Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini: Fahamu kuhusu kusitishwa kwa ajira kusiko kwa haki

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1608117488901.png

Kusitisha ajira maana yake ni kumalizika kwa mahusiano ya kikazi baina ya mwajiri na mwajiriwa au mfanyakazi, kusitisha ajira kihalali, kuachisha kazi isivyo halali, kusitisha kazi kwa makubaliano, mwajiri kusitisha kazi, kuachishwa kazi, kuacha kazi, kustaafu, kuritaya, mwenendo mbaya wa kazi, utovu wa nidhamu sehemu za kazi, kupunguzwa kazi, ridandasi, madhara ya kusitisha kazi isivyo halali, madhara ya kuachisha kazi isivyo halali

36. Kwa lengo la Sehemu hii Ndogo - (a) ''kusitishwa kwa ajira” kunajumuisha-

(i) kusitishwa ajira kwa haki chini ya sheria za kawaida zisizoandikwa;
(ii) kuacha kazi kwa mfanyakazi kwa sababu kuendelea kwake na kazi kunakuwa kugumu kwa sababu ya mwajiri;
(iii) kushindwa kuongeza mkataba kwa kipindi maalumu katika masharti yaleyale au yanayofanana nayo kama kulikuwa na matarajio ya kawaida ya kuongeza
(iv) kushindwa kumruhusu mfanyakazi kurudi kazini baada ya kuchukua likizo ya uzazi inayotolewa chini ya Sheria hii au likizo nyingine ya uzazi iliyokubaliwa; na
(v) kushindwa kumwajiri tena mfanyakazi kama mwajiri amesitisha ajira ya wafanyakazi wengi kwa sababu ileile au inayofanana na hiyo na ameamua kuwaajiri tena mmoja au zaidi kati yao;

(b) ''sitishwa ajira” ina maana inayofanana na “kusitishwa kwa ajira”. Kuachishwa kusiko kwa haki
 
Mkuu je kama mkataba umeisha na hujapewa mkataba mwingine au taarifa yoyote hapo inakuaje?
 
Mkuu je kama mkataba umeisha na hujapewa mkataba mwingine au taarifa yoyote hapo inakuaje?
Ninachojua mimi mkataba ukiisha usipopewa mkataba mwingine wala kupewa barua ya mwisho wa mkataba automatically umeingia kwenye mkataba mpya kama muendelezo wa ajira yako.

Heri ya mwaka mpya kwako kizwezwe
 
Ninachojua mimi mkataba ukiisha usipopewa mkataba mwingine wala kupewa barua ya mwisho wa mkataba automatically umeingia kwenye mkataba mpya kama muendelezo wa ajira yako.

Heri ya mwaka mpya kwako kizwezwe
Huo mkataba mpya sasa utakua unaisha lini?na vipi kuhusu mshahara itakua umebadilika?
 
Ninachojua mimi mkataba ukiisha usipopewa mkataba mwingine wala kupewa barua ya mwisho wa mkataba automatically umeingia kwenye mkataba mpya kama muendelezo wa ajira yako.

Heri ya mwaka mpya kwako kizwezwe
Usipopewa mkataba mpya automatically ajira yako imeishia hapo.

Utakachofanya ni kudai haki zako, ikiwemo barua na wewe kurudisha kilicho cha mwajiri.
 
Huo mkataba mpya sasa utakua unaisha lini?na vipi kuhusu mshahara itakua umebadilika?
Hicho ndio utatakiwa kuhoji t&c
Ila employer asipokupa maelekezo hadi inapita tarehe ya mwisho wa mkataba kazi inaendelea
 
Usipopewa mkataba mpya automatically ajira yako imeishia hapo.

Utakachofanya ni kudai haki zako, ikiwemo barua na wewe kurudisha kilicho cha mwajiri.
MosesKing nadhani mkataba utakua umeishia hapo kama ulikua una-state hivyo. Labda yeye kizwezwe aseme hiyo contract iliyoisha ilikua inasemaje?

Correct me if am wrong
 
Naomba kama kuna mwenye link ya soft copy ya hii Employment and Labor Relations Act ya kiswahili
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom