Sheria ya Ardhi ina makosa

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,455
29,134
Ndugu wapendwa,
Kuna suala moja naona kama lina walakini, na ningepata wasaa ningemshauri Waziri wa Ardhi aliangalie kwa makini.
Mtu umejipinda ukapata pesa kidogo ukaingia maeneo ya Mbezi, Bonyokwa, Goba n.k kutafuta kipande cha Ardhi ili ujenge maana kodi haziaminiki mjini.
Unamalizana mwenye ardhi na kupitia michakato yote pale kijijini ili isiwe tabu baadae.
Kwakua hutaki shida unakwenda ardhi ili kukipima upewe hati kabisa,
Cha ajabu watu wa arhi wanakuja kukuambia kua kwa mujibu wa "Master Plan" ya mji, hapo ulipopata ni eneo la wazi/soko/barabara,
Swali langu ni kua, kwanini basi hizo master plan zisiwekwe huko kijijini ili kila anaenunua ajue hukohuko kua kaliwa?
Serikali ya kijiji inakupitisha kununua kwamba ni mahali halali,
Serikali kuu inakuja kukuambia kua sio, hapa imekaaje?
Kuna masuala ya kuchukua location ya eneo (GPS) ili ukapate uweli kuhusu hilo eneo wizarani, but ni wangapi wanajua kuhusu hii kitu?
Ni kweli unaweza kuomba amendment ya hiyo plan ikafanikiwa?
 
Ndugu wapendwa,
Kuna suala moja naona kama lina walakini, na ningepata wasaa ningemshauri Waziri wa Ardhi aliangalie kwa makini.
Mtu umejipinda ukapata pesa kidogo ukaingia maeneo ya Mbezi, Bonyokwa, Goba n.k kutafuta kipande cha Ardhi ili ujenge maana kodi haziaminiki mjini.
Unamalizana mwenye ardhi na kupitia michakato yote pale kijijini ili isiwe tabu baadae.
Kwakua hutaki shida unakwenda ardhi ili kukipima upewe hati kabisa,
Cha ajabu watu wa arhi wanakuja kukuambia kua kwa mujibu wa "Master Plan" ya mji, hapo ulipopata ni eneo la wazi/soko/barabara,
Swali langu ni kua, kwanini basi hizo master plan zisiwekwe huko kijijini ili kila anaenunua ajue hukohuko kua kaliwa?
Serikali ya kijiji inakupitisha kununua kwamba ni mahali halali,
Serikali kuu inakuja kukuambia kua sio, hapa imekaaje?
Kuna masuala ya kuchukua location ya eneo (GPS) ili ukapate uweli kuhusu hilo eneo wizarani, but ni wangapi wanajua kuhusu hii kitu?
Ni kweli unaweza kuomba amendment ya hiyo plan ikafanikiwa?

A very big concern. Sheria ya ardhi ina matatizo makubwa. Haikufanyiwa utafiti wa kutosha kabla ya kuipitisha. Waziri Tibaijuka ayaangalie haya mapungufu ni ya msingi sana tena sana. Lakini wana muda huo?
 
Kweli kabisa mkuu, sheria ya ardhi ina matatizo makubwa sana. Mipango miji hwawezi kuweka master plan wazi kwa sababu wanataka usubiri viwanja wapime wao na wakuuzie kwa rushwa na tena kwa gharama kubwa. Ukinunua kiwanja kwa wanakijiji maanake wao watakosa pesa.
Pia sheria ya aridhi inachangia umaskini. Watu wenye mashamba huko nje ya mji wananyang'anywa ardhi yao wanayoitegemea kwa kilimo bila kulipwa fidia, badala yake vinapimwa viwanja ambavyo vinauzwa na halmashauri badala ya wenye mashamba. Mtu anaponyang'anywa eneo ambalo amekuwa akilitegemea kujipatia mapato yake bila fidia maana yake ni kwamba huyo mtu tumemsukuma aende kuwa ombaomba wa milele. Ni unyama wa hali ya juu.
Ni afadhali mipango miji wachore ramani, viwanja auze mwenye ardhi maana Hilo ndo tegemeo lake, upimaji ufanywe na makampuni binafsi.
 
Kweli kabisa mkuu, sheria ya ardhi ina matatizo makubwa sana. Mipango miji hwawezi kuweka master plan wazi kwa sababu wanataka usubiri viwanja wapime wao na wakuuzie kwa rushwa na tena kwa gharama kubwa. Ukinunua kiwanja kwa wanakijiji maanake wao watakosa pesa.
Pia sheria ya aridhi inachangia umaskini. Watu wenye mashamba huko nje ya mji wananyang'anywa ardhi yao wanayoitegemea kwa kilimo bila kulipwa fidia, badala yake vinapimwa viwanja ambavyo vinauzwa na halmashauri badala ya wenye mashamba. Mtu anaponyang'anywa eneo ambalo amekuwa akilitegemea kujipatia mapato yake bila fidia maana yake ni kwamba huyo mtu tumemsukuma aende kuwa ombaomba wa milele. Ni unyama wa hali ya juu.
Ni afadhali mipango miji wachore ramani, viwanja auze mwenye ardhi maana Hilo ndo tegemeo lake, upimaji ufanywe na makampuni binafsi.

Umeleta wazo la haki. Kama kuna mipango miji, basi hatukatai, lakini viwanja viwe mali ya mwenye ardhi, auze yeye mwenye ardhi. Ni uonevu na unyama kumtoa mtu kwenye ardhi ambayo ameimiliki vizazi na vizazi, leo unamtoa kwa fidia kiduchu/kidogo. Halmashauri wanauza viwanja kwa rushwa kubwa sana. History will tell, ni wizi na unyama wa serikali yetu kwa wananchi wake.
 
Ni ujinga na uzembe wa serikali kusema ukweli. Kwa kiasi kikubwa serikali ndio inahamasisha makazi holela na migogoro ya ardhi. Ilitakiwa kila mwaka wa fedha serikali iwe inapima viwanja visivyopungua 20,000 na kujenga vilevile majumba mengi ya kupangisha kutokana na sekta yenyewe ya makazi na upangaji kuwa legelege na unregulated. Sasa kunapokosekana mipango ndio kunapokuja mambo kama haya. Sasa utashangaa siku hizi hata huko vijijini na kwene miji midogo kuna makazi holela wakati Tz haina matatizo ya ardhi.
 
Kwani kuna ugumu gani kwa mfano ku-print master plan ya Goba ukawapelekea hukohuko Goba wakae nayo wao ili akija mtu kununua ardhi kwa mwanakijiji wa-verify hukohuko kijijini kuliko kusubiri mpaka Wizarani?
Hawaoni kama itawarahisishia kazi,
pili kupunguza utapeli,
Tatu kuondoa kero kwa wananchi,
Nne kupunguza ujenzi holela?
Hivi kama kijiji kimeshanipitisha kununua hiyo ardhi wakati master plan inasema ni barabara, naweza kuwashitaki serikali ya kijiji na mamihuri yao waliyoyagonga?
 
Ndugu wapendwa,
Kuna suala moja naona kama lina walakini, na ningepata wasaa ningemshauri Waziri wa Ardhi aliangalie kwa makini.
Mtu umejipinda ukapata pesa kidogo ukaingia maeneo ya Mbezi, Bonyokwa, Goba n.k kutafuta kipande cha Ardhi ili ujenge maana kodi haziaminiki mjini.
Unamalizana mwenye ardhi na kupitia michakato yote pale kijijini ili isiwe tabu baadae.
Kwakua hutaki shida unakwenda ardhi ili kukipima upewe hati kabisa,
Cha ajabu watu wa arhi wanakuja kukuambia kua kwa mujibu wa "Master Plan" ya mji, hapo ulipopata ni eneo la wazi/soko/barabara,
Swali langu ni kua, kwanini basi hizo master plan zisiwekwe huko kijijini ili kila anaenunua ajue hukohuko kua kaliwa?
Serikali ya kijiji inakupitisha kununua kwamba ni mahali halali,
Serikali kuu inakuja kukuambia kua sio, hapa imekaaje?
Kuna masuala ya kuchukua location ya eneo (GPS) ili ukapate uweli kuhusu hilo eneo wizarani, but ni wangapi wanajua kuhusu hii kitu?
Ni kweli unaweza kuomba amendment ya hiyo plan ikafanikiwa?
Shark, sheria ina tatizo gani hapo specifically? Umesema "unamalizana na mwenye ardhi" halafu unaenda Ardhi kutafuta hati unakuta "umeliwa." Sasa hapo ndugu yangu, tatizo ni sheria au ni wewe uliyefanya mambo kinyumenyume? Hata ukinunua pikipiki huwezi "kumalizana" na mwenye pikipiki halafu useme "kwa kuwa hutaki shinda" unaenda TRA kuangalia usajili wa pikipiki kama aliyekuuzia ndie alikuwa mmiliki halali. Too late! Huwezi kufanya hivyo. Sembuse kiwanja?

Kaangalie allocation ya matumizi ya kiwanja kwenye master plan kabla hujanunua, na kabla ya kulaumu sheria.

 
Shark, sheria ina tatizo gani hapo specifically? Umesema "unamalizana na mwenye ardhi" halafu unaenda Ardhi kutafuta hati unakuta "umeliwa." Sasa hapo ndugu yangu, tatizo ni sheria au ni wewe uliyefanya mambo kinyumenyume? Hata ukinunua pikipiki huwezi "kumalizana" na mwenye pikipiki halafu useme "kwa kuwa hutaki shinda" unaenda TRA kuangalia usajili wa pikipiki kama aliyekuuzia ndie alikuwa mmiliki halali. Too late! Huwezi kufanya hivyo. Sembuse kiwanja?

Kaangalie allocation ya matumizi ya kiwanja kwenye master plan kabla hujanunua, na kabla ya kulaumu sheria.


Duu bwana Taso nashukuru mungu amekuleta hapa. Pale Morogoro vijijini kuna shamba nataka kulinunua ni la ukubwa wa ekari mia tatu hivi sasa kulingana na jinsi ulivyo kritisaiz kuhusu jinsi watu wanavyo ishambulia sheria kabla ya kufanya analysis ya hali halisi kuhusu sheria na pia kufanya tafiti ya ardhi kabla ya manunuzi, embu ngoja nikimbie kwanza lakini sjui niende wapi.

Je naweza nikaingia ofisi ya ardhi ya mkoa?? maana serikali ya kijiji tayari wameshatoa baraka kuwa ardhi ni ya anayeuza na haina shida yoyote kabisa.

Please kama humo umo pls endelea kunijuza.
 
Tatizo si sheria, ni mnunuzi wa ardhi anapoenda kwenye watu wasiohusika ambao anawaita "wenye ardhi!" Kwa nini asingewaomba hao "wenye ardhi" wampimie hiyo ardhi na kukimbilia ofisi za Mipango Miji?
 
A very big concern. Sheria ya ardhi ina matatizo makubwa. Haikufanyiwa utafiti wa kutosha kabla ya kuipitisha. Waziri Tibaijuka ayaangalie haya mapungufu ni ya msingi sana tena sana. Lakini wana muda huo?
<br />
<br />
masaburi yao yooote yanafikiria gamba la 2015
 
Kuna tofauti kati ya kuthibitisha uhalali na ku-registre ardhi iwe officialy yako ambayo ndio nayoizungumzia,
Pili sizungumzii sheria kwa vigezo vya vifungu vyake, bali utaratibu unaotumika ambapo sheria ndio inayosimamia.
Kama ni kuthibitisha Kijiji kishanithibitishia kua ni mali ya muuzaji.
Na kupima ili upate hati inaweza kua ni option tu, kwani asilimia kubwa tunaishi kwenye skwata na bado maisha yanaenda,
Elewa point yangu, kuna mgongano hapa kati ya serikali ya kijiji na serikali kuu!!
 
Tumia wataalamu wa ardhi ilikuepuka matatizo baada ya kununua kiwanja.Wengi wanaliwa sababu ya kutoelewa, na ubahili. matokeo yake ni doube allocation na kujenga kwenye matumizi ya public. Pale Mbezi Makonde kuna watu wameuziwa viwanja kwenye eneo la kiwanda linalomilikiwa kwa term ya 99 years. Wamejenga magorofa mazuri tu. Wiki 2 zilizopita mmiliki halali anakuja kujenga ukuta, wao oooh ulikuwa wapi muda wote!? Tutenganishe siassa na utaalamu wa ardhi. Sheria zipo sawa tu ila tunazidharau.
 
Tumia wataalamu wa ardhi ilikuepuka matatizo baada ya kununua kiwanja.
Hapo ndipo panapotokea tatizo, ushanunua halafu ndio baadae unakwenda kwa hao wataalamu wa ardhi ambao wanakuambia kua umeuziwa barabara,
Nafikiri ungesema "kabla" ya kununua
 
namimi naongeza kwamba ni sahihi kuwasiliana na wataalam kabla ya kufanya biashara yoyote maana cku hizi usanii ni mwingi kila mtu anatafuta pesa kwa njia anayoifahamu
 
Back
Top Bottom