Shemeji haeleweki jamani!

minagirl

JF-Expert Member
Jan 15, 2013
269
35
Rafiki yangu kipenzi anasoma chuo flani hapa mjini, amekuwa katika mapenzi na mwanaume mmoja ambaye amekuwa haeleweki yaani utadhani ndo yahaya aliyeibwa na Jide.

Rafiki yangu anaonekana anampenda sana huyo bwana shemeji, wana kama almost miez mitatu tangu wamefahamiana, wamesex mara moja baada ya kupima na kukuta wote wazima.

Bwa she anafanya kazi katika kampuni flani hivi ila bi shost hajui ofisi ya mpenzi wake ilipo. Katika muda wote wa mahusiano mwanaume hajawah kumpeleka mwanamke nyumbani kwake wala inavyoelekea hana mpango. Mwanaume anapajua kwa bidada japo huwa sio mkaaji huenda kumchukuwa wanapokuwa na mtoko na baadae humrudisha coz shostito hana usafiri,

kimbembe kimeanza wiki mbili zilizopita, mwanaume kapotea kwenye cm hapatikani, rafiki yangu hajui ampate vp, hajabahatika kutambulishwa kwa rafiki wala ndugu yeyote wa mwanaume wala hapajui kwake, jamaa kapotea kama wki hivi, walikuwa wanamazowea ya kuchat kwenye moja ya mtandao wa kijamii nako akatoweka, akachange username kibaya zaid akaweka jina na picha ya kike.

Jana kaibuka! Kapiga cm anadai anataka waonane, rafiki yangu akamuomba amuelekeze kwake ili aende bwa she akagoma, alipoulizwa sababu za kutokupatikana jamaa akagoma kueleza kwamba mpaka waonane ila akadai alikuwa na matatizo,

baada kama ya nusu saa jamaa akafika kwa rafiki yangu tayar kwa mtoko, walienda hoteli moja nje kidogo ya mji.

Wakiwa huko mwanaume aliomba sana msamaha, alidai kapata matatizo kazini kutokana na loss aliyoiingizia kampuni kwa uzembe, alikiri kwamba pesa hiyo aliitumia na ndio amenunulia gari na vitu vingine na kwamba aliamua kuzima cm kwani mbali na kufukuzwa kazi anatafutwa kwa hatua zaid kisheria.

Rafiki yangu alimpa pole na kumshauri angalau atafute line nyingine ambayo watakuwa wakiwasiliana wao wawili tu, aliahid kufanya hivyo leo asubuhi kwani wakati huo ilikuwa tayari ni usiku.

Tangu jana usiku alipomshusha rafiki yangu getini shemeji yangu huyo hapatikani kwenye cm, hakuwahi hata kumwambia kama kafika salama.

Rafiki yangu kakosa raha, anafikiria kuachana naye ila anahofu mwanaume asimchukulie kwamba kamuacha kwa vile katimuliwa kazini.

Ameniomba ushauri ila mm kabla ya kumpa ushauri nimeona niwashaurishe wenzangu. Binafsi nimeshindwa kutoa ushauri kwani kunamaswali najiuliza sipati majibu

1.kama tatizo ni loss kazini ndo ashindwe kutafuta njia yoyote ya kuwasiliana na mpenzi wake?

2.kwa nini hataki rafiki yangu apafaham anapoishi na wala hajamtambulisha kwa ndugu wala rafiki yeyote?

3ivi inshu ya kazini ndo imefenye aweke username na pic ya kike kwenye account yake ya moja ya mtandao wa kijamii ambao alikuwa akiwasiliana na mpenzi wake? Na leo nasikia kajitoka kabisa hayumo kwenye mtandao huo, je hii ni sababu ya matatizo ya kikazi?

4. Aliahd leo atanunua line mpya kwaajili ya kuwasiliana na rafiki yangu mbona hajatekeleza? Na kwanini walipokuwa hotelin cm ilikuwa one na alikuwa akipigiwa na watu na kupokea?

Jamani nisaidieni mawazo mwenzangu coz nimejikuta navaa uhusika na kuumizwa sana na huyu mtu. Na ww shemeji kama unapita humu nakupa ujumbe ufanyavyo sio vizur kama unamambo yako ni bora umuweke wazi mwenzio na sio kumpotezea muda wake, nawasilisha.
 
Hapo huna shemeji ni majanga tu. Huyo shost yako kama hajui kusoma hata picha haoni?
 
SUTU..PID GIRL!!!!!!!!!! Peanut brain mkubwaaa! Mxiuuuuuuuuuuuu! THE GUY IS MARRIED! It doesnt even need 2 seconds to figure that out!
Hajafukuzwa kazi wala babu yake kibarua! How is she even sure the guy has a job? THE GIRL IS PATHETIC!!!!!!!!!!!!!

I ont even waste more of my precious time to rescue a LOST course! Natamani nimlambe BAKORA za reja reja hadi akilizichaji!
 
Hivi kwenye uagelifrendi na uboifrendi kuna mashemeji pia!!! ngoja nishangae hili kwanza kabla ya kuchangia mengine...
 
Mambo ya mapenzi huboa sana ukimpenda mtu asiyejua thamani ya pendo lako kwake
 
SUTU..PID GIRL!!!!!!!!!! Peanut brain mkubwaaa! Mxiuuuuuuuuuuuu! THE GUY IS MARRIED! It doesnt even need 2 seconds to figure that out!
Hajafukuzwa kazi wala babu yake kibarua! How is she even sure the guy has a job? THE GIRL IS PATHETIC!!!!!!!!!!!!!

I ont even waste more of my precious time to rescue a LOST course! Natamani nimlambe BAKORA za reja reja hadi akilizichaji!

wewe umesahau siridi yako....
Ndo akili zenyu.
 
Shemejiyo ni mume wa mtu! Bila kubishaaa!somen alama za nyakatii
 
shikamoo watu8..enzi zako hakukua na ushemeji kwenye u boyfrend na u galfrend?
Hivi kwenye uagelifrendi na
uboifrendi kuna mashemeji pia!!! ngoja nishangae hili kwanza kabla ya
kuchangia mengine...
 
Last edited by a moderator:
Headache yote ya nini? Tupa kuleee. Halafu mie hii midada ya kupenda penda hovyo na kulia imeumizwa siipendagi. Have some form of reservation. If not for missus down there then for your feelings, if not this then have the courage to keep your dignity as a woman. Surely you cannot give your all to every Tom Dick and Harry!!
 
huyo shosti wako ana ukame nn wa kutongozwa na watu wanaojielewa ndio maana anashindwa kujiongeza na kuchanganua ukweli wa mambo.sometimes exposure inasaidia jamani.
 
shikamoo watu8..enzi zako hakukua na ushemeji kwenye u boyfrend na u galfrend?

Sijawahi kusikia...zaidi sioni logic yoyote.

Ndio yale yale ya magelifrendi na maboifrendi kuitana mke au mume au mama na baba fulani...
 
Last edited by a moderator:
wewe umesahau siridi yako....
Ndo akili zenyu.

Data ulinimiss sana maana bil mimi wewe humu huvumi katu! kujue nani? Basi nimerudi and you can keep stalking me!

Back to topic! Mimi sinifananishe huyu innocent lamb! Mie najua A to Z sema nimeamua kubanana hapo hapo na kwenda sawa na mwenye mali zake, ila huyu hana hata idea what she is doing or up against! Katu usifananishe paka na chui japo wote jamii moja!
 
Headache yote ya nini? Tupa kuleee. Halafu mie hii midada ya kupenda penda hovyo na kulia imeumizwa siipendagi. Have some form of reservation. If not for missus down there then for your feelings, if not this then have the courage to keep your dignity as a woman. Surely you cannot give your all to every Tom Dick and Harry!!

mawazo yako yanauelekeo wa kulingana ni kile nilichotaka nitiririke hapa ila nimeona nitachafua page hii yatosha
 
Data ulinimiss sana maana bil mimi wewe humu huvumi katu! kujue nani? Basi nimerudi and you can keep stalking me!

Back to topic! Mimi sinifananishe huyu innocent lamb! Mie najua A to Z sema nimeamua kubanana hapo hapo na kwenda sawa na mwenye mali zake, ila huyu hana hata idea what she is doing or up against! Katu usifananishe paka na chui japo wote jamii moja!

ulirudi vyema hadi nikaanza kuku lavu...
Mara ghafla umepotoka tena...
Em tizama impact yako...mawazo potofu unayoyatotoa,..vischana vinayafurahia.
 
mwambie muhusika aje hapa jamvini kuna swali nataka kumuuliza,..
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom