Sheria ya bima ina upendeleo; Ukiwa huna bima ni kosa lakini ukidhulumiwa kulipwa na watoa bima wanakutelekeza

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,276
21,395
Iweje sheria iwe upande mmoja tu wa kunyonya?

Gari ikiwa haina bima ni kosa kwa mujibu wa sheria, kwahiyo polisi trafiki watakukamata mara moja! Lakini kwanini sheria hiyo hiyo haielekezi wazi ulazima wa mtoa bima kumlipa punde mteja wao bila kuzungushana? Mbaya zaidi kwanini meno ya polisi yakate upande mmoja tu wa kumshuritisha mtu akate bima ya gari, lakini wanakutelekeza unapofuatilia kulipwa.

Kwanini sheria isingewekwa wazi kwamba Mteja wa bima alipwe ndani ya siku 3 baada ya ajali kuthibitishwa na polisi na endapo akichelewa pesa iwe inaongezeka na baada ya siku 15 kama atakuwa hajalipa mtoa huduma akamatwe kwa nguvu!

Nini maana ya kumlazimishwa mtu kuwa na bima halafu asilipwe ajali inapotokea hadi wengine huamua kutengeza magari yao wenyewe?

Bongo kampuni nyingi za bima wakishapokea pesa za mteja hukimbilia kuzitumia kujengea nyumba zao na kuacha akaunti zikiwa tupu kiasi kwamba hawana uwezo wa kumlipa mteja wao akipatwa na tatizo zaidi ya kumzungusha kwasababu hakuna sheria inayowabana!
 
dmkali,

Ndio ubaya wa socialist country,nchi nzima ni welfare state

Ndio maana naikubali sana United States,ni full capitalism all out until it breaks and start again!

Greatest system ever!

Hapa mnachanga wote bima wenye uwezo,masikini wanatumia bure!
 
Ndio ubaya wa socialist country,nchi nzima ni welfare state

Ndio maana naikubali sana United States,ni full capitalism all out until it breaks and start again!

Greatest system ever!

Hapa mnachanga wote bima wenye uwezo,masikini wanatumia bure!Fvck it!
Ndo vilr
 
Iweje sheria iwe upande mmoja tu wa kunyonya?
Gari ikiwa haina bima ni kosa kwa mujibu wa sheria, kwahiyo polisi trafiki watakukamata mara moja!

Lakini kwanini sheria hiyo hiyo haielekezi wazi ulazima wa mtoa bima kumlipa punde mteja wao bila kuzungushana?
Mbaya zaidi kwanini meno ya polisi yakate upande mmoja tu wa kumshuritisha mtu akate bima ya gari, lakini wanakutekekeza unapofuatilia kulipwa.

kwanini sheria isingewekwa wazi kwamba Mteja wa bima alipwe ndani ya siku 3 baada ya ajali kuthibitishwa na polisi! Na endapo akichelewa pesa iwe inagezeka na baada ya siku 15 kama atakuwa hajalipa mtoa huduma akamatwe kwa nguvu!

Nini maana ya kumlazimishwa mtu kuwa na bima halafu asilipwe ajali inapotokea hadi wengine huamua kutengeza magari yao wenyewe?

Bongo kampuni nyingi za bima wakishapokea pesa za mteja hukimbilia kuzitumia kujengea nyumba zao na kuacha akaunti zikiwa tupu kiasi kwamba hawana uwezo wa kumlipa mteja wao akipatwa na tatizo zaidi ya kumzungusha kwasababu hakuna sheria inayowabana!
Brother siku Tatu kulipwa ni UONGO.

Kwenye Bima hao polisi Sio "final say", Kama Gharama ni kubwa hayo Makampuni ya Bima huteua "Assessor" kwa ajili ya kukagua mazingira ya hiyo ajali na value iliyokua claimed. Yaani wanakua waelekezi na washauri wa hayo makampuni ya Bima.

Mpaka kukagua na kuandika report napo huchukua siku kadhaa kulingana na muda Wao.

Tukija maofisini nako kuna mlolongo wa procedures, kama vile kufungua faili, kuitisha documents kutoka kwako mteja, documents za ajali, etc.

Na kwenye malipo napo kuna milolongo yake. Cheque aandike Mhasibu, ikahakikiwe na Mhasibu mwengine, kisha iende Signatory mmoja, kisha akamlizie Signatory mwengine, etc
 
Kingine pia cha kushangaza polisi wakiangali bima yako katika mtandao kama umepewa feki unakamatwa wewe

Wakati hizo documents za bima zina address zote kwa nini wasiende kuwakamata walio toa hiyo bima

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi kuna makampuni yanayotoa Bima feki? Na si Mpaka Wewe mwenye hiyo Bima feki uwapeleke ulikoipata. Hapo ni Sawa na umekutwa na noti feki, mtuhumiwa wa kwanza ni wewe kwanza.
 
Kwani mlolongo huo hautoshi kufanywa ndani ya siku tatu
Unajua brother fikiria tu gari iliyogongwa ikaumia vifaa mbali mbali, Hapo inabidi mtu mwenye uelewa wa mambo ya Gereji (assessor) aje akague. Sababu pia bei zinatofautiana, na pia kuna vya ku repair na kubadili vipya. Sasa kwa uelewa wangu field ya assessor and value adjustment haina watu wengi hivyo wa kuweza kufika on time eneo la tukio.

Mimi Niliwahi kupata ajali, nikaamua kufuatilia Mguu kwa Mguu with kampuni moja hivi, sikumtumia tena broker. Walikua wananipa updates kila walipofikia nkagundua kweli ukiwa nje unaweza kudhani wanafanya makusudi.
 
Sema kama umepigwa tu pasi na daladala labda nadhani hiyo ni issue ndogo tu
 
Pole mteja wa Bima, sheria zipo tatizo ni wahusika hatujatoa elimu ya kutosha au wengi hatusomi machapisho mbalimbali, karibu B&B INSURANCE BROKERS LTD, tupo mtaa wa Lindi jengo la SUWATA zilipo ofisi ndogo za UWT makao makuu mkabala na kituo cha mwendo kasi cha Gerezani, piga simu namba 0784255822, 0766898722 au 0769629833 utaelimishwa na utahudumiwa kitaaluma. Have a peace of mind and keep smiling. Karibu sana. dmkali,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole mteja wa Bima, sheria zipo tatizo ni wahusika hatujatoa elimu ya kutosha au wengi hatusomi machapisho mbalimbali, karibu B&B INSURANCE BROKERS LTD, tupo mtaa wa Lindi jengo la SUWATA zilipo ofisi ndogo za UWT makao makuu mkabala na kituo cha mwendo kasi cha Gerezani, piga simu namba 0784255822, 0766898722 au 0769629833 utaelimishwa na utahudumiwa kitaaluma. Have a peace of mind and keep smiling. Karibu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Eleza hapa hizo sheria; au tupia hizo posters hapa
 
Back
Top Bottom