Shemeji yangu tabia yako inanikera sana, nitakuchomolea betri kwa Bro, niache nijikongoje upo hatua mia mbele yangu

Nipe namba ya shemu wako ntakua nampa na yakutolea...
Hizi ni salamu kwa watu wote wenye tabia hizi, reference ni shemeji yangu.

Shemeji yangu tabia yako ya kunipiga vizinga vya mara kwa mara inanikera sana, inanirudisha nyuma.

Wewe una ajira yako, mumeo ana ajira riziki kwenu sio shida, maisha yako/yenu sio shida. Tayari mshajenga na mumeo kashapata hadi kipando/gari la kutembelea.

Sina hakika kama bro anashindwa kutimiza wajibu wake wa kuhudumia familia ikiwemo mahitaji yako binafsi.

Siku za mwanzo nilizani ni shida tu ya ghafla na hukuwa na jinsi ukaamua kuniomba assist na bila hiyana nikakusave, ila kauli ambayo sikuielewa ni pale uniponiambia "hii inatakiwa iwe siri yetu" ili mumeo asijue kuwa unaombaga assist ukiwa na shida zako binafsi. Kwa kuwa sikujua dhamira yako nilikubaliana na kauli hiyo.

Vizinga vyako hivi vinanirudisha nyuma sana, tena huna haya unaomba na ya kutolea.

Nilitarajia watu wa karibu yangu kama wewe uwe unanishauri namna ya kusave na mbinu za kuongeza kipato badala ya kutegemea malipo ya malipo ya vibarua pekee ila imekuwa tofauti na ndio kwanza umepata mteremko wa kutatua shida zako binafsi ambazo kimsingi zinakuwa nje na bajeti yako ya kila siku ambayo jukumu la mumeo kuitekeleza na nina imani anaitekelza ipasavyo.

Nipumzishe shemu wangu na mimi nijikongoje, ulipofikia wewe ni mbali mimi bado nipo mwanzo.
 
Be a man mface sio unalia lia halafu chemba
Hapa nafikisha ujumbe kwenye jamii japo unaona nalia lia, hii tabia ipo katika jamii, tukijadili hapa kwa pamoja na tukipata utatuzi tutakuwa tumesaidia watu wengi.

Sawa ahsante kwa ushauri ngoja nijitahidi kutafakari namna ya kumfungukia ili kuepuka au kupunguza madhara yatakyojitokeza baada ya hapo
 
Kamchane live huyo shemeji yako kisha ndio uje uwachane hawa usiowaona wala kuwafahamu
huwezi jua huenda yupo humu, kumbuka JF inatumiwa kwa siri sana kuliko mitandao mingine ya kijamii
 
Kwa hapo mlikofikia mkuu ni bora kumchana ukweli ila ukiona anazingua basi mwambie tu ndug yako ili kesho asianze ulikuwa unamtaka ndo ukawa unampa pesa kumnasa....
sawa mkuu, kinachonishangaza sana, anaonekana mtu poa sana katika jamii ila hii tabia yake nimemshusha sana CV ukilinganisha na wengine wanavyomchukulia.

Bro ni mtu mwema sana na tena mwenye hofu ya Mungu kulingana na Imani, jambo ambalo linamfanya aweze kutimiza majukumu ya familia yake ipasavyo ila mke wake ndio amenishangaza, kwa nini anakuwa hivi ikizingatia na yeye ana kipato chake japo sio kikubwa kivile kulingana na kazi yake.

Ngoja nijikaze nitumbue hili jibu maana hatua aliyofikia imekuwa kero sana
 
Na
Hizi ni salamu kwa watu wote wenye tabia hizi, reference ni shemeji yangu.

Shemeji yangu tabia yako ya kunipiga vizinga vya mara kwa mara inanikera sana, inanirudisha nyuma.

Wewe una ajira yako, mumeo ana ajira riziki kwenu sio shida, maisha yako/yenu sio shida. Tayari mshajenga na mumeo kashapata hadi kipando/gari la kutembelea.

Sina hakika kama bro anashindwa kutimiza wajibu wake wa kuhudumia familia ikiwemo mahitaji yako binafsi.

Siku za mwanzo nilizani ni shida tu ya ghafla na hukuwa na jinsi ukaamua kuniomba assist na bila hiyana nikakusave, ila kauli ambayo sikuielewa ni pale uniponiambia "hii inatakiwa iwe siri yetu" ili mumeo asijue kuwa unaombaga assist ukiwa na shida zako binafsi. Kwa kuwa sikujua dhamira yako nilikubaliana na kauli hiyo.

Vizinga vyako hivi vinanirudisha nyuma sana, tena huna haya unaomba na ya kutolea.

Nilitarajia watu wa karibu yangu kama wewe uwe unanishauri namna ya kusave na mbinu za kuongeza kipato badala ya kutegemea malipo ya malipo ya vibarua pekee ila imekuwa tofauti na ndio kwanza umepata mteremko wa kutatua shida zako binafsi ambazo kimsingi zinakuwa nje na bajeti yako ya kila siku ambayo jukumu la mumeo kuitekeleza na nina imani anaitekelza ipasavyo.

Nipumzishe shemu wangu na mimi nijikongoje, ulipofikia wewe ni mbali mimi bado nipo mwanzo.
Na wewe muombe. Mwenyewe atajirekebisha tu. Mfano akiomba laki ukimpa kaa wk moja muombe assist ya laki 5. Akikupa kaa kidogo mpige ndui ingine. Akishindwa kukupa na yeye hawezi kuja kuomba na akiomba unamwambia nipo juu ya mawe atarudiwa na ufahamu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom