Sheria inayomhukumu miaka 30 mwanaume aliyemtia mimba binti wanafunzi au aliye chini ya miaka18 ni kandamizi na inasababisha mzigo mzito wa walezi

sambulugu

JF-Expert Member
Jun 1, 2021
3,796
7,015
Ni kweli kutiwa mimba kwa mwanafunzi au msichana chini ya miaka 18 inamnyima fursa huyo binti ya kusoma na kutengeneza maisha yake ya baadae!

Leo waziri wa Elimu Joyce Ndalichako anatarajiwa kutoa waraka wa kuwaruhusu mabinti waliotiwa mimba kuendèlea na masomo! Je nauliza maswali yafuatayo!

•Kwanini isitafutwe adhabu mbadala kwa watuhumiwa ili kuwezesha mtuhumiwa kumhudumia mtoto huku mama akiendelea na masomo?

•Serikali haioni kuwa kumfunga baba wa mtoto ni kumnyima mtoto haki ya malezi na atakapo kua mkubwa inaweza kumwathiri kisaikojia?

•Kwanini Serikali isitoe adhabu kwa wasichana waliochini ya umri wa miaka 18 ambao tayari wamebarehe pindi watakapo bainika kujihusisha na mahusiano ya kingono?

•Kwanini sheria isiweke adhabu pekee kwa mwanaume aliyesababisha ujauzito pasipo maridhiano na binti nikimaanisha UBAKAJI?

Naomba sana kama wote tujuavyo jamii imebadilika sana na watoto wetu wanamihusisha na ngono hata wazazi bila kujua na hujua tu inapotokea mimba!

Natoa rai kwa wahusika wa kutunga sheria na haki zingine za kibinadamu kulitazama hili! Na isionekane kuwa kitendo cha mimba hata kama kulikuwa na makubalianao kati ya binti na kijana eti ni ubakaji!

Mwisho mimi ni mhanga wa kusimesha mtoto aliyeachwa na baba yake katika mazingira haya wakati najua pasina shaka kuwa wahusika walikuwa kwenye makubalianao bila kushinikizwa! Iweje ionekane uharifu!
 
Una hoja nzuri

Ila unashindwa kuiwasilisha ukaeleweka.

Hivi Unakaa unakubaliana Nini na mtoto mdogo wa chini ya miaka 18 Kwenye maswala ya ngono na uasherati?

Hivi Unataka kunambia uyo mtoto ana akili timamu ya kuweza kuchanganua lipi jema lipi baya nyege zikishampanda?

Hebu mkuu jiheshimu Basi, acha kutetea ubakaji bhana

IMG_20210928_230806.jpg
 
Una hoja nzuri,
Ila unashindwa kuiwasilisha ukaeleweka.

Hivi Unakaa unakubaliana Nini na mtoto mdogo wa chini ya miaka 18 Kwenye maswala ya ngono na uasherati?

Hivi Unataka kunambia uyo mtoto ana akili timamu ya kuweza kuchanganua lipi jema lipi baya nyege zikishampanda?

Hebu mkuu jiheshimu Basi,
acha kutetea ubakaji bhanaView attachment 2021935
Daaa mkuu! Bila shaka kunielewa ni vigumu! Ila nasema kwa nini tufunge watu wakati tunaacha watoto mtaani wakitaabika! Sheria iwepo ila marekebisho yafanyike!
 
Ni kweli kutiwa mimba kwa mwanafunzi au msichana chini ya miaka 18 inamnyima fursa huyo binti ya kusoma na kutengeneza maisha yake ya baadae!

Leo waziri wa Elimu Joyce Ndalichako anatarajiwa kutoa waraka wa kuwaruhusu mabinti waliotiwa mimba kuendèlea na masomo! Je nauliza maswali yafuatayo!

•Kwanini isitafutwe adhabu mbadala kwa watuhumiwa ili kuwezesha mtuhumiwa kumhudumia mtoto huku mama akiendelea na masomo?

•Serikali haioni kuwa kumfunga baba wa mtoto ni kumnyima mtoto haki ya malezi na atakapo kua mkubwa inaweza kumwathiri kisaikojia?

•Kwanini Serikali isitoe adhabu kwa wasichana waliochini ya umri wa miaka 18 ambao tayari wamebarehe pindi watakapo bainika kujihusisha na mahusiano ya kingono?

•Kwanini sheria isiweke adhabu pekee kwa mwanaume aliyesababisha ujauzito pasipo maridhiano na binti nikimaanisha UBAKAJI?

Naomba sana kama wote tujuavyo jamii imebadilika sana na watoto wetu wanamihusisha na ngono hata wazazi bila kujua na hujua tu inapotokea mimba!

Natoa rai kwa wahusika wa kutunga sheria na haki zingine za kibinadamu kulitazama hili! Na isionekane kuwa kitendo cha mimba hata kama kulikuwa na makubalianao kati ya binti na kijana eti ni ubakaji!

Mwisho mimi ni mhanga wa kusimesha mtoto aliyeachwa na baba yake katika mazingira haya wakati najua pasina shaka kuwa wahusika walikuwa kwenye makubalianao bila kushinikizwa! Iweje ionekane uharifu!
Nani kasema huyo Ni baba wa Mtoto wakati hakuna fungamano la ndoa hapo?
Hana haki hata ya kurithi kwa mujibu wa sheria za Tanzania na za Kiislamu,
Huyo Kijana ameongeza Machokoraa mtaani. wacha yamkute hayo.
Kama ingelikuwa tunatumia sheria za kislamu, Mwanaume angelichapwa bakora 100 na Binti naye 100 bila huruma mutawaliya.
Kama wangelibuka bila kifo au vilema baada ya kuchapwa wangeliachiwa kuendelea na maisha.lakini Ngono zembe na nyege mshindo wangeliikimbia kama ukoma katika maisha yao .

sasa miaka 30 au 80 kule zenji ni sawa na nusu kifo cha uhai wa mtu mwenye umriwa miaka 23+ 30 ni 53 na akiwa na 30+30 ni 60
hali si shwari.
 
Hoja yako ni nzuri na pia ni fikirishi.

Naungana na ww. Adhabu hiyo ni kandamizi kwa mwanaume.

Kama hoja ni kumuhadaa/kumlaghai mtoto wa kike. Basi Mm nadhan wangeweka sheria. Na Kuhukumu huyo aliyempa Mimba kulingana na Miaka aliyonayo.

Kijana wa miaka 20(hana pesa, hata kaz ya kuunga unga) na msichana wa miaka 16 au 17 . Wanalaghaliana vipi? Si Wooote wanadanganyana hawa.

Ila kwa mm nina miaka yangu 30's nikitembea na msichana anayesoma sekondari na nikampa Mimba basi sheria ndio inihukumu.

Ila sio hawa vijana wetu wadogo aiseee.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Kwanini wasifungwe wote jela na huyo mtoto mwenyewe maana jela Kuna chakula kule japo saa 10 jion mmeshalala
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom