Babu wa Kambo
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 559
- 808
MAREKEBISHO ya Sheria mpya ya Manunuzi, yamewasilishwa bungeni yakitamka kufyeka posho za watendaji, wanaosimamia mchakato wa zabuni na kuondoa vikao vya bodi kutoka 12 kwa mwaka hadi vinne, ikisisitiza kuziba mianya ya rushwa na kuongeza uwazi.
Aidha, muswada wa marekebisho hayo, unataka kampuni au mshauri wa nje ili apewe zabuni katika shughuli zinazogharimiwa na fedha za umma, ahakikishe asilimia 60 ya wafanyakazi wa kampuni yake ni Watanzania.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, aliyasema hayo jana mjini Dodoma wakati akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016.
Kupungua kwa vikao vya bodi, kumeelezwa na Dk Mpango kuwa kutapunguza gharama zinazotokana na posho ya vikao vya bodi ya zabuni na ada zinazolipwa kwa kamati zinazohusika na mchakato ya zabuni.
Aidha, posho zinazotokana na utekelezaji wa majukumu ya kazi ya kila siku ya washiriki itafutwa. Hata hivyo, imeruhusu kuwapo kwa vikao vya dharura pale Mwenyekiti wa Bodi akiona ni lazima.
Pamoja na kupunguzwa vikao, muda wa zabuni nao umepunguzwa na pia taasisi nunuzi itaruhusiwa kufanya majadiliano ya bei wakati wa mchakato wa zabuni kwa lengo la kupunguza bei ya ununuzi na kuongeza bei ya kuuza mali za serikali.
Dk Mpango alisema pamoja na kuongeza uwajibikaji, sheria hiyo mpya itapunguza vikao vya bodi hadi kuwa kimoja kwa robo mwaka na vikao vya dharura, kufanyika pale ambapo mwenyekiti ataona inabidi.
Pamoja na maelekezo hayo mapya, serikali pia itaanza kununua bidhaa na huduma kwa bei inayoendana na bei ya soko, iwapo wabunge watapitisha marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Pamoja na ununuzi wa bei ya soko, sheria mpya imelenga kuweka sharti la kisheria kutoa upendeleo katika zabuni mbalimbali, hasa kwa makundi maalumu kama vile wanawake, vijana, wazee na watu wenye mahitaji maalumu.
Aidha, muswada wa marekebisho hayo, unataka kampuni au mshauri wa nje ili apewe zabuni katika shughuli zinazogharimiwa na fedha za umma, ahakikishe asilimia 60 ya wafanyakazi wa kampuni yake ni Watanzania.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, aliyasema hayo jana mjini Dodoma wakati akiwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016.
Kupungua kwa vikao vya bodi, kumeelezwa na Dk Mpango kuwa kutapunguza gharama zinazotokana na posho ya vikao vya bodi ya zabuni na ada zinazolipwa kwa kamati zinazohusika na mchakato ya zabuni.
Aidha, posho zinazotokana na utekelezaji wa majukumu ya kazi ya kila siku ya washiriki itafutwa. Hata hivyo, imeruhusu kuwapo kwa vikao vya dharura pale Mwenyekiti wa Bodi akiona ni lazima.
Pamoja na kupunguzwa vikao, muda wa zabuni nao umepunguzwa na pia taasisi nunuzi itaruhusiwa kufanya majadiliano ya bei wakati wa mchakato wa zabuni kwa lengo la kupunguza bei ya ununuzi na kuongeza bei ya kuuza mali za serikali.
Dk Mpango alisema pamoja na kuongeza uwajibikaji, sheria hiyo mpya itapunguza vikao vya bodi hadi kuwa kimoja kwa robo mwaka na vikao vya dharura, kufanyika pale ambapo mwenyekiti ataona inabidi.
Pamoja na maelekezo hayo mapya, serikali pia itaanza kununua bidhaa na huduma kwa bei inayoendana na bei ya soko, iwapo wabunge watapitisha marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Pamoja na ununuzi wa bei ya soko, sheria mpya imelenga kuweka sharti la kisheria kutoa upendeleo katika zabuni mbalimbali, hasa kwa makundi maalumu kama vile wanawake, vijana, wazee na watu wenye mahitaji maalumu.