Mimi nimekuwa nikijiuliza sababu gani Mbunge anayeishi Kinondoni Dar, anaweza vipi kugombea Ubunge jimbo la Babati au Rorya wakati mwananchi asiyeishi jimbo hilo haruhusiwi kupiga kura jimbo lolote.
Kuna sababu gani haswa zilizopelekea sheria hii kutungwa na kuna faida gani? Je, sheria hii haizai Ukabila kiasi kwamba mkazi wa Dar ataenda kwao kugombea Ubunge wakati si mkazi wa huko na kishahama yeye na familia yake?.
Nijuavyo, kwa taratibu za Kugombea Ubunge, mgombea hatakiwi kugombea nje ya jimbo analoishi maana wananchi wa huko hawamfahamu vizuri uwezo wake, sii mkazi hawezi kuyajua ama kuyafuatilia matatizo yao na pili kuhusiana na wakazi wanalazimika kupiga kura katika majimbo yao kwa sababu wanayataka maendeleo ya jimbo wanaloishi na kiongozi watakayemchagua ndiye anayefaa kukuwakilisha jimboni.
Mpango huu una mantiki na unaeleweka sehemu zote duniani lakini mfumo wa Tanzania kusema kweli siuelewi maana yake wala sababu za kwa nini mbunge anaruhusiwe kugombea sehemu yoyote asiyoishi? Kwanini? Halafu upande wa pili mpiga kura haruhusiwi kupiga kura sehemu asiyoishi.
Wanabodi nawaomba darasa maana nijuavyo gharama za Ubunge zinazidi kuwa kubwa kutokana na mifumo vibovu kama hii.
Kuna sababu gani haswa zilizopelekea sheria hii kutungwa na kuna faida gani? Je, sheria hii haizai Ukabila kiasi kwamba mkazi wa Dar ataenda kwao kugombea Ubunge wakati si mkazi wa huko na kishahama yeye na familia yake?.
Nijuavyo, kwa taratibu za Kugombea Ubunge, mgombea hatakiwi kugombea nje ya jimbo analoishi maana wananchi wa huko hawamfahamu vizuri uwezo wake, sii mkazi hawezi kuyajua ama kuyafuatilia matatizo yao na pili kuhusiana na wakazi wanalazimika kupiga kura katika majimbo yao kwa sababu wanayataka maendeleo ya jimbo wanaloishi na kiongozi watakayemchagua ndiye anayefaa kukuwakilisha jimboni.
Mpango huu una mantiki na unaeleweka sehemu zote duniani lakini mfumo wa Tanzania kusema kweli siuelewi maana yake wala sababu za kwa nini mbunge anaruhusiwe kugombea sehemu yoyote asiyoishi? Kwanini? Halafu upande wa pili mpiga kura haruhusiwi kupiga kura sehemu asiyoishi.
Wanabodi nawaomba darasa maana nijuavyo gharama za Ubunge zinazidi kuwa kubwa kutokana na mifumo vibovu kama hii.