Shell ilivyoimiiki Nigeria, Je si ndivyo ilivyo kwa Tanzania?

Rugemeleza

JF-Expert Member
Oct 26, 2009
668
136
Nadhani mnaendelea kufuatilia kwa makini jinsi gazeti la Guardian la Uingereza linavyozidi kutuhabarisha jinsi nyaraka za kibalozi za Marekani zinavyosema kuhusu nchi mbalimbali. Moja ya habari iliyonigusa ni ile inayozungumzia jinsi Kampuni ya Shell ilivyopenyeza watu wake katika kila idara na ofisi ya serikali ya Nigeria. WikiLeaks cables: Shell's grip on Nigerian state revealed | Business | The Guardian

Hii imenifanya nami niwaze na kuwazua jinsi ambavyo kampuni za madini zilivyojipenyeza na kuweka watu wao katika idara na wizara nyeti nchini mwetu. Vilevile zina watu wenye uhusiano na viongozi na mawaziri wa serikali wanaohusika na madini na sekta nyingine muhimu. Ukisikiliza kauli za viongozi hao utaona jinsi wanavyotetea mikataba ya shanga ambayo nchi yetu imesaini. Tunatakiwa tuamke na tupinge vitendo hivyo na haki ya nchi yetu katika raslimali zake.
 
Nadhani mnaendelea kufuatilia kwa makini jinsi gazeti la Guardian la Uingereza linavyozidi kutuhabarisha jinsi nyaraka za kibalozi za Marekani zinavyosema kuhusu nchi mbalimbali. Moja ya habari iliyonigusa ni ile inayozungumzia jinsi Kampuni ya Shell ilivyopenyeza watu wake katika kila idara na ofisi ya serikali ya Nigeria. WikiLeaks cables: Shell's grip on Nigerian state revealed | Business | The Guardian

Hii imenifanya nami niwaze na kuwazua jinsi ambavyo kampuni za madini zilivyojipenyeza na kuweka watu wao katika idara na wizara nyeti nchini mwetu. Vilevile zina watu wenye uhusiano na viongozi na mawaziri wa serikali wanaohusika na madini na sekta nyingine muhimu. Ukisikiliza kauli za viongozi hao utaona jinsi wanavyotetea mikataba ya shanga ambayo nchi yetu imesaini. Tunatakiwa tuamke na tupinge vitendo hivyo na haki ya nchi yetu katika raslimali zake.


Unge......chagua CHADEMA mkuu hayo yote yangewezekana ila CCM mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh
 
Rugemeleza,
Kampuni za madini, hasa Barrick, haina haja ya kupenyeza watu wake katika idara mbalimbali kwa sababu wanajua kuwa mkuu wa nchi tayari yumo mfukoni mwao. Wakati wa zoezi la majadiliano ya tume ya Bomani, Sinclair, huyu ni CEO wa Barrick, aliwaandikia wana hisa wake kuwa hakuna litakalobadilika. Alikuwa ameshapewa rasimu ya mapendekezo ya tume ya Bomani hata kabla ya wabunge wetu kuyaona. Kuna wakati nilipata habari kuwa Sinclair alipokuwa Dar-es- Salaam alifanya kikao katika Ikulu pamoja na Kikwete na Joseph Kahama. Barrick wataendelea kupeta chini ya uongozi wa Kikwete.
 
Back
Top Bottom