Shemeji anaharibu ndoa yangu

kazikubwa

JF-Expert Member
Oct 8, 2010
598
143
Jamani mwenzenu ninamasikitiko makubwa sana. Shemeji aliyeoa dada yangu ananichukulia mke wangu, nilikuwa nasikia tu fununu siku za nyuma lakini sasa ushahidi umekuwa dhahiri. Kulipa kisasi kwake haiwezekani kwani mkewe ni dada yangu wa tumbo moja. Naogopa kuliweka wazi hili kwa sababu naona aibu kwa familia yetu.
Ndugu zangu naomba ushauri wenu katika hili, nifanyeje jamani...
 
Hiki kitu huwa kinanishangaza sana. Mkeo anatoka nje ya ndoa, wewe unamlalamikia mwanaume anayemchukua mkeo. Kwani mke wako huwa anashikiwa panga ili akubali? Kama mkeo ndo anayemtongoza shemeji yako je? Wewe shughulika na mkeo, habari za anayemchukua wewe zinakuhusu nini? Kama ukimuonya mkeo akashindwa kubadilika basi huyo si riziki kwako. Pole lakini.
 
Ukiona aibu kuliweka wazi,badae itakula kwako..huyo shem ni fisi tu,c vinginevyo.
 
Kwa nini ulipe kisasi kwa kutembea na mkewe hata kama siyo dada yako? Unajua kwa ukiwembe wake yupo salama? Kaa na mkeo, kama unaushahidi wa kutosha mwambie kuwa umegundua nyendo zao na mpe ushahidi.
Ndo maana wengine hawataki video camera, wanataka picha za mnato.
 
kha!"! umegegedewa mke wako aibu!!! jamaa janja kweli alijua huwezi mgegeda dada yako. mwekee tego mke wako ili wanase alafu unamkataa dushelele lake
au tafuta wajanja mjini wamtigorize
 
hey umetoka ulimwengu upi??? Acha kujisononesha wewe......wewe ongea na mkeo umrudishe kwao pengine mapenzi yamepungua kwako
 
Mkuu kazikubwa, Pole kwa masikitiko na mkasa mzima.

Lakini, ulifanya nini pale ulipopata fununu, kabla ya kuwa dhahiri?Ushahidi umekuwa dhahiri kwa nani?..Sidhani kama ni busara kulipa kisasi(kwa jambo lolote), maana hata ukifanya hivyo huondoi tatizo.

Nadhani, ninaunga mkono kama Lukolo alivyosema, Haina haja ya kuanza kusolve tatizo kwa shemeji wako.Hukumuoa shemeji, mambo ya ndani hutatuliwa kwa kuanzia huko huko, ongea na mkeo kujua tatizo liko wapi, kisha unaweza kuendelea na shemeji wako.

Sijaelewa unaposema ni aibu kwa familia, na wakati huo huo unasema sasa mambo ni dhahiri(ushahidi)! Inawezekana unaogopa kueleza wanafamilia lakini wao pia wanajua kwakuwa mambo tayari ni dhahiri!

Mshirikishe MUNGU.
 
Last edited by a moderator:
Kama ushahidi unao wa kutosha, achana na huyo mke wako, ila inabidi umwambie huyo shemeji yako ukweli wa mambo kwamba wewe unajua kila kitu kinachoendelea.
 
Huyo shemeji yako nahisi atakuwa na pesa na tabia za unyama unyama....wengi wenye hizo skando nawajua...unakuta anaonekana Mungu mtu ukweni basi analamba kuanzia mke alomuoa wadogo zake na dada zake na yeyote mwenye jinsia ya kike anayekatiza....kwa ufupi atamaliza ukoo na wenye uhusiano na huo ukoo....peleka kwao huyo mke mtakufa ukoo mzima.

Kuna jirani zetu fulani walipukutika kwa sababu ya kula na shemeji alokuwa na pesa za kumwaga...na wengine wanaendelea kuchongeka...shemeji alikuwa ana finance familia nzima huku anajisevia. Wife na watoto wote weshakufa kwani inaonekana alioa akiwa tayari positive...mashemeji nao wanaondoka mmoja baada ya mwingine.
 
Shemeji nae, yaani kakuolea dadako bado kamlamba na mkeo?

Kwanza ongea na mkeo, ukamnye na umuonyeshe huo ushahidi ulionao au wakutanishe wote mkeo na shemeji uwape vidonge vyao wasipoacha tabia yao, nakushauri umrudishe mkeo kwao akafundwe upya
 
uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii ukimwi uliwekwa pabaya(source mzee ruksa) tutakwisha! UNANGOJA NINI KUMUACHA HUYO MWANAMKE?? NGOJA USIKIE KALALA NA MZAZI WAKO, NDIYO LABDA FAHAMU ZITAKURUDIA!
 
kazikubwa, pole sana kwa matatizo. However, mara nyingi kwenye maswala kama haya, mhusika mara nyingi ndio anakuwaga wa mwisho kujua yanayoendelea. Meaning, kama ni aibu, hio tayari ipo...na kuna uwezekano mkubwa kuwa baadhi ya ndugu wanalifahamu hili. Niungane tu na waliokushauri kulijadili hili swala na mkeo.
 
Last edited by a moderator:
Wewe ogopa kuiabisha familia...AKULETEENI UKIMWI WEWE NA DADA YAKO... Familia yako itakuwa imepata heshima kubwa mtu na dada yake kupata ngoma. HAPO NI KAMA ANAWAB*#*DUA WEWE NA DADA YAKO... Ungekuwa karibu ningekupigz bonge la m'kibao
 
Jamani mwenzenu ninamasikitiko makubwa sana. Shemeji aliyeoa dada yangu ananichukulia mke wangu, nilikuwa nasikia tu fununu siku za nyuma lakini sasa ushahidi umekuwa dhahiri. Kulipa kisasi kwake haiwezekani kwani mkewe ni dada yangu wa tumbo moja. Naogopa kuliweka wazi hili kwa sababu naona aibu kwa familia yetu.
Ndugu zangu naomba ushauri wenu katika hili, nifanyeje jamani...
HEHEHEHEEE,yaani unaogopa kusema,na ukimwi je?embu kuwa mwanaume wa ukweli wewe.
 
Mkuu pole sana na hilo lililokupata, chamsingi hapo kama suala linaukweli wowote, tumia hekima ya hali yajuu. Mosi, mkeo kashindwa kuilinda heshima yako; Pili mkeo kavunja uaminifu kwakutembea na shemeji yako hiyo nidharau kubwa sana pia nakupongeza kwa uvumilivu, ingekuwa mimi tungekuwa tunaongea mengine sasahivi. Tatu nadhani mkeo hana malezi ya kutosha toka kwao ndomaana anadiriki kukuvunjia heshima kiasi hicho. Nini kifanyike? Ili kuepuka fedheha na kama haya unayo yaongea yanaukweli wowote, huyo mwanamke safiri nae mpaka kwao mkiwa na zawadi kedekede kwaajili ya wazazi, mkifika kule lala sikumoja kesho yake asubuhi kabla hawajatawanyika kwenda kwenyemihangaiko, waambie unataka kuwaona kwa dakika tano, wakiridhia waambie nia na madhumuni ya kuja nikwaajili ya kuwakabidhi binti yao asiye na adabu, taja vyote ambavyo amekufanyia. Baada ya hapo rudi kwako na kisha uende angaza kucheki afya kama itakuwa fiti. Kama upo safi subiri, Mwenzi wako anakuja na yule ulibugi tu. Kila la heri!!
 
Nahis na wewe unatatizo, yani unajua alafu et naogopa? ahha! kweli mungu aliumba watu mzungu akatengeneza viatu...yaan, yaani mimi shemeji, ah, shemeji alieoa kwenu akulie na mkeo..

Nahic huyo shemeji yako ana mapesa na familia yenu inamtegemea, na wewe ni kabwela tu..ndo maana wamuogopa (ninahic) hata kama ni hivyo wewe ni mwanaume (nakushauri sasa) kama unaushaidi kabisa

ita dada yako, mkeo na shemeji yako weka chini, anza kumwaga mchele kuku wale yaan wambie kila kitu (onyo) akikisha unaushaidi wa kutosha).

kwa mkristo kosa la zinaa linaacha mke! epuka matapeli nyumba ya kishimo haichangiwi...PIGA CHINI C MKE HUYO BORA LAWAMA KULIKO FEDHEA
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom