Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu nimeuona muswada unaompa Waziri wa fedha nguvu ya kufuta kodi mbalimbali atakapoona inafaa. Ikumbukwe hili lilikuwepo miaka ya huko nyuma lakini lilirudishwa kwenye baraza la mawaziri baada ya mawaziri aidha kwa kuchomekewa au kwa makusudi kuitumia bila kuwa na tija kwa taifa;
Baadhi ya Mawaziri wa fedha waliowahi kukumbwa na kadhia ya nguvu waliopewa na sheria hii ni kama ifuatavyo;
Prof. Mbilinyi (enzi za Mkapa) Kilonsi Mpologonyi (alikuwa naibu wa wizara ya fedha enzi za Mkapa)
Daniel Yona na Basil Mramba hawa walikuwa mawaziri wa fedha nyakati tofauti enzi za Mkapa (Yona aliwahi kuwa waziri wa madini pia).Ikumbukwe hawa wazee walienda jela kutokana na nguvu hizi.
Kwa uchache, sheria hii ya kumpa waziri wa fedha mamlaka ya kusamehe kodi inachochea rushwa na ufisadi wa hali ya juu kwani wanufaika wa sheria hii ni wajanja wajanja na mara zote misamaha hii haina tija kwa taifa.
Ninashauri Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni raisi libaki na jukumu hili.
Kama hili litapita litakuwa shimo la kisiasa kwa Mwigulu Nchemba kwani wabaya wake watatatumia sheria hii kumtega na kummaliza kisiasa na haitaishia kwake, CCM watakuwa na mzigo wa kujisafisha nalo.
Baadhi ya Mawaziri wa fedha waliowahi kukumbwa na kadhia ya nguvu waliopewa na sheria hii ni kama ifuatavyo;
Prof. Mbilinyi (enzi za Mkapa) Kilonsi Mpologonyi (alikuwa naibu wa wizara ya fedha enzi za Mkapa)
Daniel Yona na Basil Mramba hawa walikuwa mawaziri wa fedha nyakati tofauti enzi za Mkapa (Yona aliwahi kuwa waziri wa madini pia).Ikumbukwe hawa wazee walienda jela kutokana na nguvu hizi.
Kwa uchache, sheria hii ya kumpa waziri wa fedha mamlaka ya kusamehe kodi inachochea rushwa na ufisadi wa hali ya juu kwani wanufaika wa sheria hii ni wajanja wajanja na mara zote misamaha hii haina tija kwa taifa.
Ninashauri Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni raisi libaki na jukumu hili.
Kama hili litapita litakuwa shimo la kisiasa kwa Mwigulu Nchemba kwani wabaya wake watatatumia sheria hii kumtega na kummaliza kisiasa na haitaishia kwake, CCM watakuwa na mzigo wa kujisafisha nalo.