Sheria ipi na kifungu gani kinachoruhusu wanafunzi elimu ya juu kubeba mimba au kuoa au kuolewa

magaka Makoye

Member
Sep 11, 2011
5
2
Wana JF nisaidieni.
Pia wataalamu au wanojua mnifahamishe. Kwamba form Four wamemaliza mitihani na form Six wanamaliza mitihani yao mwezi wa pili mwaka kesho 2012. Lakini wote hao wangeoa, kuolewa ama kupata mimba wakiwa wanafunzi wangepata matatizo makubwa sana ikiwemo kufukuzwa shule au kufungwa jela.
LAKINI kwa mwanafunzi wa chuo hata kama anasomea cheti AKIBEBA MIMBA, KUOLEWA AMA KUOA huwa hawachukuliwi hatua yoyote........! Sasa naambiwa kuna sheria ya elimu ya juu inaruhusu. Naomba mnisaidie ni sheria gani (jina lake) na kifungu kipi (kama ikibidi). Kisha tujadili mfano mwanafunzi anayesomea cheti je nayeye anahesabika kuwa anasoma elimu ya juu?
Asanteni sana.
 
kwani ni kifungu kipi cha sheria kinachoruhusu kuwa na bf chuoni? unajua kama kuna limit ya umri wa kusoma sekondari,ndo maana ilibidi ianzishwe programu ya memkwa kwa ajili yetu sie senior hgalz? kuna mtu ameolewa vyuo viwili na ana watoto 6 saa hizi ndo yuko chuo kikuu,huwezi kumkataza kuzaa kaka!
 
kuhusu cheti, nadhani wanaosomea ualimu ndo wanalazimika kuahirisha masomo kama watakua wajawazito(ukizingatia vyuo vya ualimu viko chini ya wizara na sio higher learning).kule nahisi hata kusimamisha mnazi unaweza kupewa adhabu ya kufyeka.
 
Hili swali halijakaa sawasawa! Kwani kubeba mimba ni lazima uruhusiwe? Itabidi tutunge sheria za kuruhusu mambo mengi sana kama ni hivyo!
 
Sidhani kama kuna sheria kama hiyo, kama amefikia umri wa kisheria kuolewa/oa (18 kwa mwanaume na 15 kwa msichana) hakuna tatizo.
Pia hakuna sheria inayokataza mwanafunzi wa primary/secondary kupata mimba, ila sheria inasema unaweza kufukuzwa shule kama
a) atakuwa na tabia ambayo inaweza kuchafua jina la shule na kuvuruga kabisa
viwango vya nidhamu vilivyowekwa hapo shuleni,
b) atatenda kosa la jinai au,
c) ataoa au kuolewa

So hiyo section A inategemea na interpretation yako, unaweza kuiapply sehemu yoyote.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom