Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Mkuu Daata, kulingana na Sheria tajwa,ndoa ni muungano wa mwanaume na mwanamke wenye lengo la kuwafanya waishi pamoja katika maisha yao yote na katika kujitenga na wengine wote waliobaki. Ndoa ina taratibu zake Mkuu.Hakuna aina au namna yoyote ya ndoa inayotokana na kuishi na mwanamke au mwanaume kwa muda fulani. Dhanio la ndoa lililopo chini ya kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa huwahusu wau waliohitilafiana na ambao waliishi kwa miaka miwili au zaidi.

Asante Petro E. Mselewa kwa ufafanuzi. Msingi wa swali langu ni kwamba mara nyungi nimewahi kusikia kuwa ukikaa/ishi na mwanamke kwa miezi sita mfululizo huhesabiwa kama ndoa na huyo mwanamke ana haki ya umiliki wa mali zote mlizochuma pamoja
Je kuna ukweli wowote katika madai haya kulingana na sheria hiyo?
 
Last edited by a moderator:
Asante Petro E. Mselewa kwa ufafanuzi
Msingi wa swali langu ni kwamba mara nyungi nimewahi kusikia kuwa ukikaa/ishi na mwanamke kwa miezi sita mfululizo huhesabiwa kama ndoa na huyo mwanamke ana haki ya umiliki wa mali zote mlizochuma pamoja
Je kuna ukweli wowote katika madai haya kulingana na sheria hiyo?

Hakuna ukweli wowote hapo Mkuu Daata. Kifungu cha 160 cha Sheria husika kinatoa Dhanio la Ndoa.Hili huwepo pale ambapo mwanamke na mwanaume huishi kama mke na mume kwa miaka miwili au zaidi.Wakati wa kuishi kwao na kupata heshima ya jamii kama mke na mume wanaweza kuchuma mali mbalimbali.Sasa katika kuhitilafiana kwao,mwanamke hataondoka mikono mitupu. Hiyo ni dhana tu ya Dhanio la Ndoa na hutumika hivyo na si vinginevyo
 
Sheria inazungumziaje uhusiano uliopo kati ya ndoa na talaka?
Talaka ni nini
Aina za talaka
Ipi talaka halali
 
Wana-JF,karibuni hapa kwa maswali mbalimbali yahusuyo Sheria ya Ndoa,1971.Wale wote waliopo kwenye ndoa na wanaotarajia kuwa kwenye ndoa wanakaribishwa hapa kuuliza na kujibiwa. Nitashirikiana na Mawakili Wasomi wenzangu waliopo humu kuwajibu maswali yenu.

Mods, mnaweza kuufanya uzi huu kuwa 'sticky'? Asanteni na karibuni!

ahsante mkuu sasa hiyo sheria ya ndoa ya 1971 haina CAP? hebu naomba full citation mkuu
 
hivi mme akiwa na watoto wa nje,halafu mimi na yeye tumeoana tukiwa hatuna kitu,then tukafight tukawa matajiri,siku akifa je wanae wa nje wana haki ya kurithi na wanangu wa ndani ya ndoa?

Mkuu Victoire, kwanza yategemea namna ya ndoa iliyofungwa baina yenu.Kama ni ya kiislam,kwa mfano,watoto wa nje ya ndoa hawawezi kurithi. Kama ni ndoa ya kimila,yategemea mila za kabila lenu husika. Kama ni ndoa ya Bomani, yategemea na makubaliano yenu katika ndoa yenu.Hii ni kwakuwa,kifungu cha 58 cha Sheria ya Ndoa kinaruhusu uwepo wa Makubaliano juu ya umiliki wa mali za ndoa.Umiliki ndio unaelekeza urithi hapo baadaye.

Nataka nieleweke kuwa, kama mali ni binafsi kama inavyoruhusiwa chini ya vifungu vya 56 na 57,urithi waweza kufuata sheria,mila au Wosia.Lakini,kama ni mali ya pamoja watoto wa nje ya ndoa (kwa ndoa za bomani na za kikristo) hurithi kutokana na matakwa ya wanandoa tu na si vinginevyo.
 
Sheria inazungumziaje uhusiano uliopo kati ya ndoa na talaka?
Talaka ni nini
Aina za talaka
Ipi talaka halali


Kwanza,talaka ni mwisho wa ndoa.Pili,talaka hutolewa na Mahakama tu na si vinginevyo.Tatu, talaka ina taratibu zake.Kwa mfano,ni lazima kwa mwombaji wa talaka apitie katika Baraza la Usuluhishi la Ndoa kabla ya kwenda Mahakamani kudai talaka. Pia,Baraza husika lazima litoe kibali cha kushindwa kuwasuluhisha wanandoa hao ambao mmoja wao anataka kutalikiwa. Nne, talaka hutolewa tu pale ambapo ndoa hiyo itaonekana kuwa haiwezi tena kubaki a kurekebishika.

Kimsingi,Mahakama hulenga hasa katika kuilinda ndoa.Ndiyo maana,mwombaji wa talaka lazima athibitishe uwepo wa sababu za talaka kwa mfano mateso,kutelekezwa na uasherati wa mwenza wake.Ieleweke kuwa talaka zitolewazo kiislam ni hatua tu.Hii ni kwakuwa ni Sheria ya Ndoa tu ndiyo inayotumika katika suala hilo.
 
Mkuu nina maswali mawili,moja je kama mume na mke wanaishi pamoja halafu mwanamke akawana ishu zake binafsi for years,mume akavumlia mwishowe mume aamua waachane,ssa mke alipoambiwa hakuini maana alidhani mwaaume lofa,so mwanamke akafanya attempt ya kujiua,kwa kunywa sumu,bahati nzuri mume akamuokoa kwa kumuwahisha hosp,baada ya muda kidogo mke alipopata nafuu,mume na mke wakaamua kutengana na wakaandikishana mbele ya serikali ya mtaa kuwa wanatengana wakati wakisubiria taratibu nyingine za kuachana kisheria ziendelee,na wakati huo mwanaume anaamua kuandikisha mali zote anamwachia mke pamoja na magari,nyumba na asset zote,na mke anasaini kukubaliana na hii hali tena mbele ya ndugu mmoja kila upande kama shahidi.je document hii inaweza kusaidia mahakamani kupata talaka. (n.b ktk makabidhiano hakuna sababu iliyoainisha chanzo cha kutengana)
 
Mkuu andishile, simulizi yako yote imejaa ubatili mtupu katika jicho la kisheria na haitasaidia kupatikana kwa talaka. Watu wengi katika jamii huamini njia za kimtaani na kuamini kumaliza kila kitu.

Lakini, njia pekee sahihi ni Mahakama tu. Hata Amri ya Kutengana huombwa na kutolewa na Mahakama. Kutengana na Talaka ni Amri zitolewazo na Mahakama tu Mkuu. Kuna matatizo mengi hapa kwenye Sheria ya Ndoa. Ndiyo maana tunadokezana angalau njia sahihi.

Mkuu Invisible,tafadhali ufanye uzi huu kuwa 'sticky' ili wengi na kwa siku nyingi wafaidike nao.

Asante
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, nauliza je kuna sheria zetu zina ile kitu wazungu wanaita "pre-nuptials" au utaratibu kama huo ambapo wanandoa wakiachana kila mtu anaendelea kumiliki mali zake binafsi?
 
Mke na mume waliooana miaka nane iliyopita,mume akidai wafunge ndoa ya dharura kanisani anatakiwa kwenda masomoni nje ya nchi baada ya kugundua manmke mjamzito ,wakafunga ndoa,cheti hawakupewa kanisani,hadi wiki ikapita mwanamke akafuatilia cheti akapewa lakini kilijazwa mbele yake akishihudia tena kikiwa tayari kimenyofolewa ina maana hakuna nakala imebaki kanisani,je hapo kuna ndoa kweli? Halafu baada ya miezi kadhaa mwanamke anagundua mwanaume ni majanga na hakuna cha kwenda kusoma wala nini,mwanamke alipojifungua akaona yu salama kiafya,akaamua bora kutengana na mwanaume.mwanaume akamsusa kwa miaka saba kumtelekeza full!sasa mwanamke anataka rasmi apewe talaka hata kikanisa maana ni almost hakufunga ndoa halali,je afanyeje?ukizingatia mwanaume baada ya kutengana na huyo mwanamke kashaishi na wanawake zaidi ya tisa na kwa bahati mbaya wawili wamefariki na ukimwi!
Hizi kesi zote mbili zinahitaji msaada wako,unapatikana wapi?yani hawa nawambia inawezekana kupatatalaka hawaamini!
 
Kwa mfano nimeoa, ila mke kanikuta na kila kitu nikaishi nae miaka 5, hatuna watoto kwa bahati mbaya tukaachana je mali alizo zikuta tutagawana?
 
mkuu nauliza je kuna sheria zetu zina ile kitu wazungu wanaita "pre-nuptials" au utaratibu kama huo ambapo wanandoa wakiachana kila mtu anaendelea kumiliki mali zake binafsi?


Mkuu jMali, kiufupi,hata ndani ya ndoa,wanandoa wanaruhusiwa chini ya kifungu cha 56 cha Sheria ya Ndoa,kumiliki mali binafsi. Kwahiyo, hata baada ya kuachana,mgawanyo wa machumo utajikita kwenye mali za pamoja tu na zile binafsi kuelekea sehemu stahiki.
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu.
Mahakama ya mwanzo imetengua ndoa. Nataka kukata rufaa. Ndoa imetenguliwa Iringa. Ninayemkatia rufaa yupo kigoma
1.Rufaa nikate katika mahakama gain?
2.Rufaa nikate pale nilipo Mimi au alipo mkatiwa rufaa au mkoa wowote?
Karibu
 
Mkuu andishile, simulizi yako yote imejaa ubatili mtupu katika jicho la kisheria na haitasaidia kupatikana kwa talaka. Watu wengi katika jamii huamini njia za kimtaani na kuamini kumaliza kila kitu.Lakini,njia pekee sahihi ni Mahakama tu. Hata Amri ya Kutengana huombwa na kutolewa na Mahakama. Kutengana na Talaka ni Amri zitolewazo na Mahakama tu Mkuu. Kuna matatizo mengi hapa kwenye Sheria ya Ndoa.Ndiyo maana tunadokezana angalau njia sahihi.

Mkuu Invisible,tafadhali ufanye uzi huu kuwa 'sticky' ili wengi na kwa siku nyingi wafaidike nao.Asante

sasa kwa kesi kama hii unawasaidiaje?wakienda mahakamani wanaweza kupeana talaka?
 
swali la pili,mke na mume waliooana miaka nane iliyopita,mume akidai wafunge ndoa ya dharura kanisani anatakiwa kwenda masomoni nje ya nchi baada ya kugundua manmke mjamzito ,wakafunga ndoa,cheti hawakupewa kanisani,hadi wiki ikapita mwanamke akafuatilia cheti akapewa lakini kilijazwa mbele yake akishihudia tena kikiwa tayari kimenyofolewa ina maana hakuna nakala imebaki kanisani,je hapo kuna ndoa kweli?halafu baada ya miezi kadhaa mwanamke anagundua mwanaume ni majanga na hakuna cha kwenda kusoma wala nini,mwanamke alipojifungua akaona yu salama kiafya,akaamua bora kutengana na mwanaume.mwanaume akamsusa kwa miaka saba kumtelekeza full!sasa mwanamke anataka rasmi apewe talaka hata kikanisa maana ni almost hakufunga ndoa halali,je afanyeje?ukizingatia mwanaume baada ya kutengana na huyo mwanamke kashaishi na wanawake zaidi ya tisa na kwa bahati mbaya wawili wamefariki na ukimwi!
hizi kesi zote mbili zinahitaji msaada wako,unapatikana wapi?yani hawa nawambia inawezekana kupatatalaka hawaamini!


Mkuu andishile, nilitamani kujibu swali lako hapa.Lakini, kwakuwa unampango wa kunitafuta,fanya hivyo.Nje ya hapa mjiandae na ada ya ushauri. Ni-PM nambari yako Mkuu nikuelekeze nilipo
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom