protect themselves against the wrath of the law. ................ Source: GS for A - Level.
 
Hizi sheria za 2007 zilipitishwa makusudi na serikali ya kifisadi ili kujilinda wenyewe na maswahiba wao. Zitahitaji kubadilishwa haraka mara tutakapokuwa na bunge linalowakilisha maslahi ya watanzania.
 
Kama haya asemayo Hosea ni kweli - Anachotuambia ni kwamba wapowapo tu lakini tusitegemee chochote.

Swali ni je, haya kayajua lini na je, kwa nini asiachie ngazi kuliko kuendelea kuigiza kufuatailia mafisadi wakati anajua hakuna kitu?
 
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah

1. ......Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007 ni mbovu kwa kuwa inambana na kumfanya ashindwe kuwafikisha watuhumiwa wa rushwa kubwa mahakamani.

2. sheria hiyo inamruhusu kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wadogo wa rushwa na wale wakubwa inamtaka apeleke kwanza jalada kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), jambo ambalo linafanya aonekane hafanyi kazi yake ipasavyo.

3. Alisema anajua matarajio ya wananchi ni makubwa kwa Takukuru, lakini akasema sheria hiyo imewafunga mikono kwa kuwa hawawezi kuchukua uamuzi dhidi ya kesi kubwa za ufisadi bila ushauri wa DPP.

4. “Sheria yetu imetufunga mikono kwa kuwa kumpeleka mtu mahakamani siyo uamuzi wangu, bali wa DPP.” (a) Kifungu cha 37 hakimruhusu kutaja majina ya watuhumiwa wa rushwa; (b) Kifungu cha 57 inamzuia kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wakubwa wa rushwa, mpaka awafikishe kwa DPP. (c) Kifungu hicho cha 57 (1) kinasema kuwa shtaka lolote la kosa lililoelezwa kwenye Sheria ya Takukuru lazima lifunguliwe kwa ruhusa ya maandishi kutoka kwa DPP. (d) Kifungu cha 57 (2) kinamtaka DPP ndani ya siku 60 kutoa au kukataa ruhusa ya kushtakiwa.

5. wananchi wasubiri mabadiliko ya kiutendaji kama sheria itabadilika na kumruhusu kufanya hivyo.

6. “Tusaidieni sheria hii ibadilishwe ili iweze kuturuhusu kufanikisha kupambana na rushwa nchini,”

7. Dk Hoseah alisema ofisi yake inazo taarifa kuna mabilioni ya fedha yamefichwa Uswisi na kwamba taasisi yake inayafuatilia.

Source: Mwananchi:Thursday, 16 August 2012
Rushwa ni Taasisi!! Kweli tuna kazi kumbe Hosea yuko chini wa DPP!! Ndiyo maanaaaa!!!
 
wahuni watupu,serikali hii ni ya viongozi dhidi ya wananchi kwa kutumia kigezo cha sheria.Tuliona Africa kusini tukapiga makelele kwelkweli,leo kwetu walewale tunaona sawa tu mradi hatujagombana na ukiuliza unahatarisha amani kama ilivyokuwa kule.Inabidi wananchi waunde serikali yao itakayo wajali na viongozi wa leo wabaki na yao watafunane,hapo ndo kwenye suluhisho
 
Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne
Watu
Ardhi
Siasa safi
Uongozi

Adui yetu mkuu ni CCM. Ameleta ujinga, maradhi na dhulma (Ufisadi). Darasa la saba hajui kusoma? Duhhh
 
Hizi sheria za 2007 zilipitishwa makusudi na serikali ya kifisadi ili kujilinda wenyewe na maswahiba wao. Zitahitaji kubadilishwa haraka mara tutakapokuwa na bunge linalowakilisha maslahi ya watanzania.

Alikaa kimya muda wote amengundua ipo siku watu watamdai yeye kama Hosea kwamba ndiye aliyeshindwa kazi.
 
Back
Top Bottom