Rugemeleza
JF-Expert Member
- Oct 26, 2009
- 668
- 136
Nadhani mnaendelea kufuatilia kwa makini jinsi gazeti la Guardian la Uingereza linavyozidi kutuhabarisha jinsi nyaraka za kibalozi za Marekani zinavyosema kuhusu nchi mbalimbali. Moja ya habari iliyonigusa ni ile inayozungumzia jinsi Kampuni ya Shell ilivyopenyeza watu wake katika kila idara na ofisi ya serikali ya Nigeria. WikiLeaks cables: Shell's grip on Nigerian state revealed | Business | The Guardian
Hii imenifanya nami niwaze na kuwazua jinsi ambavyo kampuni za madini zilivyojipenyeza na kuweka watu wao katika idara na wizara nyeti nchini mwetu. Vilevile zina watu wenye uhusiano na viongozi na mawaziri wa serikali wanaohusika na madini na sekta nyingine muhimu. Ukisikiliza kauli za viongozi hao utaona jinsi wanavyotetea mikataba ya shanga ambayo nchi yetu imesaini. Tunatakiwa tuamke na tupinge vitendo hivyo na haki ya nchi yetu katika raslimali zake.
Hii imenifanya nami niwaze na kuwazua jinsi ambavyo kampuni za madini zilivyojipenyeza na kuweka watu wao katika idara na wizara nyeti nchini mwetu. Vilevile zina watu wenye uhusiano na viongozi na mawaziri wa serikali wanaohusika na madini na sekta nyingine muhimu. Ukisikiliza kauli za viongozi hao utaona jinsi wanavyotetea mikataba ya shanga ambayo nchi yetu imesaini. Tunatakiwa tuamke na tupinge vitendo hivyo na haki ya nchi yetu katika raslimali zake.