Sherehe za uhuru wa zanzibar 10 december 1963 zafanyika scandinavia leo

Fatal5

Senior Member
Jul 1, 2011
187
34
Maadhimisho ya kumbukumbu ya siku ya Uhuru wa Zanzibar

PIC_0325-564x272.jpg


Wazanzibari kutoka sehemu mbalimbali za Skandinavia walikutana jana kusherehekea kumbukumbu ya siku ya Uhuru wa Zanzibar wa tarehe 10 Disemba 1963. Sherehe hizo zilifanyika katika mgahawa maarufu mjini Copenhagen ujulikanao kama Ankara Restaurant. Mbali ya wazawa wa Zanzibar, walihudhuria pia wageni mbalimbali kutoka Uingereza, Poland, Uturuki na sehemu nyingine duniani kuunga mkono hafla hiyo.
Katika maadhimisho hayo, mwandishi na mtafiti wa siasa za Tanzania Ludovick Mwijage alipata nafasi ya kuhutubia hadhara hiyo kwa kuwaunga mkono Wazanzibari juu ya uamuzi wao wa kusherehekea siku hii adhimu. Pamoja na mambo mengine, Mwijage amewashajiisha Wazanzibari kuendelea kuikumbuka siku hii kwani ni siku muhimu sana katika historia ya visiwa vya Zanzibar.
Kamati ya maandalizi ya sherehe za kumbukumbu ya siku ya Uhuru wa Zanzibar inapenda kuwashukuru wote waliohudhuria katika hafla hiyo pamoja na wale waliochangia kwa hali na/au mali kufanikisha siku hii.
Kamati maalum,
11 Disemba 2011
Copenhagen
 
Kuna watu Kwa makusudi wanataka kukiaminisha kizazi hiki kuwa mapinduzi ya January 1964 ndio siku ya uhuru
 
Je, Wazanzibari wenyewe wanasemaje kuhusu hili? Kama wanaunga mkono kwa nini walazimishwe vinginevyo? Kwa manufaa ya nani?
 
Kumbe zanzibar ilikuwa nchi.

Hata sasa hivi 2018 Zanzibar ni nchi, ina katiba yake, ina bunge, ina wimbo wao wa taifa la Zanzibar, ina mawaziri, ina Rais Dr Shein tena Mpemba, ina wimbo wao wa Taifa, na kadhalika! Nchi ya Zanzibar
imeungana na nchi ya Tanganyika kuunda Tanzania! Historia fupi.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom