Sherehe zinazofanywa na Ubalozi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Waungwana,

Kama mtakumbuka wiki chache zilizopita mwenzetu mmoja wa Sweden (kama sikosei) aliandika hapa kuonyesha kushangazwa kwake na sherehe ya Muungano ya 2008 ambayo ubalozi wa Tanzania Sweden ulitangaza itafanyika na hivyo kuwaalika Watanzania toka miji mbali mbali ya Sweden na nchi za jirani. Mwenzetu huyo alidai kwamba alishangazwa baada ya balozi kutotokea kwenye sherehe hizo na hata hakukuwa na ofisa yeyote toka ubalozini. Ninachofahamu ni kwamba balozi zetu zinapewa fungu maalum ili kufanyia sherehe za Muungano.

Je, inawezekana hizi sherehe zinatumika kufanya ufisadi? Hapa kuna uwezekano ubalozi haukutumia hata senti tano, lakini labda huko mambo ya nje inapelekwa bill kwamba walialikwa Watanzania 300 na zilitumika kiasi kadhaa kugharamia sherehe hizo.

 
Waungwana,

Kama mtakumbuka wiki chache zilizopita mwenzetu mmoja wa Sweden (kama sikosei) aliandika hapa kuonyesha kushangazwa kwake na sherehe ya Muungano ya 2008 ambayo ubalozi wa Tanzania Sweden ulitangaza itafanyika na hivyo kuwaalika Watanzania toka miji mbali mbali ya Sweden na nchi za jirani. Mwenzetu huyo alidai kwamba alishangazwa baada ya balozi kutotokea kwenye sherehe hizo na hata hakukuwa na ofisa yeyote toka ubalozini. Ninachofahamu ni kwamba balozi zetu zinapewa fungu maalum ili kufanyia sherehe za Muungano.

Je, inawezekana hizi sherehe zinatumika kufanya ufisadi? Hapa kuna uwezekano ubalozi haukutumia hata senti tano, lakini labda huko mambo ya nje inapelekwa bill kwamba walialikwa Watanzania 300 na zilitumika kiasi kadhaa kugharamia sherehe hizo.


Fungu lipo.
Iwapo linatumiwa ipasavyo, wanaweza kutueleza wakaguzi wa mahesabu.
 
Fungu lipo.
Iwapo linatumiwa ipasavyo, wanaweza kutueleza wakaguzi wa mahesabu.

Watatueleza vipi ikiwa wanaona bili ya ukumbi na chakula kumbe hakuna ukumbi uliokodishwa, chakula kilichonunuliwa na hata ofisa mmoja wa ubalozi hakuonyesha pua yake. Umeshawahi kusikia matumizi mbali mbaliya mabilioni katika balozi zetu ambayo hayana stakabadhi? Basi nadhani ya sherehe zinazosimamiwa na balozi nayo hufichwa humo humo.
 
Mnakamata wenzenu pabaya wajameni, wenzenu walishaandika kwamba mkutano uliwagharimu dola 50,000/-; sasa munaleta kelele zenu...

kwi kwi kwi
 
Mnakamata wenzenu pabaya wajameni, wenzenu walishaandika kwamba mkutano uliwagharimu dola 50,000/-; sasa munaleta kelele zenu...

kwi kwi kwi

Tutalala mbele na mafisadi kila kona ili kuhakikisha tunawasambaratisha.
 
Niliishi Japani miaka ya 90, lakini hata mara moja hatukuwahi kualikwa ubalozini kwa ajili ya sherehe yeyote.Cha ajabu sisi Watanzania tuliokuwa tunaishi kule tulikuwa tunachangishana kwa ajili ya kufanya sherehe. na huwezi amini,tulikuwa tunambembeleza balozi aturuhusu tufanye tafrija ktk ukumbi wa pale ubalozini. Nakumbuka ni mara moja tu balozi alikuja ktk sherehe hiyo. Kwetu sisi ubalozi ilikuwa ni kero na walikuwa hawatoi msaada wowote. sasa hivi nimemsahau kidogo jina la huyo balozi mstaafu lakini aliwahi kugombea ubunge Kigamboni na akashinda anaishi pale Mlalakuwa na anatoka Mtwara au Lindi
 
Niliishi Japani miaka ya 90, lakini hata mara moja hatukuwahi kualikwa ubalozini kwa ajili ya sherehe yeyote.Cha ajabu sisi Watanzania tuliokuwa tunaishi kule tulikuwa tunachangishana kwa ajili ya kufanya sherehe. na huwezi amini,tulikuwa tunambembeleza balozi aturuhusu tufanye tafrija ktk ukumbi wa pale ubalozini. Nakumbuka ni mara moja tu balozi alikuja ktk sherehe hiyo. Kwetu sisi ubalozi ilikuwa ni kero na walikuwa hawatoi msaada wowote. sasa hivi nimemsahau kidogo jina la huyo balozi mstaafu lakini aliwahi kugombea ubunge Kigamboni na akashinda anaishi pale Mlalakuwa na anatoka Mtwara au Lindi


Ahsante kwa kutufahamisha hii habari. Lazima tulipigie kelele hili kwa uwezo wetu wote maana baadhi ya mabalozi hata maofisa hujiona kama miungu watu na hutumia balozi hizo kufanya ufisadi kama alioufanya Mahalu pale Italy. Nadhani ufisadi alioufanya Mahalu pale Italy wa kununua nyumba na kuoverstate bei ya nyumba ile unafanyika katika balozi nyingi tangu serikali ilipoamua kwamba kupangisha nyumba ni more expensive ukilinganisha na kuwa na nyumba zao wenyewe. Labda aliyekuja na hiyo idea aliona kuna mwanya unaoweza kutumika kufanya ufisadi wao kupitia nyumba walizonunua.
 
Back
Top Bottom