Sheria ya Uchaguzi ni mbovu! Kuendelea kuitumia sio Ujinga? Kuwabebesha masikini gharama za Uchaguzi sio Dhambi?

Mkuu ChaterMaster, kwanza hakuna mtu ambaye hana shida ya pesa, tena please usiite shida ya pesa, bali ita mahitaji, hakuna binadamu yoyote ambaye hana mahitaji, wala mimi sio tajiri kusema sina shida ya pesa, mimi ni masikini wa kutupwa ila ni masikini jeuri, pango tuu ninalolipa NHC ni Zaidi ya mshahara wa DC, hivyo niutafute u DC ili nipate nini?.

Amini usiamini, kazi kubwa na muhimu kuliko zote ni kazi ya urais, kuna Watanzania kibao, wanauwezo wa kuwa rais mzuri kwa Tanzania mara kumi ya Magufuli, lakini huo urais hata bure hawautaki!. Kuna watu kibao wako kama mimi, japo ni masikini kuliko DC, lakini huo uDC hata bure hawaufikirii, they are just happy doing what they do, they live happy with the little they make kwa kujituma wenyewe na sio kuwa proud na kazi za kutumwa!.

Paskali
Ooky thx kwa ufafanuz na historia yko binafsi... btw ni muda muafaka wa kuunganisha nguvu zako ktk kikundi au union/organization fulaani ambayo itamuvu forwad agenda unazoziamini..
Pia uhakikishe unakuwa na msimamo ktk unayoyaamini hii ni pamoja na kuacha kuwa na double standard ya mambo.
Sijui unajisafishaje ktk hili linalolalamikiwa na wengi hapa kuwa ni ndumilakuwili. Hii si SIFA nzuri hasa kwa wanaojiita wazalendo/wapambanaji. Utakuwa huna tofauti na Zitto ambaye ni mjenga hoja mzur ila kiukwel wengi wanambeza na kumpuuza sababu ya undumilakuwili wake.

Please define your Way of Life, hii itakupa heshima badala ya dharau. Ukushindwa bora uwe kimya maana wengi watakuupuuza pale usemapo.

Lastly, natamani uteuliwe kisha nithibitishe kuwa wew huna njaa za kijinga kama walizonazo wengii
 
Ralph Nader je?

Marekani huwa hadi kuna wagombea wa chama cha Kisoshalist ambao hugombea urais.

Hadi write-in candidates huwa wapo na wapo kwenye ngazi zote hadi urais.

Uzuri wa Marekani madhali mtu umetimiza vigezo vya kikatiba kugombea ni rukhsa.

Halafu sijui watu hudhani kuwa Marekani wagombea urais huwa ni wawili tu wakati ukweli wa mambo huwa ni wengi.
Anaongelea habari ya kushinda uchaguzi.

Mtu anayepima effectiveness ya private candidates kwa kushinda uchaguzi hajaelewa dhana nzima ya uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa.

Halafu hapo anakwambia amefanya research Marekani.

Si ajabu hajawahi hata kumsikia Tocqueville, seuze kumsoma.

Definitely hajamsoma na kumuelewa, angemsoma na kumuelewa asingeandika ujinga huo.
 
Tunafahamu kuwa uchaguzi mdogo wa udiwani na ubunge unahitaji maandalizi ya lazima kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Je uchaguzi wa mbunge kwenye jimbo moja unaigharimu tume, vyama na wanachama kiasi gani jumla?

Tunafahamu kuwa kuna watu wananufaika na chaguzi hizi moja kwa moja, wangependa chaguzi hizi zifanyike kila mwezi.

Lazima sasa taifa liangalie njia bora za kuondokana na gharama za chaguzi ndogo za kila mara kwa kuweka masharti magumu sana ya mbunge kuweza kujiuzulu au kufukuzwa ubunge au udiwani. Na hata kama akifa kusiwe na uchaguzi mwingine.

Hii inakera wengi
 
Hakika wakati umefika Kwa watanzania kujua gharama za Chaguzi za marudio Kwa kila JIMBO ili tujue hawa Wabunge wanaoamua KUJIUZULU na kuliingiza Taifa kuitisha uchaguzi wanatutia HASARA kiasi gani.
 
Ungeomba angalau mwenye kujua partially gharama ungepata majibu kwa haraka. Ila jinsi ulivyoliweka swali lako, kila mtu atasita kujibu maana haujali-direct towards wana jamvi bali kwa watu wa tume ya uchaguzi.
 
Heshima kwako Pascal Mayalla hoja zako nzuri sana... lakini zina ukakasi... nitasema kwa nini? Umetumia neno "ujinga" mara nyingi.
Naomba nikwambie watu walioandika sheria katiba miaka 33 iliyopita nikimaanisha kutoka 1984; hawakuwa na information kama ulizo nazo wewe leo.
Indeed hata hoja zako hizo zimetokea kwa sababu sheria zimekuwa practically tested...

Hivyo ndugu hata sisi twaweza tunga sheria leo na baada ya 10years au 20 years tukaonekana kama tulikuwa tumelewa vile..

Hivyo tuamini tu kwamba taifa linaishi na liko dynamics... issue ni kukubali kwamba some of laws are due to be ammended or even repealed... bila matusi ya namna yoyote.

Natumaini umenielewa, hatuna sababu ya kuwalaaumu wa zamani... bali sisi tufanyie kazi sasa kwa reality tunazoziona... etc.
 
Ooky thx kwa ufafanuz na historia yko binafsi... btw ni
  1. muda muafaka wa kuunganisha nguvu zako ktk kikundi au union/organization fulaani ambayo itamuvu forwad agenda unazoziamini..
  2. Pia uhakikishe unakuwa na msimamo ktk unayoyaamini hii ni pamoja na kuacha kuwa na double standard ya mambo.
  3. Sijui unajisafishaje ktk hili linalolalamikiwa na wengi hapa kuwa ni ndumilakuwili. Hii si SIFA nzuri hasa kwa wanaojiita wazalendo/wapambanaji. Utakuwa huna tofauti na Zitto ambaye ni mjenga hoja mzur ila kiukwel wengi wanambeza na kumpuuza sababu ya undumilakuwili wake.
  4. Please define your Way of Life, hii itakupa heshima badala ya dharau. Ukushindwa bora uwe kimya maana wengi watakuupuuza pale usemapo.
  5. Lastly, natamani uteuliwe kisha nithibitishe kuwa wew huna njaa za kijinga kama walizonazo wengii
Mkuu Chater Master,
  1. Limeishafanyika, its just a matter of time tuu kabla ya roll out plan.
  2. Mimi ni dynamic na sio static, bali pia ni realist, kuukubali ukweli halisi ulivyo hata kama kuwa mkweli utaonekana ni kuwa na double standards, I stick to the truth na sio kuangalia watu wanataka nini, au wanasema nini and I'm happy kusimama kwenye kweli daima!.
  3. We are living in a jungle, the law of the jungle is to struggle for existence and survival is for the fittest, ili uweze ku fiti, ni lazima uwe na uwezo wa kubadilika kutokana na time and place, hata kama utaonekana ni ndumilakuwili, na mfano mzuri ni Magufuli, nimeandika humu ndani jinsi ambavyo namkubali Magufuli kwa utendaji wake kwenye vita dhidi ya rushwa na ufisadi, na kwenye mazuri nampongeza, lakini wakati wakati huo huo, sikubaliani na Magufuli katika udikiteta wake kwenye baadhi ya maeneo, na hapo hapo kukubali kuwa udikiteta ukitumika vizuri ndio the best solution kwa nchi yetu hapa tulipofika na hapa kwenye nyuzi hizi mbili nimeeleza Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba! na hapa ninasema tumuombee, If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!, sijali kuhusu kupuuzwa as long as nimesimama kwenye kweli, hata kama at the end of the day, nitabaki peke yangu niliyesimama kwenye kweli, then bei it.
  4. Msimamo wangu ni ule ule mmoja tuu, kweli, kweli, kweli, nothing but the truth, watu wenye pande zao, wananata kuusikia ukweli utaowafurahisha, sasa ili usiwaudhi, unaweza kuamua bora kunyamaza, mimi msimamo wangu siku zote ni ukweli usemwe, no matter what, na ni kweli wengi watapuuza, ila mwisho wa siku, ni ukweli tuu ndio utakaosimama mpaka mwisho, na mi mi ndio nasimama nao!.
  5. Utasubiri sana!.
Paskali
 
Nimeona katuni ya masoud kipanya ya siku ya leo, ambayo inaelezea ishu ya mbunge kujivua ubunge.. Kuwa kuna kitu nyuma ya pazia.
Wabunge wengi tunafahamu wanchaguliwa na wananchi kupitia vyama vyao, then wakishapata hiyo nafasi wanakuwa wamesimama badala ya wananchi bungeni kutetea na kuwaombea wananchi wao haki yao ya kupata maendeleo pia uwakilishi katika kufanya maamuzi?
Iweje mbunge wa upinzani ama chama tawala ujiuzulu na kuiingiza serikali katika gharama kubwa?
Huu ni ukosefu wa maadili, uzalendo na elimu ya kujitambua. Na hii kitu inakuwa itafsiriwe kama ni ujinga.. Hivi wakati unaomba kura na kutaka hiyo nafasi uliwaza na kufikiria kuwa upo pale kwa ajili ya chama chako ama mhemuko wa kisiasa? Kwa maana hiyo hukujitambua, kwanini ujivue ubunge na kukihama chama kwa kufuata upepo na wakati upo kwa ajili ya watu walokuchagua.
Pia si vyema jimbo kukaa bila mbunge mpaka uchaguzi utakapofanyika..kwa sababu uwakilishi unakosekana. Nashauri wananchi wasichague tena hao watu, kupitia chama chochote.
[HASHTAG]#inauma[/HASHTAG]
 
Demekrasia ina gharama zake lakini pia ina mipaka yake. Haiwezakani wananchi wale wale wawe wanachagua mbunge huyo huyo kila anapohama chama hayo ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi. Wewe ukiachia ubunge au udiwani nenda ukafanye shughuli nyingine kwani ulikuwa na uwezo wa kukitumikia hata chama tawala bungeni ukiwa upinzani. Kwa mfano pale bungeni wapo wabunge wa Chadema wanamuunga mkono Rais Magufuli na tumeona michango yao kwenye kazi za kamati mfano Silinda na Ole Milya, na wamefanya hivyo bila kuhamia CCM. Ifike mahali tusikubali huu ujinga wa kumchagua mtu huyo huyo kila " anapojisikia" kuhama hama vyama huu umalaya wa kisiasa utaligharimu taifa na hawa wanasiasa wa aina hii ni Wahujumu wa Uchumi. Nawasilisha!
 
Mi nimeshachoka na hii nchi inayobana matumizi kibaguzi,kuna wanaobanwa na waliopewa uhuru waswahili wanasema kunya anye kuku akinya bata kaharisha
 
Kumbe ukitembelea V8 ujui kama barabara ni mbovu hivi fedha za marudio ya uchunguzi zisingetosha hata kujenga kituo cha afya au bara bara ya Buguruni kwa mnyamani
 
Hawa wabunge walikuwa wabunge halali wa majimbo halali,hawa wabunge hawakuwa na pingamizi lolote kuhusu ushindi wao,walishinda kuhalali walitangazwa na hatimaye kuapishwa na wakawa wabunge,

Dr Mollel na Mtulya,kati ya hawa hakuna Mbunge yeyote aliyefariki na kufufuta akakuta CUF na CHADEMA wakawapata wagombea then baada ya kufufuka wakaamua kwenda ccm,

Hawa wabunge kwa hiari yao waliamua kujiuzulu wakiwa na akili timamu(sina uhakika) kwamba hawataki tena kuwaunganisha wananchi waliowachagua na serikali.....

Waliamua kuondoka kwa hiari yao,

Halafu Leo hii wanaletwa watu walewale waliojiuzulu kwa majimbo yaleyale hii n dharau kwa wananchi wa majimbo husika(Siha na Kinindoni)
 
Kiukweli kitendo kilichofanywa na CCM kuwasimamisha wabunge wale wale waliotufanyia ujinga wa kujiuzulu, na kutuingiza ghara za uchaguzi wa mazudio kwa sababu za kijinga, ni ujinga uliopitiliza!.

Hii inaamisha CCM inawaona wana Kinondoni na wana Siha kuwa ni wajinga!, yaani mtu aliyeaminiwa na wananchi, na kuchaguliwa kuwa mwakilishi wao, halafu anajiuzulu kwa sababu za kijinga, kisha kugombea tena kupitia cha kingine, akitaraji atachaguliwa tena!, ikitokea ni kweli akachaguliwa, wananchi wa maeneo hayo, watakuwa ni wajinga wa kutupwa, kwa kufanywa wajinga na kuukubali ujinga huu!. Kwa sasa siwezi kuwasemea wananchi wa Siha, ila kwa vile mimi ni mkazi wa Kinondoni, na ni mpiga kura wa Kinondoni, kamwe siwezi kuukubali ujinga huu, hivyo nitawahamasisha wana Kinondoni, wanaojielewa ma kujitambua, wasiukubali ujinga huu wa CCM, kutaka kutufanya mazuzu!, hivyo kutoa wito kwa wana Kinondoni wote, wakiwemo wana CCM, kuutumia uchaguzi huu wa marudio, kutuma ujumbe Mzito kwa Chama cha Mapinduzi, kuwa Wana Kinondoni sio wajinga, sio mazuzu, na hawakubali kuletewa ujinga!, hivyo watamchagua mhombea yoyote, kutoka chama kingine chochote but not CCM!.

Paskali
 
Tukiomba chama cha Mapinduzi CCM hizi Chaguzi inazozilazimisha kwa kuwarubuni madiwani wa upinzani zinatutia umasikini sisi Masikini wa nchi hii.
Kuna wakati walipa kodi inafaa mjionee huruma wenyewe sasa! Chagua CCM hawanunuliwi, vinginevyo mtafanya uchaguzi kila mwaka mkijitia ununda...
 
Back
Top Bottom