Sherehe za miaka 50 JMt, bila kumbkumbu hata ya kupanda mti!

Mwikimbi

JF-Expert Member
Mar 8, 2008
1,762
825
watanzania walipa kodi bila shaka sasa wanaugulia maumivu ya mabilioni yaliyotumika katika kilele cha sherehe za muungano, ni kweli sherehe zilifanya sana, acha vifaru, jwtz ilirudisha heshima yake kwa kuanika wazi silaha zetu za kivita, tumefaulu kuwapasha wale tunaowaita majirani wenye chokochoko akina banda na kagame


ni kweli ni sherehe nzuri , hata hivyo hakuna kumbukumbu itakayosalia baada ya sherehe hizi, leo nimeshuhudia lowloader za jeshi zikiwa mororgoro road kwenda kurudisha vile vifaru ngerengere, na huko mjini vijana wako busy wakibandua yale mabango! wiki mbili kuanzia leo labda kumbukumbu itabaki kuwa ni picha

tunaweza kujifunza kutoka afrika kusini katika kusherekea miaka 75 ya ANC walijenga na kuzindua Guntram train , treni ya umeme inayoenda kwa kasi kati ya johansburg na pretoria

tungeweza hata kutenga bilioni 50 tukajenga ile flyover ya ubungo na nyingine kule zanzibar na tukazindua siku ya muungano tukayaita haya madaraja kuwa muungano bridge ingebaki kumbukumbu ya kudumu, sasa tumetumia nasikia 76 bilioni na hakuna kumbukumbu yoyote zaidi ya mbwembwe za kuonyesha vifaru.

kama yote yangeshindikana basi tungeotesha miti ya muungano
 
Tangu nimeanza kusoma mada za watu hii nayo ni mada ya aina yake ni zaidi ya kituko katika utaifa wako wewe umewahi kupanda miti mingapi.

suala la kupanda miti unataka kiongozi aje kuhamasiaha kupanda miti wakati wenzako kila tukijisikia kupand miti na kufanya kazi za kijamii tunafanya bila kusukumwa.

kwa jinsi mawazo yako yalivyo siku moja utaomba kusukumwa hata kwenye majukumu ya kifamilia yanayokuhusu wewe binafai.
 
Tangu nimeanza kusoma mada za watu hii nayo ni mada ya aina yake ni zaidi ya kituko katika utaifa wako wewe umewahi kupanda miti mingapi.

suala la kupanda miti unataka kiongozi aje kuhamasiaha kupanda miti wakati wenzako kila tukijisikia kupand miti na kufanya kazi za kijamii tunafanya bila kusukumwa.
wakti mwingine wehu ni wengi kuotesha miti kulinda mazingira ni jambo moja ila kuotesha miti kwa ajili ya kumbukumbu ni tofauti

kwa jinsi mawazo yako yalivyo siku moja utaomba kusukumwa hata kwenye majukumu ya kifamilia yanayokuhusu wewe binafai.
acha wehu soma mada yote
 
Ni wazo zuri sana mkuu..tunataka mawazo chanya kama haya ili nchi iendelee
 
Back
Top Bottom