Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
na Hellen Ngoromera
MNAJIMU Mashuhuri wa Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein, amemtabiria Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk. Willbrod Slaa kukaa pamoja.
Kutokana na hali hiyo, Sheikh Yahya ameitaka jamii kuvuta subira kwani watapata habari njema kuhusu viongozi hao hivi karibuni.
Mnajimu huyo alitoa utabiri huo juzi usiku jijini Dar es Salaam wakati akizungumza katika kipindi cha Nyota Zenu kinachorushwa hewani na Channel ten.
"Namsalimu rais mpendwa Kikwete, namsalimu Dk. Slaa kwa kuonyesha juhudi zake katika kuleta amani, kinyota nawaona Dk. Slaa namwona Rais Kikwete wanapeana mikono, nawaona watakuwa pamoja," alisema Sheikh Yahya.
Aliongeza kuwa kinyota anawaona pia Rais Kikwete na Dk. Slaa na wenzake kuwa watakaa pamoja na kula pamoja.
Alitabiri pia kuwa CHADEMA kushirikiana na CCM pamoja na Chama cha Wananchi (CUF) na kueleza kuwa Mungu ndivyo anavyotaka.
Sheikh huyo aliweka wazi kuwa kuanzia Februari 18 mwakani, CHADEMA na Chama cha Mapinduzi (CCM) wataelewana vilivyo lakini amani kubwa itakapatikana Novemba 21 mwakani.
Aliwataka wananchi kuacha mambo aliyoyaita ya kipuuzi na kuwaambia wavute subira kwani Mwenyezi Mungu anatawala kupitia uchaguzi.
MNAJIMU Mashuhuri wa Afrika Mashariki na Kati, Sheikh Yahya Hussein, amemtabiria Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk. Willbrod Slaa kukaa pamoja.
Kutokana na hali hiyo, Sheikh Yahya ameitaka jamii kuvuta subira kwani watapata habari njema kuhusu viongozi hao hivi karibuni.
Mnajimu huyo alitoa utabiri huo juzi usiku jijini Dar es Salaam wakati akizungumza katika kipindi cha Nyota Zenu kinachorushwa hewani na Channel ten.
"Namsalimu rais mpendwa Kikwete, namsalimu Dk. Slaa kwa kuonyesha juhudi zake katika kuleta amani, kinyota nawaona Dk. Slaa namwona Rais Kikwete wanapeana mikono, nawaona watakuwa pamoja," alisema Sheikh Yahya.
Aliongeza kuwa kinyota anawaona pia Rais Kikwete na Dk. Slaa na wenzake kuwa watakaa pamoja na kula pamoja.
Alitabiri pia kuwa CHADEMA kushirikiana na CCM pamoja na Chama cha Wananchi (CUF) na kueleza kuwa Mungu ndivyo anavyotaka.
Sheikh huyo aliweka wazi kuwa kuanzia Februari 18 mwakani, CHADEMA na Chama cha Mapinduzi (CCM) wataelewana vilivyo lakini amani kubwa itakapatikana Novemba 21 mwakani.
Aliwataka wananchi kuacha mambo aliyoyaita ya kipuuzi na kuwaambia wavute subira kwani Mwenyezi Mungu anatawala kupitia uchaguzi.