Sigara Kali
JF-Expert Member
- May 28, 2017
- 3,623
- 8,428
Wasalaam wananzengo
Ilikuwa mwaka 2016 pale nilipotembelewa na shemeji yangu ambaye wakati huo ndio alikuwa kwenye balehe maana mimi ni mtu mzima na tabia za vijana walio kwenye balehe nazijua.
Basi bhana wakati huo nami nimemtembelea wife manake tulikuwa tunaishi mikoa tofauti japo ya jirani Sana.
Sasa katika kuishi ishi pale yule shem wangu alikuwa analeta mitego ya ajabu ajabu ukizingatia ndio alikuwa ana balehe basi nahisi alikuwa anawashwa.
Sasa kwa kujenga heshima kwa dadake mi nikawa nampotezea potezea na sometimes namsifia sifia hadi pale nilipoondoka kurudi mkoani kwangu.
Huyu shemeji yangu ni mama mkubwa kwa mdogo na wife na wife alikuwa na bifu na huyo mamake mdogo, sasa baada ya huyu shemeji yangu kurudi kule Ukweni yani kwa mamake mkubwa akaanza kutangaza nimemtongoza, nimekaa nashangaa napigiwa simu na wife analalamika eti nimemtongoza mdogo wake, nikamwambia aache kutugombanisha.
Kama kweli nimemtongoza kwanini asikuambie mwenyewe wakati upo nae na mimi nilikuwepo badala yake anaondoka anaenda kutangaza kwenu.
Basi ilipofikia likizo wife akaenda kwao wakanipigia simu kuniuliza mbele ya huyo shem wangu kwanza hakuongea kitu, mi nikawapa shit kuanzia wife, mamake(mama mkwe) na huyo dogo hadi mamake dogo nikamwambia sipendi kunizushia habari za kidwanzi, nia yenu mnione mbaya ukoo wenu wote.
Sasa baada ya miaka kupitia leo nimesikia huyo shem wangu anakuja kumtembelea dadake, hapa najiuliza nimtimue asikanyage hapa kwangu(kwa sasa dadake na watoto wapo hapa mkoa ninaoishi) au nimpotezee tu nisubiri wamalize hizi sikukuu waondoke.
Manake nikikumbuka alivyonitangaza kwao alinidhalilisha Sana.
Ushauri wenu wadau.
Ilikuwa mwaka 2016 pale nilipotembelewa na shemeji yangu ambaye wakati huo ndio alikuwa kwenye balehe maana mimi ni mtu mzima na tabia za vijana walio kwenye balehe nazijua.
Basi bhana wakati huo nami nimemtembelea wife manake tulikuwa tunaishi mikoa tofauti japo ya jirani Sana.
Sasa katika kuishi ishi pale yule shem wangu alikuwa analeta mitego ya ajabu ajabu ukizingatia ndio alikuwa ana balehe basi nahisi alikuwa anawashwa.
Sasa kwa kujenga heshima kwa dadake mi nikawa nampotezea potezea na sometimes namsifia sifia hadi pale nilipoondoka kurudi mkoani kwangu.
Huyu shemeji yangu ni mama mkubwa kwa mdogo na wife na wife alikuwa na bifu na huyo mamake mdogo, sasa baada ya huyu shemeji yangu kurudi kule Ukweni yani kwa mamake mkubwa akaanza kutangaza nimemtongoza, nimekaa nashangaa napigiwa simu na wife analalamika eti nimemtongoza mdogo wake, nikamwambia aache kutugombanisha.
Kama kweli nimemtongoza kwanini asikuambie mwenyewe wakati upo nae na mimi nilikuwepo badala yake anaondoka anaenda kutangaza kwenu.
Basi ilipofikia likizo wife akaenda kwao wakanipigia simu kuniuliza mbele ya huyo shem wangu kwanza hakuongea kitu, mi nikawapa shit kuanzia wife, mamake(mama mkwe) na huyo dogo hadi mamake dogo nikamwambia sipendi kunizushia habari za kidwanzi, nia yenu mnione mbaya ukoo wenu wote.
Sasa baada ya miaka kupitia leo nimesikia huyo shem wangu anakuja kumtembelea dadake, hapa najiuliza nimtimue asikanyage hapa kwangu(kwa sasa dadake na watoto wapo hapa mkoa ninaoishi) au nimpotezee tu nisubiri wamalize hizi sikukuu waondoke.
Manake nikikumbuka alivyonitangaza kwao alinidhalilisha Sana.
Ushauri wenu wadau.