Sheria: Upelelezi usipokamilika ndani ya siku 60 mshatakiwa kuachiwa huru

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kifungu namba 225 (4) inasema Upelelezi usipokamilika ndani ya siku 60 mshatakiwa kuachiwa huru. Hiki ni kitu ambacho hakitekelezwi ipasavyo na mahakama na baadhi ya watuhumiwa wamekuwa wakikaa muda mrefu mahabusu

Hayo yameelezwa Februari 10, 2020 na wakili wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Fulgence Massawe katika maadhimisho ya siku ya sheria na mapendekezo ya maboresho ya mifumo ya utoaji haki

"Kuna haja ya wizara ya katiba na sheria kusisitiza utekelezaji katika hili kwani mbali na kuwapa haki watuhumiwa pia itapunguza msongamano wa mahabusu magerezani ambao wanaelezwa kuwa wengi kuliko wafungwa," amesema.

Mkurugenzi mtendaji wa LHRC, Anna Henga ameshauri makosa yote yawe na dhamana kwa kubadilisha masharti ya dhamana kulingana na aina ya kosa jambo litakalosaidia kudumisha dhana ya mtu kutoonekana kuwa na hatia mpaka pale mahakama itakapothibitisha

"Pia tunaunga mkono kauli ya Rais John Magufuli aliyoitoa siku ya maadhimisho ya sheria kuwa bado kuna changamoto kubwa ya upelelezi wa kesi, jambo linaloashiria kwamba Serikali ipo tayari kuchukua hatua katika kudumisha ustawi wa haki za binadamu hususani katika eneo la mfumo wa utoaji haki," amesema.
 
Tatizo liko kwetu wananchi kutokupigia kelele mambo ya msingi kama haya na kubaki tunakanyagana kugombea mafuta ya kichawi kutoka kwa maaskofu uchwara
 
Tatizo liko kwetu wananchi kutokupigia kelele mambo ya msingi kama haya na kubaki tunakanyagana kugombe mafuta ya kichawi kutoka kwa maaskofu uchwara
kwenye mambo hayo "wananchi" utasubiri sana.
watu kila uchao tunapandishiwa bei za vyakula (unga, sukari, mchele, nyanya, nk) lakini ah.. tupo tupo tu kama hatupo vile!
 
Tatizo lipo kwa maafisa wa mahakama na na kwa askari wanaofanya upelelezi na siyo vinginevyo.

Hakimu- ushahidi ukamilike au usikamilike hana cha kupoteza ilmradi tu mshahara wake unaingia mwisho wa mwezi.

Wakili wa kujitegemea hataki kesi iishe mahakamani haraka maana atakosa riziki.

Wakili wa serikali- pia na cha kupoteza hata kesi ikikaa miaka 20 ilmradi tu mwisho wa mwezi anapata mshahara wake.

Wapelelezi- hawa nao hawana cha kupoteza kabisa.

Mwananchi/mtuhumiwa- Huyu huwa hajui afanye nini mahakamani kama anajitetea mwenyewe. chochote anachoambiwa anakubali hawezi kupinga maana hajui sheria inasemaje kuhusu hilo jambo. ingawa kutokujua sheria siyo kinga kisheria. Hivyo huyu hupelekwa kama ng'ombe tu.

MWISHO: Ukitaka kesi iishe haraka ongea vizuri na wakili wako. Baada ya hapo wakili ataongea na Hakimu, wakili wa serikali na wapelelezi na siku inayofuata kesi itaisha haraka sana hata kwa kufutwa kabisa au wataonesha nia ya kutoendelea na hiyo kesi.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Tatizo lipo kwa maafisa wa mahakama na na kwa askari wanaofanya upelelezi na siyo vinginevyo.

Hakimu- ushahidi ukamilike au usikamilike hana cha kupoteza ilmradi tu mshahara wake unaingia mwisho wa mwezi.

Wakili wa kujitegemea hataki kesi iishe mahakamani haraka maana atakosa riziki.

Wakili wa serikali- pia na cha kupoteza hata kesi ikikaa miaka 20 ilmradi tu mwisho wa mwezi anapata mshahara wake.

Wapelelezi- hawa nao hawana cha kupoteza kabisa.

Mwananchi/mtuhumiwa- Huyu huwa hajui afanye nini mahakamani kama anajitetea mwenyewe. chochote anachoambiwa anakubali hawezi kupinga maana hajui sheria inasemaje kuhusu hilo jambo. ingawa kutokujua sheria siyo kinga kisheria. Hivyo huyu hupelekwa kama ng'ombe tu.

MWISHO: Ukitaka kesi iishe haraka ongea vizuri na wakili wako. Baada ya hapo wakili ataongea na Hakimu, wakili wa serikali na wapelelezi na siku inayofuata kesi itaisha haraka sana hata kwa kufutwa kabisa au wataonesha nia ya kutoendelea na hiyo kesi.
Umehitimisha vyema sana. Wakili, hakimu, mwanasheria wa serikali na mpelelezi lao ni moja. Na ndiyomaana ukikata hela ndefu kwa wakili wako kesi hata iwe nzito vipu, hubadilika ghafla na kuwa nyepesi kwani wakili humkatia hakimu, mwanasheria wa serikali na mpelelezi. Shida ni kwetu sisi wananchi walalahoi na wakosaji, unaozea jela au unapoteza haki yako kama huna pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio matatizo ya kuishi in a pithole country,kisheria unatakiwa umpeleke mahakamani suspect within 48hrs baada ya kumkamata kwa kosa,na pia huwezi to ARREST hadi utakapokuwa umejiridhisha without doubts kuwa mtuhumiwa ana kesi ya kujibu sisi tunakamata kwanza na upelelezi unafuatia badala ya kuwa otherway round.
 
Back
Top Bottom