MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,783
Makosa ya uhaini,
Mara nyingi hutafsiriwa kama nyanja ya mahusiano baina ya Serikali na raia wa nchi husika. Raia wa nchi husika anapofanya vitendo vya hujuma dhidi ya taifa lake huyo huhesabiwa kama mhaini. Vitendo hivyo ni kama Kushirikiana na adui wa Jamhuri, Kutaka kumdhuru Raisi wa nchi yako, Kutaka kupindua serikali na Kuitesa Serikali.
Hapa nchini Tanzania uhaini umetafsiriwa kisheria katika barabara iendayo kumoja tu, ambapo uhaini ni vile vitendo vinavyoweza kufanywa na raia dhidi ya Serikali yao. Hii dhana imejikita katika kuamini kwamba MTAWALA HAWEZI KUKOSEA KAMWE wala hawezi kufanya hujuma dhidi ya Jamhuri anayoingoza. Je, hii dhana ina ukweli wowote ule ndani yake ???
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikosea na wananchi wasiridhike naye Katiba yetu ya mwaka 1977 inasema ataondolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano tu. Mbali na hapo haitawezekana kabisa kumgusa kabisa kwasababu amepewa kinga (Immunity) inayomlinda dhidi ya kuburuzwa mahakamani akiwa madarakani na akistaafu. Kwa kiingereza tunasema Functional Immunity na Personal Immunity, hivyo hawezi kuguswa kabisaaa.
Sasa naomba niulize:
Je, kama imegundulika kwamba mkuu wa nchi amefanya hujuma dhidi ya Jamhuri ya anayoiongoza hapa Sheria ya nchi yetu inasemaje ???? Ataguswa na nani ???
Mara nyingi hutafsiriwa kama nyanja ya mahusiano baina ya Serikali na raia wa nchi husika. Raia wa nchi husika anapofanya vitendo vya hujuma dhidi ya taifa lake huyo huhesabiwa kama mhaini. Vitendo hivyo ni kama Kushirikiana na adui wa Jamhuri, Kutaka kumdhuru Raisi wa nchi yako, Kutaka kupindua serikali na Kuitesa Serikali.
Hapa nchini Tanzania uhaini umetafsiriwa kisheria katika barabara iendayo kumoja tu, ambapo uhaini ni vile vitendo vinavyoweza kufanywa na raia dhidi ya Serikali yao. Hii dhana imejikita katika kuamini kwamba MTAWALA HAWEZI KUKOSEA KAMWE wala hawezi kufanya hujuma dhidi ya Jamhuri anayoingoza. Je, hii dhana ina ukweli wowote ule ndani yake ???
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikosea na wananchi wasiridhike naye Katiba yetu ya mwaka 1977 inasema ataondolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano tu. Mbali na hapo haitawezekana kabisa kumgusa kabisa kwasababu amepewa kinga (Immunity) inayomlinda dhidi ya kuburuzwa mahakamani akiwa madarakani na akistaafu. Kwa kiingereza tunasema Functional Immunity na Personal Immunity, hivyo hawezi kuguswa kabisaaa.
Sasa naomba niulize:
Je, kama imegundulika kwamba mkuu wa nchi amefanya hujuma dhidi ya Jamhuri ya anayoiongoza hapa Sheria ya nchi yetu inasemaje ???? Ataguswa na nani ???