inspectorbenja
JF-Expert Member
- Oct 14, 2012
- 462
- 394
Mara kwa mara wanufaika wa bodi ya mikopo wamekuwa wakilalamika juu ya kitu kinachoitwa retention value fee kinachotozwa na bodi. Yaani kila mwaka mtu anatozwa 6% ya ya deni ili kutuinza thamani ya shilingi.
Hiki ndio kilio watu wamekuwa wakiomba kipengele hiki kandamizi kiondolewe. Watu wengine wamekiwa wakiomba hata mbele ya viongozi wakuu wa nchi. Mfano wakati wa mei mosi lilizungumzwa, mhe rais alipoenda sua. Kuna mhadhiri alilizungumzia mbele ya rais. Lakini kwa bahati mbaya huwa linapuuzwa wala hakuna kiongozi mkubwa anayeonekana kuguswa nalo.
Bhati mbaya zaidi,mara zote bodi wanapotoa majibu au ufafanuzi,wamekuwa wakibwabwaja bwabwaja tu na kutolea ufafanuzi wa vitu ambavyo hata sisi hatuhitaji,siyo jero wala kilio. Yaani wamekuwa wakileta ngojera tu. Hata majibu ambayo amejibiwa mwalimu Iddy, wamebwabwaja bwabwaja tu, kilio cha mwalimu Iddy ilikuwa ni hii 6% anayotozwa mtu kila mwaka. Sasa wanavyisema mwalimu Iddy kaelewa na atakuwa balozi mwema sijui yeye binafsi wamemuondolea hiyo 6%
Kipengele hiki ni kandamizi, mbona watu wanaoidai serikali kwa miaka nenda rudi na wanambiwa wasubiri wao hawaikwekei serikali 6% kila mwaka kutunza thamani ya shilingi.
Jamani 6% ya kila mwaka inatuua, enyi viongozi wetu na bodi mtuonee huruma jamani. Tamzania ni yetu wote
Hiki ndio kilio watu wamekuwa wakiomba kipengele hiki kandamizi kiondolewe. Watu wengine wamekiwa wakiomba hata mbele ya viongozi wakuu wa nchi. Mfano wakati wa mei mosi lilizungumzwa, mhe rais alipoenda sua. Kuna mhadhiri alilizungumzia mbele ya rais. Lakini kwa bahati mbaya huwa linapuuzwa wala hakuna kiongozi mkubwa anayeonekana kuguswa nalo.
Bhati mbaya zaidi,mara zote bodi wanapotoa majibu au ufafanuzi,wamekuwa wakibwabwaja bwabwaja tu na kutolea ufafanuzi wa vitu ambavyo hata sisi hatuhitaji,siyo jero wala kilio. Yaani wamekuwa wakileta ngojera tu. Hata majibu ambayo amejibiwa mwalimu Iddy, wamebwabwaja bwabwaja tu, kilio cha mwalimu Iddy ilikuwa ni hii 6% anayotozwa mtu kila mwaka. Sasa wanavyisema mwalimu Iddy kaelewa na atakuwa balozi mwema sijui yeye binafsi wamemuondolea hiyo 6%
Kipengele hiki ni kandamizi, mbona watu wanaoidai serikali kwa miaka nenda rudi na wanambiwa wasubiri wao hawaikwekei serikali 6% kila mwaka kutunza thamani ya shilingi.
Jamani 6% ya kila mwaka inatuua, enyi viongozi wetu na bodi mtuonee huruma jamani. Tamzania ni yetu wote