Pythagoras
JF-Expert Member
- Sep 24, 2013
- 1,632
- 3,814
mkubwa akipita katikati ya uwanja wote mnaganda ata kama ulianguka unakaa chini hapo hapo hadi amalize kupita
Ukisafa mpk mwisho ujue umelala nacho na wimbo unaimbiwa.Dana dana kuhesabihana, iwe ya mguu mmoja au iwe ya miguu miwili.
Kontroo, Vichwa, Tobo bao.
Mtu kati (unasafa), hapa zipo za aina mbili. Kuna ile moja ukigusa tu Mpira kwa yule aliekuwa nao, ujue hapo umejikomboa na yeye inakuwa zamu yake kusafa.
Na kuna ile nyingine lazima unyang'anye Mpira ndio ujikomboe na yule uliemnyang'anya inakuwa zamu yake kusafa.
Hapa kwenye kusafa panakuwaga patamu, pale inapotokea mmoja wenu kusafa kwa muda mrefu, mpaka anaesafa anakasirika.
Kabla ya kuanza napenda zaidi pale mnapoanza kuweka uamuzi kusafa kwa aina gani, Kugusa au kunyang'anya.
Maisha haya.
Eti sasa hivi na mie HARUFU naitwa Baba.
Jamani
Hapo kwenye Mdako umenikumbusha mbali.Kweli kabisa yani kwa wasichana siku hizi hata rede,makida na mdako ni nadra sana kukuta wakicheza..utandawazi pia umetuathiri tunajenga nyumba ndani tiles nje vitofali vile chini hatubakizi ata kasehemu ka mchanga na udongo mtoto ata achimbe shimo la mdako na vishimo vya bao au achore kipande aruke aruke mtoto siku hizi akishika tu udongo mzazi anafoka minyoo akienda kucheza rede anaambiwa chokoraa...nitoe wito kwa wazazi watoto ni michezo ukiruka stage za mchezo utotoni matokeo yake ukikua sasa unaanza kuruka ruka kama mtoto
Hyo kwetu inaitwa toka ingia hapo kama marafiki na mnapenda mcheze timu moja mnatafta mtu mnamuweka katikati yenuNakumbuka wakati wa kuchagua team mnajipanga mstari mmoja mrefuu halafu yule mbabe ndio anasimamia zoezi la waliojipanga,mmoja anarudi nyuma na anayefuatia anapiga hatua mbele,ilikua mmoja anasogea mbele anayefuata anarudi nyuma mpaka zinapatikana team mbili,team ya waliorudi nyuma na waliopiga hatua mbele!!
Mimi hata REDE nilikuwa najichanganya pia.Kweli kabisa yani kwa wasichana siku hizi hata rede,makida na mdako ni nadra sana kukuta wakicheza..utandawazi pia umetuathiri tunajenga nyumba ndani tiles nje vitofali vile chini hatubakizi ata kasehemu ka mchanga na udongo mtoto ata achimbe shimo la mdako na vishimo vya bao au achore kipande aruke aruke mtoto siku hizi akishika tu udongo mzazi anafoka minyoo akienda kucheza rede anaambiwa chokoraa...nitoe wito kwa wazazi watoto ni michezo ukiruka stage za mchezo utotoni matokeo yake ukikua sasa unaanza kuruka ruka kama mtoto
Nakumbuka nilijikata Mguuni (Nyayoni), na kwa jinsi nlivyokuwa naupenda Mpira nilikuwa nakosa raha sana.Kuna watu ambao ilikuwa ukipigana nao Bambi lazima mguu uvimbe.
Mkuu usiumie sana,furahia maisha kwa wakati ulio nao coz hata huu wakati ulionao sasa pia utaujutia au utaukumbuka baada ya miaka 10 au 20 ijayo,Wengine wamefurahishwa na huu uzi.Lakn mi nimeumia san.Nimekumbuka maisha ambayo hayatarudi had naingia kaburini
Kama Mimi aisee, walikupa aka gani?Hii ilinipa aka
SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha