Ravalomanana
JF-Expert Member
- Sep 8, 2018
- 1,384
- 1,310
Ndugu zangu watanzania katika siku za karibuni kumekua na utaratibu kwa hospitali za serikali kuwalazimisha wagonjwa kupima virusi vya ukimwi kama masharti ya kupata matibabu na ukikataa hupati matibabu,lengo langu ni kutaka kujua je ni kweli wizara ya afya imetoa agizo hilo au ni taratibu tu za hospitali husika kwa maana utaratibu huu unapingana na sheria ya ukimwi ya mwaka 2008