‘Sheria hairuhusu vileo kuingizwa Pemba’

Pepombili

JF-Expert Member
Dec 20, 2010
439
58
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Hassan Nasir amesema Sheria ya Kupiga Marufuku Kuingiza Vinywaji vyenye Kilevi katika kisiwa cha Pemba ya mwaka 1928 bado ipo na haijafutwa.
Kamanda Nassir alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Waislamu waliokuwa wakitishia kufanya maandamano kupiga kuwepo kwa ghala la kuhifadhi vinywaji vyenye kilevi huko Tibirinzi.
Nassiri alisema sheria hiyo inapiga marufuku watu binafsi kuingiza na kuuza vinywaji hivyo katika kisiwa cha Pemba isipokuwa kwa taasisi za ulinzi tu ikiwemo Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika makambi yao.
“Sheria ya Kupiga Marufuku Kuingiza Kinywaji chenye Kilevi kisiwani Pemba ipo na haijafutwa…. ni marufuku kuingiza kinywaji hicho isipokuwa kwa taasisi za ulinzi tu na kinywaji hicho kipatikane katika kambi za jeshi,” alisema.
Aliwataka Waislamu waliokuwa wakitishia kufanya maandamano kuwa watulivu wakati shauri lao hilo likifanyiwa kazi na taaasi husika ikiwemo vyombo vya ulinzi.

Safi sana wananchi wa pemba hakikisheni munalinda na kusimamia hio sheria
 
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Hassan Nasir amesema Sheria ya Kupiga Marufuku Kuingiza Vinywaji vyenye Kilevi katika kisiwa cha Pemba ya mwaka 1928 bado ipo na haijafutwa.<br />
Kamanda Nassir alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Waislamu waliokuwa wakitishia kufanya maandamano kupiga kuwepo kwa ghala la kuhifadhi vinywaji vyenye kilevi huko Tibirinzi.<br />
Nassiri alisema sheria hiyo inapiga marufuku watu binafsi kuingiza na kuuza vinywaji hivyo katika kisiwa cha Pemba isipokuwa kwa taasisi za ulinzi tu ikiwemo Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika makambi yao.<br />
“Sheria ya Kupiga Marufuku Kuingiza Kinywaji chenye Kilevi kisiwani Pemba ipo na haijafutwa…. ni marufuku kuingiza kinywaji hicho isipokuwa kwa taasisi za ulinzi tu na kinywaji hicho kipatikane katika kambi za jeshi,” alisema.<br />
Aliwataka Waislamu waliokuwa wakitishia kufanya maandamano kuwa watulivu wakati shauri lao hilo likifanyiwa kazi na taaasi husika ikiwemo vyombo vya ulinzi.<br />
<br />
Safi sana wananchi wa pemba hakikisheni munalinda na kusimamia hio sheria
<br />
<br />
kuna ulanzi na gongo vyote vyatengenezwa kutoka kwenye karafuu ni noma
 
Wakaangalie kwenye takwimu za VAT (Zanzibar). Makato yatokanayo na mauzo ya pombe ndiyo yanaongoza kwenye mapato ya VAT!
 
Wakaangalie kwenye takwimu za VAT (Zanzibar). Makato yatokanayo na mauzo ya pombe ndiyo yanaongoza kwenye mapato ya VAT!
<br />
<br />
Sio kweli umedanganya wana JF. Tuwekee takwimu hapa. Tuhakikishe.
 
wanafiki wakubwa hao Wapemba na sheria zao kandamizi,. Uislam hauishii kwenye vilevi, wanafikiri kirahisi sana, na huenda wao wenyewe wanakunywa sana pombe ya mnazi, wivu umewajaa labda hawana fedha ya kununulia Pombe za madukani, Ujinga, ujinga , ujinga.
 
wanafiki wakubwa hao Wapemba na sheria zao kandamizi,. Uislam hauishii kwenye vilevi, wanafikiri kirahisi sana, na huenda wao wenyewe wanakunywa sana pombe ya mnazi, wivu umewajaa labda hawana fedha ya kununulia Pombe za madukani, Ujinga, ujinga , ujinga.
Ningelifurahi kusikia maneno kama haya yakisemwa na Mpemba angalau mmoja, lakini kusemwa na mtu wa nje....mmmmmhhh!
 
wakataa pombe huku mgao utokanao na kodi ya kilevi i.e konyagi, lager n.k wanachukua na kukomaa mgao uongezwe, naona kama wana matatizo mengi hivi, mara kigezo cha uislamu mara uzanzibar, naona wanataka kwenda peponi bila kuishinda dhambi, nawashauri wapambane kwani kwa mujibu wa vitabu shetani tunaye duniani, alitimuliwa mbinguni, na znz ni sehemu ya dunia, kama vipi wahame wenyewe.
 
Back
Top Bottom